LATRA wekeni ukatishaji tikiti uwe kwenye data bila malipo

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,670
22,260
Mfumo wa ukatishaji tikiti kwa njia ya mtandao ni nzuri, pamoja na hilo kikwazo ni lazima uwe na bando ndipo utaweza kukata tikiti, hapa ndipo unapojikuta unatumia pesa nyingine huenda kuliko mfumo wa zamani, mfano mtu anayetoka Dar kwenda Chalinze ambapo angelipa shs. Elfu tano hivi, sasa analazimika Kununua bando kwanza labda shs. Elfu mbili au zaidi ili aweze kupakua aplikesheni ya LATRA na kununua tikiti, kwa hiyo gharama tayari inakaribia nauli!

Tatizo jingine ni ununuaji wa vocha hasa wakati wa usiku au baadhi ya maeneo hata wakati wa mchana. Ukitumia mfumo wa DATA BILA MALIPO matatizo yote haya hayatakuwepo, hivyo LATRA kama mna nia ya kutusaidia wananchi bila kujali kukosa kipato toka kwetu, tumieni mfumo huu.
 
Mbna mi huwa nakata Dar lux online , mfumo bomba Sana huo , yaan unajichagulia siti na ni impossible kukatiwa ticket watu wawili , niliwakubali hao jamaa...yaan unakata ticket upo home na mama watoto anakupapasa , hii ya kwenda stend Kwanza unazongwa zongwa na wapiga debe daah.... Alaf office nying nying gari moja , ndo mambo ya kukatiwa tiketi moja watu wanne
 
Kwani wasitumie mitandao ya simu, au wawe na USSD code yao? Wale wasio na simu zenye uwezo wa mtandao inakuwaje sasa!
 
Kwa hili mimi sumo, miaka hiyo ambavyo UDA walikatisha tikiti kwa mtandao! Mimi sikuwepo duniani na sijawahi kusikia kuwa mabasi ya UDA yalikuwa yanaenda mikoani, labda kama yalikuwa yanatoka mikoani tu kuna Dar!
Ipo hivi, ilikuwa ukipanda UDA kondakta anakukatia tiketi kutoka kwenye kimashine alichokivaa shingoni, baada ya kulipa nauli..
najaribu kuwaza, ikiwa miaka hiyo waliweza leo teknolojia imekuwa
tunakosea wapi?
 
Kwani wasitumie mitandao ya simu, au wawe na USSD code yao? Wale wasio na simu zenye uwezo wa mtandao inakuwaje sasa!
Hili nilishauri walipotangaza mfumo mpya katika Post yangu ambayo Mods walibadili kichwa. Tatizo hawapokei maoni na mawazo yetu labda yatoke kwa viongozi wa CCM.
 
Mfumo wa ukatishaji tikiti kwa njia ya mtandao ni nzuri, pamoja na hilo kikwazo ni lazima uwe na bando ndipo utaweza kukata tikiti, hapa ndipo unapojikuta unatumia pesa nyingine huenda kuliko mfumo wa zamani...
Mi5 tenadata itakuwa free
 
Ipo hivi, ilikuwa ukipanda UDA kondakta anakukatia tiketi kutoka kwenye kimashine alichokivaa shingoni, baada ya kulipa nauli..
najaribu kuwaza, ikiwa miaka hiyo waliweza leo teknolojia imekuwa
tunakosea wapi?
Ile haikuwa ya elekitroniki ilikuwa manual sawa na zilizokuwa madukani tofauti ni kuvaa shingoni au kuweka mezani, hata hivyo mfumo huu hauhusu mabasi ya ndani ya jiji kwani hayana buking'i, sijui kwa nini umeuleta mfano huu hapa!
 
Huu mfumo gundu sana, zaman nilikuwa na mwambia tu konda niuzie seat iliyo na mtoto mzuri (mrembo) bac mambo yanakuwa baridiiii nikikuwa na pataga videm sasa kwa mfumo huu ah ........alisema kijana mmoja
 
Huu mfumo gundu sana, zaman nilikuwa na mwambia tu konda niuzie seat iliyo na mtoto mzuri (mrembo) bac mambo yanakuwa baridiiii nikikuwa na pataga videm sasa kwa mfumo huu ah ........alisema kijana mmoja
Ukikata kwa kutumia kompyuta na ukaingiza matakwa yako inakutafutia na kukuweka kwenye siri unayoitaka ya mtoto mzuri, ila mwenziyo aliibiwa simu kijinga Himo njia Panda stendi, kabinti kameacha pochi kwenye siri kanampigia dadii Moshi huku kako chini kanajidai eti kununua maparachichi, basi inataka kuondoka hakaonekani, mjamaa kamwambia kondakta, kinda haoni mpiga simu yeyote chini, mjamaa kazunguka basi maratatu tupu! Abiria wakamshauri aangalie ndani ya pochi, kufungua wakakueta mazagazaga matupu ambayo hayafanani na pochi.
 
Ukikata kwa kutumia kompyuta na ukaingiza matakwa yako inakutafutia na kukuweka kwenye siri unayoitaka ya mtoto mzuri, ila mwenziyo aliibiwa simu kijinga Himo njia Panda stendi, kabinti kameacha pochi kwenye siri kanampigia dadii Moshi huku kako chini kanajidai eti kununua maparachichi, basi inataka kuondoka hakaonekani, mjamaa kamwambia kondakta, kinda haoni mpiga simu yeyote chini, mjamaa kazunguka basi maratatu tupu! Abiria wakamshauri aangalie ndani ya pochi, kufungua wakakueta mazagazaga matupu ambayo hayafanani na pochi.
Huyo alikuwa BOYAAA sana, sio kila nyama inauzwa buchani ...
 
Back
Top Bottom