miss strong
JF-Expert Member
- Jul 4, 2012
- 7,012
- 3,694
Poleni wana JF na majukumu ya kila siku.
Nimerudi tena kwa muendelezo wa ile kesi,nisiwachoshe sana lakin hali iliyofikia ni kutishiwa aman kabisa kwa ujumbe mfupi wa maaandishi kupitia simu yangu ya mkononi.
Kama nilivyotoa maelezo katika thread ile ya pili juu ya hatua zangu nilizochukua .........hatimaye ss uongozi katika ngazi ya mkurugenzi wa mafunzo alimuandikia barua huyo lecturer juu ya mimi kutojaziwa course work na kumuamuru nijaziwe course work yangu ndani ya masaa 12.
Lecturer huyo alifanya hivyo lakin hakuipeleka kwa mkuu huyo na badala yake akaipeleka kwa mkuu wa idara yangu........!
Kilichotokea sasa ametoa excuse kuwa alikuwa anaona majina mawili kwahyo ndo yalimchanganya.......mfano;TINA JOEL NA TINA KIMARO(majina haya si rasmi) wakati ukweli mtu huyo anatumia TINA JOEL KIMARO,hiyo ni sababu iliyomfanya acheleweshwe course work yangu.
Tukumbuke mtu huyo alishawahi niifundisha semister iliyokwisha somo jingine na haijawahi tokea tatizo hilo.Lakini leo hii anatoa hiyo sababu.
Lecturer huyo baada yakuwekwa kiktimoto na mkurugenz wa mafunzo,usiku wa siku hiyo hiyo nilipokea ujumbe uliotumwa na namba ngeni nao unasema hivi "Acha mchezo mchafu binti utaharibika kwa uzembe wako,hayo ni mambo yakupita binti yangu acha masihara utajuta.Yangu macho,usiku mwema."
Nilitafakari huo ujumbe sana,lakini nilijitia moyo.....Nilitolea taarifa kesho yake asubuhi kwa Mkurugenzi wa mafunzo.
Bado sijaitwa kwenye hiyo bodi ingawa kuna tetesi kuwa huyu mtu amekwisha andikiwa barua yakutaka kusimamishwa.
Tuombeane sana maana ni vita kubwa,nasubiri kuitwa tu.Nimesukumwa kuandika hili na moyo wangu ili muweze kufahamu nilipofika na pia hata kama lolote linatokea bas mtasikia tu, hata kama sintakuwepo katika dunia ila mtakuwa mmepata angalau kitu fulani.
ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI.
Nimerudi tena kwa muendelezo wa ile kesi,nisiwachoshe sana lakin hali iliyofikia ni kutishiwa aman kabisa kwa ujumbe mfupi wa maaandishi kupitia simu yangu ya mkononi.
Kama nilivyotoa maelezo katika thread ile ya pili juu ya hatua zangu nilizochukua .........hatimaye ss uongozi katika ngazi ya mkurugenzi wa mafunzo alimuandikia barua huyo lecturer juu ya mimi kutojaziwa course work na kumuamuru nijaziwe course work yangu ndani ya masaa 12.
Lecturer huyo alifanya hivyo lakin hakuipeleka kwa mkuu huyo na badala yake akaipeleka kwa mkuu wa idara yangu........!
Kilichotokea sasa ametoa excuse kuwa alikuwa anaona majina mawili kwahyo ndo yalimchanganya.......mfano;TINA JOEL NA TINA KIMARO(majina haya si rasmi) wakati ukweli mtu huyo anatumia TINA JOEL KIMARO,hiyo ni sababu iliyomfanya acheleweshwe course work yangu.
Tukumbuke mtu huyo alishawahi niifundisha semister iliyokwisha somo jingine na haijawahi tokea tatizo hilo.Lakini leo hii anatoa hiyo sababu.
Lecturer huyo baada yakuwekwa kiktimoto na mkurugenz wa mafunzo,usiku wa siku hiyo hiyo nilipokea ujumbe uliotumwa na namba ngeni nao unasema hivi "Acha mchezo mchafu binti utaharibika kwa uzembe wako,hayo ni mambo yakupita binti yangu acha masihara utajuta.Yangu macho,usiku mwema."
Nilitafakari huo ujumbe sana,lakini nilijitia moyo.....Nilitolea taarifa kesho yake asubuhi kwa Mkurugenzi wa mafunzo.
Bado sijaitwa kwenye hiyo bodi ingawa kuna tetesi kuwa huyu mtu amekwisha andikiwa barua yakutaka kusimamishwa.
Tuombeane sana maana ni vita kubwa,nasubiri kuitwa tu.Nimesukumwa kuandika hili na moyo wangu ili muweze kufahamu nilipofika na pia hata kama lolote linatokea bas mtasikia tu, hata kama sintakuwepo katika dunia ila mtakuwa mmepata angalau kitu fulani.
ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI.