NA SHAABAN MDOE. ARUSHA NJAMA za mbunge wa Arusha Mjini Gogbless Lema (CHADEMA) kushinikiza mgomo wa daladala na pikipiki , ikiwa ni ishara ya kupinga kuwekwa rumande, zimegonga mwamba , baada ya wamiliki wa vyombo hivyo vya usafiri kutomuunga mkono. Habari zilizopatikana mjini hapa zinasema wamiliki wa vyombo hivyo waliamua kutounga mkono mgomo huo , baada ya kutafakari na kuhoji mantiki yake kwa kuwa dhamana ulikuwa wazi kwa Lema lakini alikataa kudhaminiwa ili apelekwe rumande. Jana asubuhi vijana waliosadikiwa kuwa ni wafuasi wa Lema walifanya vurugu kwa kupiga mawe kila daladala na pikipiki iliyotoa huduma ya usafiri ili kuwashinikiza wahusika kugoma. SOURCE: UHURU [/QU SOURCE NINI UHURU! YALAAH NA WEWE ULIYE-POST ULIFIKIRIA NINI? LEMA YUPO JELA KAHAMASISHAJE MGOMO! TZ HII TUTAFIKA KWELI?