Lema 'aichana' Idara ya Usalama wa Taifa

Status
Not open for further replies.
Nafikiri Arusha siku moja itakuwa Banghazi ya Tanzania maana chadema inatafutiwa kila sababu ili iangushwe lakini hawataweza maana watu Wa Arusha sasa hivi wako tayari kwa lolote.Niliona siku ya mkutano Wa chadema ulifanyika mwezi uliopita.Ombi langu kwa usalama Wa taifa wasitumiwe na vyama kutuharibia nchi.
Hawasikii wala hawaoni yaliyotokea LIBYA,MISRI,TUNISIA NA IVORY COAST!Wamepofushwa na dhambi zao dhidi ya wa TZ.MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI NA AIBU.Vifaru na maji ya pilipili na usalama wa taifa huu kamwe hautaishinda haki kwani anaemiliki haki ni Mungu.Mungu ibariki Tanzania kama MISRI NA LIBYA.waache wafanye shingo zao ngumu, wananchi tutazivunja kwa nguvu ya umma kama zile shingo za Gadafi na MubaraK!A-town, lianzisheni tumalize fasta.
 
Yaliyotokea Libya, Tunisia na Misri si lazima yatokee Tanzania kwa staili ile ile
 
Hawa usalama wa taifa,wanatumia kodi zetu,kwa manufaa ya ccm,mara baada ya Viongozi wa Chadema Arusha,kuwalipua,kuna habari za uhakika kuwa sasa usalama wa Taifa wanatafuta jinsi ya kuwauzia gari au chombo kingine feki,Jumamosi walidhani Lema angesafiri hivyo kuweka gari ya wizi pale airport ambapo wangejifanya wanauza na Lema akiwa anaishangaa wamkamate kuwa yeye ndio kaagiza gari ya wizi,kimsingi mipango yao yote inafichuka mapema,nawashuri wakae upande wa haki.
 
<font size="4">Yote haya ni sehemu tu ya matokeo ya KILIO CHA WALAZWAHOI nchini pindi wanapoona genge la mafisadi nchini wakiingia Igunga kwa mbwembwe, mikogo na ufedhuli wa kujitutumua na mali ya wizi wa mali za umma kwenye kampeni zao.<br />
<br />
Ni sharti Mafisadi wote wamrudie Mungu nchini, kutubu na kurudisha mali zote hazina ya taifa; la sivyo zahama huenda usiishe kwao tangu sasa. Mambo yataendelea KI-GUNDU GUNDU KWA CCM kila kona wasipotubu hadharani kwa umma wa Tanzania.</font>
<br />
<br />
Fisadi kumrudia mungu ni ngumu kama ilivyo ngamia kupita tundu la sindano
 
ni watu wachache sana wasiojua uongo wa mbunge lema ndio maana kamanda alimuumbua..shauri lake watammaliza kwa maneno yake ya uongo na kuisingizia seriklai na vyombo vya dola
 
Yaaani ninavyoipenda chadema sijui nisemeje,viongozi wako safi na hawaogopi mtu wanawapa ukweli vibalaka wa ccm bila kuficha hata neno 1,yaani siku likilipuka ni kuwasaka vibala kwanza na kuwapa haki yao kabla ya wengine.
&lt;br /&gt;
&lt;br /&gt; Yaani tayari maumivu ya kichomi yashahamia the other side? Oh mamma! Kichomiz au Kinyongaz???
 
Kizuri ni kujua mazingira, nasaba na haiba ya wakazi wa majimbo hayo kwa kila mmoja.Lema anawakilisha jimbo la Arusha mjini ambalo lina wakazi wake wana mchanganyiko lakini wenyeji walio wengi ni Waarusha,Wamelu,Masai,Wachaga na hao wote kiahaiba wanajulikana ni aina ya watu walio wazi kiasilia na wasio taka mzaa na ubabishaji au kupindisha maneno, Wakazi hao wa Arusha ni wafuasi wa kutambua Koleo ni koleao na kijiko ni kijiko,na hivyo si sawa kusema koleo ni kijiko kikubwa.

Wakati huo mnyika ni mwakilishi wa jimbo la Ubungo ambalo wakazi wake ni mchanganyiko wa makabila tofauti tofauti na wenyeji wake wengi ni wazaramo na mchanganyiko wa makabila ya pwani kama wakwere nk,ambayo kihaiba ni watu wa kuchukulia utatuzi wa matatizo kwa misingi ya maongezi ya muda hata kama yatakuwa na kero kubwa kwao na hasara yoyote wao imani kubwa kuwa mtapata suluhu muda ukifika.

Kwa picha hiyo utaona kila mmoja anaongoza jimbo likiwa na utamaduni tofauti wa wenyeji wake wakiwa na mtizamo tofauti wa kiamapokeo na utatuzi wa matatizo yao.

Msimuonee Lema angalieni jamii,na tamaduni,Nyerere na uwezo wake wote wa kuwajenga watanzania bado alipofika kwa ndugu zake wakurya ilikuwa ni kazi kuwaelimisha na kuwafikishia ujumbe,na mpaka ameondoka bado mkoa ule kauacha akiwa hana jibu kamili ni watu wa aina gani.

Mkuu kwa kuwa Lema ni mchaga basi ndio hivyo tena anaita Koleo Koleo na si kijiko kikubwa. Wakurya pia wanaaminika kwa kuita Koleo Koleo lakini marehemu pamoja na ukurya wake hakuwa na vitisho kama vya huyu Lema.

Kwa taarifa yako wakazi wengi wa Ubungo ni Wachaga na wala si wazaramo. Nadhani hauko nchini Tanzania upo Afrika magharibi. Namkubali Mnyika kwa kuwa anajenga hoja bila vitisho. Hakika nakuambia kwa mwendo huu wa Lema uchaguzi ujao sijui kama atanusurika kama hatajitambua na kubadilika na pia hakika nakuambi Mnyika atafika mbali kisiasa labda apete uroho wa pesa aingizwe kwenye rushwa vinginevyo yeye ataenda mbali. Kijana ana hoja za utaifa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom