Lema 'aichana' Idara ya Usalama wa Taifa

Lema 'aichana' Idara ya Usalama wa Taifa

Status
Not open for further replies.
"Wao wanapesa! Sisi tuna Mungu"!! Niko Igunga hakika kitaeleweka!!!
 
Natilia sana mashaka umakini wa huyu mheshimiwa, hasa pale anapotaka kulinganisha TZ na Libya au waTZ na walibya nadhani atakuwa anafanya makosa makubwa sana kama si kujidangaya. Niangalizo tu.

Wewe endelea kutilia mashaka umakini wake,uta-prove umakini wake baada ya utawala wa JK kung'olewa na watu kama nyinyi ndio tutawatafuta,vibaraka wa chama cha magamba na serikali yake...
 
Naona huu sasa ni usalama wa waliowateua!
 
LOL. kama mambo yako hivi inatisha! Uchunguzi ufanyike na Kamati ya Bunge
 
Wewe ndiyo Duwanzi mwenye ganzi usiyeumia au una hisa katika mateso yetu.
Kama huna hoja nyamaza au acha upuuzi.

Hivi nikuulize kuwa na hoja maana yake ni kuwa na mitizamo sawa? Tafakari halafu jaza mwenyewe nani duwazi, mpuuzi nk. kati yangu mie na wewe?
 
Niliwahi kuwambieni kwamba ukombozi wa kweli wa taifa hili UTAANZIA ARUSHA na kusambaa kama moto wa Msitu wa Amzon kote nchini na kumbe hatukuelewana vema.

Muda u karibu sana na yeyote atakayepoteza muda kufukuzia nyuma viongozi wa CHADEMA huku wakiendelea kukalia UONEVU wa dhahiri pale, naona dakika zinatoweka kwa kasi mno.

Jua la Dikteta Gaddafi huenda LIKAZAMA KWA PAMOJA na mikoloni mieusi hawa tulionao madarakani hivi sasa wasiosikia cha mtu hawa.

Jama mbwa koko(WALAZWAHOI) kafukuzwa sana kiuonevu sasa kafikia ukutani; mwenye kumkabili saana kwa ufisadi na hali ngumu ya maisha bora ujiandae kujdiliana leo au tusijadili katu tena sakata la AArusha.
 
Ninaona tunazidi kuchelewa. Wanaendelea kupima umma kama wanaweza kujibu.
 
Tanzania hii ina wenyewe, wazalendo wa kweli ambao hatuko tayari kuona inachezewa.
Wana-Arusha tumechoshwa na vitisho na pumba za huyu Mbunge. Thubutu kulianzisha uone jinsi wananchi watakavyoungana na vyombo vya dola kuwaweka sawa. Hatujasahau jinsi wewe na wasanii wenzako mlivyosababisha watu kufa na baadaye kutumia maiti zao kujinadi kisiasa. Hamtapata nafasi nyingine ya kufanya huo ufedhuli.

  • Tuacheni tuchape kazi tujenge nchi yetu, Hatuna muda wa kupoteza vijiweni kama machalii na masela wako.
  • Ngebe za kisiasa zisubiri 2016.

Mkuu yaani hujui hata uchaguzi ujao utakuwa lini!!!? Au mmepanga kuusogeza mbele uchaguzi? halafu watu kukaa kijiweni sio kama wanapenda ila hawajaandaliwa mazingira ya kazi, Sawa ndugu kwa kuwa na kazi nzuri mpaka kuwadhalrau walio kijiweni. Lakini usisahau hali hii imesababishwa nani, sidhani kama kuna mzazi anayependa kuona mwanae yupoyupo tu... OLE WAO WANAOCHEKA SASA.
 
Hapo kwenye red (maneno yako) kwa hali ilivyo hapa tanzania chama kama cdm kinatakiwa kiwe na military wing yake au la? maana yake ccm its seems wanazo tayari sasa nyie mnasubiri nini?

Hapa unamuuliza nani hasa wewe?. Nani kakwambia mimi CHADEMA?, si wote wanaopinga udhalimu wa CCM ni CHADEMA au wapinzani. Wapo CCM ndani ya chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi na wapo wasiokuwa ma chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi. Mwaka 1992 tuliporudisha mfumo wa vyama vingi, wakati Tanzania ilipokuwa na viongozi wanaofikiria wananchi zaidi ya matumbo yao na familia zao kama Mwl Nyerere walilisemea hili la kuambatanisha siasa na vyombo vya usalama. Unapokuwa na watu waliokabidhiwa dhamana ya kulinda raia na mipaka ya nchi kwa mujibu wa katiba kuwa mashabiki wa siasa unajenga mazingira ya kulipua nchi, wananchi watakapokata tamaa na vyombo hivi.

Kwa kuwa leo hii nchi inashikiliwa na genge la watu waliojimbikizia mali kifisadi na wanahitaji kulindwa na mkono wa sheria, matokeo yake wanavunja katiba kwa masilahi binafsi. Hakuna haja ya CDM wala chama chochote cha upinzani kuwa na armed wing, Armed wing ni PUBLIC TRUST, siku wakisema wananchi NO tunataka kuongozwa na X badala ya CCM, maghala ya risasi yataisha na bado hawatarudi nyuma.

Hakuna kitu kibaya kama kupoteza public trust, na kwa hili serikali ya CCM imefanikiwa sana. Hakuna mtanzania leo hii anayeiamini mahakama, polisi, Usalama wa taifa, na hivi karibuni Shimbo alipeleka shombo hiyo JWTZ japo walimdhibiti na kuminimise damage. Huwezi jenga Public trust kwa oppression or aggression, wananchi hawapaswi kuwaogopa au kuwachukia Polisi, au TISS, Tume ya uchaguzi au mahakama, bali wanapaswa kuwaheshimu na kuwaamini. Unapotumia vyombo hivi kisiasa kwa masilahi yako si tu vinakusaidia kubakia madarakani bali vinakufanya uongoze watu wasikuwa na imani nawe na kuvifanya vyombo vya dola kuonekana kandamizi badala ya saidizi kwa wananchi.
 
Hapa unamuuliza nani hasa wewe?. Nani kakwambia mimi CHADEMA?, si wote wanaopinga udhalimu wa CCM ni CHADEMA au wapinzani. Wapo CCM ndani ya chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi na wapo wasiokuwa ma chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi. Mwaka 1992 tuliporudisha mfumo wa vyama vingi, wakati Tanzania ilipokuwa na viongozi wanaofikiria wananchi zaidi ya matumbo yao na familia zao kama Mwl Nyerere walilisemea hili la kuambatanisha siasa na vyombo vya usalama. Unapokuwa na watu waliokabidhiwa dhamana ya kulinda raia na mipaka ya nchi kwa mujibu wa katiba kuwa mashabiki wa siasa unajenga mazingira ya kulipua nchi, wananchi watakapokata tamaa na vyombo hivi.

Kwa kuwa leo hii nchi inashikiliwa na genge la watu waliojimbikizia mali kifisadi na wanahitaji kulindwa na mkono wa sheria, matokeo yake wanavunja katiba kwa masilahi binafsi. Hakuna haja ya CDM wala chama chochote cha upinzani kuwa na armed wing, Armed wing ni PUBLIC TRUST, siku wakisema wananchi NO tunataka kuongozwa na X badala ya CCM, maghala ya risasi yataisha na bado hawatarudi nyuma.

Hakuna kitu kibaya kama kupoteza public trust, na kwa hili serikali ya CCM imefanikiwa sana. Hakuna mtanzania leo hii anayeiamini mahakama, polisi, Usalama wa taifa, na hivi karibuni Shimbo alipeleka shombo hiyo JWTZ japo walimdhibiti na kuminimise damage. Huwezi jenga Public trust kwa oppression or aggression, wananchi hawapaswi kuwaogopa au kuwachukia Polisi, au TISS, Tume ya uchaguzi au mahakama, bali wanapaswa kuwaheshimu na kuwaamini. Unapotumia vyombo hivi kisiasa kwa masilahi yako si tu vinakusaidia kubakia madarakani bali vinakufanya uongoze watu wasikuwa na imani nawe na kuvifanya vyombo vya dola kuonekana kandamizi badala ya saidizi kwa wananchi.

Well said, Muda si mrefu bomu litalipuka na mafisadi wote wataangamia kama Tunisia, Misri na Libya
 
Hawana jipya Usalama wa Taifa wa bongo, tunawajua kazi yao kushinda bar na kujigamba, 'unanijua mimi?', Masaburi tu!

ha ha ha ha ha ha! yaani hapa ndo nimecheka hadi baasi, ndo walivyo,
 
UWT yanayoendelea Arusha sio sifa nzuri kwa chombo hicho,jamani UWT angalieni shilingi ikilushwa juu yaweza kudondokea kichwa au mwenge.Wana UWT ni vyema mkalinda Nchi na si watu.Ni vyema nyie mkawa marefalii kuangalia na kulusha shilingi na itakako dondokea nyie kwenu ni sawa tu.Kwa kuwa kama nyie hamta tenda haki nani atatenda haki hiyo kwa Watanzania hawa maskini wa Taifa hili.

Ifike sehemu UWT wajue kuwa Taifa ni la CCM na Taifa nila CHADEMA pia,na ni Taifa la vyama vingine na si kuwa Taifa hili ni Mali ya CCM pekee tu.Ni aibu kuwa mambo ya UWT yanasikika katika upande wa kubomoa na si kujenga,huyo anae sababisha mtafaruku huo na Wanaarusha awekwe kando kuondoa uchafuaji wa idara hiyo muhimu kwa Taifa hili.Ifike sehemu good thinkers wawepo kutathimini maaamuzi dhalimu yenye nia mbaya ya kuibua chuki dhidi ya idara hiyo na umma wa Watanzania.
 
Hapa unamuuliza nani hasa wewe?. Nani kakwambia mimi CHADEMA?, si wote wanaopinga udhalimu wa CCM ni CHADEMA au wapinzani. Wapo CCM ndani ya chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi na wapo wasiokuwa ma chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi. Mwaka 1992 tuliporudisha mfumo wa vyama vingi, wakati Tanzania ilipokuwa na viongozi wanaofikiria wananchi zaidi ya matumbo yao na familia zao kama Mwl Nyerere walilisemea hili la kuambatanisha siasa na vyombo vya usalama. Unapokuwa na watu waliokabidhiwa dhamana ya kulinda raia na mipaka ya nchi kwa mujibu wa katiba kuwa mashabiki wa siasa unajenga mazingira ya kulipua nchi, wananchi watakapokata tamaa na vyombo hivi.

Kwa kuwa leo hii nchi inashikiliwa na genge la watu waliojimbikizia mali kifisadi na wanahitaji kulindwa na mkono wa sheria, matokeo yake wanavunja katiba kwa masilahi binafsi. Hakuna haja ya CDM wala chama chochote cha upinzani kuwa na armed wing, Armed wing ni PUBLIC TRUST, siku wakisema wananchi NO tunataka kuongozwa na X badala ya CCM, maghala ya risasi yataisha na bado hawatarudi nyuma.

Hakuna kitu kibaya kama kupoteza public trust, na kwa hili serikali ya CCM imefanikiwa sana. Hakuna mtanzania leo hii anayeiamini mahakama, polisi, Usalama wa taifa, na hivi karibuni Shimbo alipeleka shombo hiyo JWTZ japo walimdhibiti na kuminimise damage. Huwezi jenga Public trust kwa oppression or aggression, wananchi hawapaswi kuwaogopa au kuwachukia Polisi, au TISS, Tume ya uchaguzi au mahakama, bali wanapaswa kuwaheshimu na kuwaamini. Unapotumia vyombo hivi kisiasa kwa masilahi yako si tu vinakusaidia kubakia madarakani bali vinakufanya uongoze watu wasikuwa na imani nawe na kuvifanya vyombo vya dola kuonekana kandamizi badala ya saidizi kwa wananchi.

Nilikuuliza wewe ndio sababu nilinukuu maandishi yako. Bado nakuliza tena hivi vyombo vya usalama vilivyoko vinatumiwa na ccm na kwa maneno yako vinapoteza public trust. Je huoni ni wakati muafaka kwa vyama vya saisa ikiwemo cdm kuanzisha military wings zao. Hivi vilivyoko nivya ccm na kwa manufaa ya ccm. Au nikuulize hivi kifanyike nini ili vyombo hivi virudishe hiyo public trust ambayo vimeipoteza.
 
Waachaeni wafanye kazi zao, nchi hii ya utawala wa sheria
Hata Libya na Tunisia imewahi kudhaniwa kuwa ni nchi ya utawala wa sheria, kwa kifupi tuliosoma Sheria katika vyuo vya sheria kubambikiwa kesi si utawala wa sheria kama unadhani CCM inachofanya ni utawala wa sheria basi una muda mfupi wa kuamini katika hilo potofu nunaloliamini
 
Nilikuuliza wewe ndio sababu nilinukuu maandishi yako. Bado nakuliza tena hivi vyombo vya usalama vilivyoko vinatumiwa na ccm na kwa maneno yako vinapoteza public trust. Je huoni ni wakati muafaka kwa vyama vya saisa ikiwemo cdm kuanzisha military wings zao. Hivi vilivyoko nivya ccm na kwa manufaa ya ccm. Au nikuulize hivi kifanyike nini ili vyombo hivi virudishe hiyo public trust ambayo vimeipoteza.
Nini cha kufanya sheria za nchi zipo wazi kabisa kama huelewi rejea katiba jeshi halipaswi kuwa na mfungamano na na chama chochote cha siasa,ila CCM wanakiuka kama wanavyafanya ila kwa kifupi wanaitengenezea nchi JENEZA.
 
Anaitwa nani huyo Msaidizi wa Mkuu wa Usalama wa Taifa, Arusha tuanze naye yeye kwanza?
Hakuna haja ya jina la huyo msaidizi kwani cheo kiko wazi kabisa kama kuna hatua yoyote ya manufaa unayo anza tu bila wasiwasi
 
Nini cha kufanya sheria za nchi zipo wazi kabisa kama huelewi rejea katiba jeshi halipaswi kuwa na mfungamano na na chama chochote cha siasa,ila CCM wanakiuka kama wanavyafanya ila kwa kifupi wanaitengenezea nchi JENEZA.

Kwa kutumia sheria hizo za nchi (katiba) hawa wakuu wa vyombo vya usalama wanateuliwa na nani na unatarajia wajipendekeze kwa nani? Alitokana na chama gani?
 
Huyu Lema ana matatizo gani?
Kwanini asiige kutoka kwa Zitto na Mnyika?
Anaonekana mtu wa vurugu muda wote, ameshasababisha wakazi wa Arusha kumwaga damu na bado anaendelea kuchochea vurugu!
Wakazi wa Arusha amkeni, huyu siyo mtu mzuri kwenu.
 
tukukumbuke mazuri ya CHADEMA yanayofanywa,tunajua sasa kuwa hata ajira nyeti za serikali zimekuwa za upendeleo hata huku USALAMA WA TAIFA,watu wamekwa kulinda mafisadi ndio maana tunakuta tunaongoza kwa madawa ya kulevya baada ya kuwakamata wanatengeneza picha za video,leo hii wanyama wanapakizwa KIA ,usalama wako wapi madini yanaibiwa,intelejensia yenu i wapi?

ila mnayaona ya CHADEMA ambayo ni ya kukomboa Nchi, ni dhahiri kwa sasa wanatengeneza majeneza nasi hatuogopi kwani wote tutaingia ila suala nani atakuwa wa kwanza na nani wa mwisho ili mradi tuu Tanzania hii iliyopoteza heshima ipate heshima, Tanzania hii inayoendeshwa kwa dhuluma na hila ikapate kukomboka.

Najua kinchofanyika hata huko JESHINI/POLISI/USALAMA ni watu wa ngazi za juu ndio wanojikomba kwa viongozi CCM kutetea ulaji lakini askari wa chini ni maskini ambao wanatii amri za wakubwa wao ili wapate mkate wa kila siku.Ukitaka kujua hili nenda katazame vituo vya kupiga kura katika makambi ya JESHI utapata jibu sahihi.JUENI KUWA MNATEGA MABOMU KATIKA CHUMBA MANCHOLALA.
 
Huyu Lema ana matatizo gani?
Kwanini asiige kutoka kwa Zitto na Mnyika?
Anaonekana mtu wa vurugu muda wote, ameshasababisha wakazi wa Arusha kumwaga damu na bado anaendelea kuchochea vurugu!
Wakazi wa Arusha amkeni, huyu siyo mtu mzuri kwenu.
Hivi nani alimwaga damu kama c polisi? hivi amfuate Mnyika na Zitto hivi tatizo la Arusha ndilo la Ubungo na Kigoma ? HIVI YUPI mwenye fujo anetishiwa anayetishia ebu usiwe mchumu wa kufikiri?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom