Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,879
LAZIMA UJIFUNZE MAMBO HAYA.
Anaandika Robert HERIEL
Yule Mtibeli.
Lazima ujifunze kuona pasipo kutumia macho.
Tena ujifunze kusikia pasipo kutumia masikio.
Kama haitoshi ujifunze kusema pasipo kutumia mdomo,
Kwa maana Maisha ni vita isiyohitaji hayo, tena ni mbio zisizohitaji Farasi.
Niite Taikon wa Fasihi, mkimbiza WAKATI.
Naye ayategemeaye macho yake hataona, na apendaye kusikia hatosikia.
Nawe usisubiri majibu Kama hukutafuta maswali.
Napo uwapo katikati ya maswali usilete majibu, nawe uwapo katikati ya majibu usiweke Maswali.
Ujifunze kulia na kuomboleza pasipo kutoa machozi na ukelele,
Nawe ujifunze kufurahi pasipo kutoa Tabasamu.
Ujifunze ishara, Alama na kuzisoma nyakati, Kwa maana hizo hazitoi sauti lakini zinasema, nazo zipo lakini wenye macho hawazioni, ndio maana nalikuambia ujifunze kuona pasipo macho, tena kusikia pasipo masikio.
Looh! Taikon nimejihangaisha sasa!
Ujifunze kuuficha ukweli Kwa wapumbavu, tena ujifunze kuufichua ukweli Kwa wenye Hekima. Wala usijeukachanganya mambo hayo.
Jifunze kuona njaa wakati WA chakula, tena ujifunze kuwa na chakula wakati wa njaa, Kama utaweza kujizuia nafsi yako utakuwa umeyaweza maisha, tena Kama utaweza kuyazuia matamanio yako, utakuwa umejiepusha na maanguko.
Jifunze kuujua ukweli uliojificha kwenye Hila. Nao ukweli uliojificha kwenye hila na njama kamwe haionekani Kwa macho wala kusikika Kwa masikio ndio maana nalikuambia ujifunze kuona pasipo macho, na kusikia pasipo masikio. Hivyo ndivyo utakavyoishi.
Ujifunze kuona Shaka nafasi yako itakapoona upo salama kwani hiyo ndio salimini yako. Kwa maana waovu huweka mazingira salama kusudi kuteka Imani yako kusudi wakuangushe Kwa ghafula. Hayo nayo nilikuambia.
Ujifunze kumfurahisha Mkeo hata akiwa na huzuni, tena ujifunze kumchukiza awapo na furaha iliyopitiliza.
Ujifunze ku-balance furaha na huzuni yake. Kwa maana furaha ya mke ikizidi huweza kuangusha Nyumba, na huzuni ya Mke ikizidi huleta machafuko na mauti.
Ujifunze kumpenda Mkeo hata akiwa anakuudhi, tena ujifunze kumchukia wakati akikufurahisha. Hivyo ndivyo namna Bora ya kuishi na Mke wako.
Usiache usiku ukawa mrefu kuliko mchana, wala usiache mchana ukawa mrefu zaidi ya usiku. Hayo nayo niliyasema.
Ujifunze mbio ndefu hata Kama wewe ni wambio fupi, tena ujifunze mbio fupi hata Kama wewe ni wambio ndefu.
Jifunze kuwa Yatima hata Kama unawazazi, tena ujifunze kuwa Mjane hata Kama Una mume. Hivyo ndivyo utakavyoishi.
Jifunze kuudhiwa, kukerwa, tena ujifunze kufanya mambo yako ukiwa chini ya shinikizo, ukiwa umepaniki au kupanikishwa, tena katika Hali hiyo ujifunze kutenda Kwa usahihi pasipo kuathiri matokeo.
Ujifunze kusema Ahsante haraka Kama haujaridhika, na ujifunze kutoshukuru hata Kama umeridhika.
Niseme nini tena???
Sasa Taikon ataenda kupumzika, Kwa leo hayo yakutoshe.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika Robert HERIEL
Yule Mtibeli.
Lazima ujifunze kuona pasipo kutumia macho.
Tena ujifunze kusikia pasipo kutumia masikio.
Kama haitoshi ujifunze kusema pasipo kutumia mdomo,
Kwa maana Maisha ni vita isiyohitaji hayo, tena ni mbio zisizohitaji Farasi.
Niite Taikon wa Fasihi, mkimbiza WAKATI.
Naye ayategemeaye macho yake hataona, na apendaye kusikia hatosikia.
Nawe usisubiri majibu Kama hukutafuta maswali.
Napo uwapo katikati ya maswali usilete majibu, nawe uwapo katikati ya majibu usiweke Maswali.
Ujifunze kulia na kuomboleza pasipo kutoa machozi na ukelele,
Nawe ujifunze kufurahi pasipo kutoa Tabasamu.
Ujifunze ishara, Alama na kuzisoma nyakati, Kwa maana hizo hazitoi sauti lakini zinasema, nazo zipo lakini wenye macho hawazioni, ndio maana nalikuambia ujifunze kuona pasipo macho, tena kusikia pasipo masikio.
Looh! Taikon nimejihangaisha sasa!
Ujifunze kuuficha ukweli Kwa wapumbavu, tena ujifunze kuufichua ukweli Kwa wenye Hekima. Wala usijeukachanganya mambo hayo.
Jifunze kuona njaa wakati WA chakula, tena ujifunze kuwa na chakula wakati wa njaa, Kama utaweza kujizuia nafsi yako utakuwa umeyaweza maisha, tena Kama utaweza kuyazuia matamanio yako, utakuwa umejiepusha na maanguko.
Jifunze kuujua ukweli uliojificha kwenye Hila. Nao ukweli uliojificha kwenye hila na njama kamwe haionekani Kwa macho wala kusikika Kwa masikio ndio maana nalikuambia ujifunze kuona pasipo macho, na kusikia pasipo masikio. Hivyo ndivyo utakavyoishi.
Ujifunze kuona Shaka nafasi yako itakapoona upo salama kwani hiyo ndio salimini yako. Kwa maana waovu huweka mazingira salama kusudi kuteka Imani yako kusudi wakuangushe Kwa ghafula. Hayo nayo nilikuambia.
Ujifunze kumfurahisha Mkeo hata akiwa na huzuni, tena ujifunze kumchukiza awapo na furaha iliyopitiliza.
Ujifunze ku-balance furaha na huzuni yake. Kwa maana furaha ya mke ikizidi huweza kuangusha Nyumba, na huzuni ya Mke ikizidi huleta machafuko na mauti.
Ujifunze kumpenda Mkeo hata akiwa anakuudhi, tena ujifunze kumchukia wakati akikufurahisha. Hivyo ndivyo namna Bora ya kuishi na Mke wako.
Usiache usiku ukawa mrefu kuliko mchana, wala usiache mchana ukawa mrefu zaidi ya usiku. Hayo nayo niliyasema.
Ujifunze mbio ndefu hata Kama wewe ni wambio fupi, tena ujifunze mbio fupi hata Kama wewe ni wambio ndefu.
Jifunze kuwa Yatima hata Kama unawazazi, tena ujifunze kuwa Mjane hata Kama Una mume. Hivyo ndivyo utakavyoishi.
Jifunze kuudhiwa, kukerwa, tena ujifunze kufanya mambo yako ukiwa chini ya shinikizo, ukiwa umepaniki au kupanikishwa, tena katika Hali hiyo ujifunze kutenda Kwa usahihi pasipo kuathiri matokeo.
Ujifunze kusema Ahsante haraka Kama haujaridhika, na ujifunze kutoshukuru hata Kama umeridhika.
Niseme nini tena???
Sasa Taikon ataenda kupumzika, Kwa leo hayo yakutoshe.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam