Lets Share
JF-Expert Member
- Jun 7, 2019
- 517
- 722
Truth should be told, nakubali pia naungana na wewe, lengo kubwa la kuchepuka sio kuwasaidia wanawake ambao hawana wanaume ila ni tamaa binafsi, ni katika hali ya kutafuta na kuboresha experience pamoja na burudani ya kubadili ladha..Siwezi kuunga mkono dhambi na ndo kama nilivyokwambia kwamba maandiko yanasema uzinzi na uasherati ni dhambi na hayajasema kwa jinsia ipi halafu kuhusu swala la wanawake kuwa wengi duniani kuliko wanaume hiyo siyo sababu ya ninyi kuchepuka
Labda nikwambie kitu kimoja ambacho pengine unakijua ila unajifanya haukijui ni hivi siyo kila binadamu alikuja hapa duniani kutimiziwa mahitaji yake yote ndo maana kuna matajiri na masikini yaani ili maisha yabalance ni lazima kuwe na waliopata na waliokosa hivyo pia lazima kuwe na waliooa/walioolewa na wasiooa/wasioolewa na hao waliokosa walipangiwa kukosa na siyo lazima wapate
Kwahiyo wewe oa mwanamke wako mmoja kama Mungu anavyotaka tulia naye hao wengine waliokosa waume wewe hawakuhusu halafu wanaume sijui mnatuona wanawake ni wapumbavu sana yaani kabisa eti mnataka tuamini huo uongo wenu kwamba mnachepuka ili muwasaidie wanawake wasio na wanaume wakati kiuhalisia hata mioyoni mwenu mnajua kabisa kuwa mnachepuka kwa tamaa zenu wenyewe mlivyo wabinafsi hivyo tangu lini mkafanya vitu kwa ajili ya wanawake hapo mnafanya kwa sababu mnajua ninyi ndo mnafaidika zaidi
Halafu kwani hizo roho za msaada zipo kwenye maswala ya ngono tu? Kama lengo ni kusaidia kweli mbona hamuonyeshi jitihada kutaka kusaidia masikini wasio na mali ili angalau kila mmoja awe na mali ila mnataka kusaidia tu wanawake wasio na waume ili kila mmoja awe na mwanaume? Bado narudi pale pale kwamba hakuna jinsia iliyoruhusiwa kutenda dhambi ila tunatenda dhambi kwa sababu sisi binadamu ni dhaifu na hata Mungu anaelewa ndo maana anatupa nafasi ya kutubu ili atusamehe kabla hatujafa mwenye macho na aone mwenye masikio na asikie
Hivyo tuombeane ili tuweze kuridhika na mke mmoja na wasio na waume tuachane nao wapambene na genye zao, pia tuombeane kupata nafasi ya kutubu kwa baadhi tutakaochepuka kabla ya kifo..🤝🤝


