Laana ya mwanamke

Umemaliza kiongozi,I think wakuhukumu hapa ni Mungu na sio mtu tena kwa sababu wote mnakuwa mmetenda dhambi ila kuna mtu hapa yupo likely kuhukumiwa kwa dhambi nyingi zaidi
 
Hakuna kitu kinauma kama kupotezewa Muda, Ex wangu hadi leo pamoja na kuwa na kazi nzuri maisha yake hayaeleweki, kwenye mahusiano ndo usiseme, nabado napiga goti kwa Mungu siku atakayorudi kuomba msamaha kwakunikosea ndo amwachilie.
Nahisi kwamba nawe umejifunga. Huna raha mpaka umwone ameumia! Mwachilie, msamehe, msamehe kabisa. Utaona raha kubwa. Usijali kama ataenda mbele au atarudi nyuma. Wewe mwombee kwa Mungu kwa kumsamehe kabisa. Utajifungulia milango mingi zaidi.
 
I can feel you on this.. It hurts so much... But let him go so God can use you more ..Thanks..
Exactly..hakuna haja ya kumbeba mtu moyoni...samehe huko aliko ili nawe uwe na aman moyonI na upate nafasi ya kuweka mwingine...nisipomsamehe itanisaidia nn...mangapi namkosea Mungu na ananisamehe..mimi ni nanI ht nijibebeshe mizigo ...akhaaaaaa
Yn I thank God for that nitaumia mwanzoni but na let it go..nakuwa na amaani...hukupangiwa kuwa wangu ..go....full stop
Only God knows why amemuondosha
 
Hivi nisiposamehe nikienda kanisani kusali napiga goti naanzaje kumuomba Mungu.??kwanza nasikia aibuu ht kuomba..na ikitokea naenda kanisan nitakuwa tu km picha ...nashindwa kabisa kumuomba Mungu ipasavyo cz kuna kitu moyon kinanisuta....GUYS FORGIVE AND FORGET KUNA RAHA KUBWA SANA YA KUMSAMEHE ALOKUKOSEA
kwanza huko aliko vitamsuta
Pili unajiongezea baraka
Visasi na maugomvi sio mazuriiiii....dunia itakua chungu kila siku ukiendekeza mavisasi na kubeba watu moyoni
 
Mambo kama hayo hayapo,huo ni uongo na uzushi, ni mambo tu ya kiswahili kupenda ushirikina na uchawi ambao kiuhalisia haupo.

Yani mtu awe na kinyongo na wewe mganga ndio ajue kua kuna mtu ana kinyongo na wewe? Sema unataka tu kusema hua unaenda kwa waganga wa kienyeji ila mambo kama hayo hayapo.
 
Nisamehewe tuu nanaomba huyu mwanaume apate pigo la maisha hadi ajue kweli macjoz yangu na mwanangu tumboni mungu anatusikia!!!
 
 
Wanawake wengi warembo ni watoto wa shetani...nuksi tupu...au hawana kibali chochote mbele ya mungu kukubariki....mara nyingi ukiingia hapo basi hata kile kidogo ulichonacho kinapotea...
Kwa kauli yako hii Basi Nyani Ngabu atakuwa mtoto wa malaika manake ana sura mbovu ka nyani kaonja ukwaju.
 
Katika masuala ya mahusiano mwanaume ndio muanzilishi....ni agharabu sana kwa mwanamke kumtongoza mwanaume ingawa hutokea....
Katika kushawishi huko unaweza ukamtoa mwanamke katika hali fulani hivi ya kutokukuamini na hatimaye akakuamini na hatimaye mkawa kwenye mahusiano.....
Wakati mwingine huyo mwanamke anaweza kuwa alikuwa kwenye mahusiano na mtu mwingine wenye mipango ya muda mrefu lakini kuringana na sera zako za kuvutia hatimaye ukambadilisha maamuzi na kuingia kwenye imaya yako.....kumbuka hata hapo kwenye kumtoa mwanamke kwenye imaya ya mtu mwingine tayari umeshaumiza nafsi ya mtu mwingine.....

Hadi kufikia hapo mwanamke huyu atakuwa na matumaini makubwa sana kwako....mapenzi yake na yote atayahamishia kwako akiamini kuwa wewe ndiye yule aliyeletewa na Bwana.....wakati mwingine huwa anakuulizia masuala ya kuona na wewe unamuambia kuwa dear mbona mapema sana....

Kwa kuwa lengo lako ni kumvua tu nguo na kumuacha unaanza harakati za kuomba ngono kwa kushawishi kwa aina mbali mbali na yeye lazima atakupa akiamini kuwa ni moja wapo ya njia ya kudumisha penzi lenu ili mfike mbali.....mtoto wa kike anajiachia kwako kwa raha zote hakuna sehemu ya mwili wake usiyoijua kwa jinsi alivyojiachia kwako akiamini kabisa kuwa wewe ndiye mumewe.....

Siku zinavyoende kwa kuwa umeshapata ulichokuwa unakitaka mapenzi yanapungua....unaanza kumuona kama kero fulani hivi....yaani kama anajipendekeza fulani hivi kwako.....hali hiyo inaendelea mpaka mwanamke anaanza kuwa na wasi wasi kuhusu hali ya uhusiano wenu....unaamzungusha na hatimaye unaamua kumuambia live kuwa huna mpango nae....

Hebu jiweke katika nafasi ya mwanamke je ungejisikiaje...

Hakika ni jambo lenye kukera na kusononeka maaana katika muda huo labda alipuuzia mahitaji ya watu wenye upendo wa kweli huku akiishi katika uongo wako....
Ni jambo ambalo kwa mwanadamu mwenye akili ya kawiada hangependa limtokee kwani ni jambo kuumiza moyo kama sio kuuchoma moyo....

Yale manung'uniko, masononeko na machozi yasiyokauka muda wote kila akifikiria jinsi ulivyozikatisha ndoto zake nyingi tu kwa ajili ya uongo wako ndivyo vinavyokuletea mikosi kwenye maisha yako.....

Ndio maana hata nyakati hizi utafutaji ridhiki umekuwa ni mgumu sana kwa vijana wa kiume kwa sababu ya madhambi makubwa sana waliyowatendea mabinti wa watu.....maana kuna mabinti wengine walijitunza sana lakini wakashawishika kwa ulaghai wao.....
Na mambo ambayo ni ngumu kuyathibitisha kama ambavyo ilivyo kwa nguvu za giza lakini yapo na watu wanateseka kwa ajili ya hayo....
Hujawahi kuona anakuwa kama kachanganyikiwa baaada ya kuachika na mtu ampendaye....wengine huenda mbali mpaka kunywa sumu na kuutoa uhai wako mtukufu kwa ajili ya ulaghai wako tu......sasa hapo kuna baraka gani kwenye maisha yako ikiwa wewe ndiyo chanzo cha mahangaiko na vifo vya mabinti wengi sana mtaani......??
 
Nisamehewe tuu nanaomba huyu mwanaume apate pigo la maisha hadi ajue kweli macjoz yangu na mwanangu tumboni mungu anatusikia!!!
Pole sana dada yangu....Mungu humzidishia baraka yule mwenye kusamehe.....kuendelea kuhifadhi hasira kifuani mmwako ni sawa na kushikilia kaa la moto....maana yake kabla ya kumrushia mtu limuunguze kwanza linaanza kukuunguza wewe......samehe uone jinsi gani kama umezaliwa upyaa.....
 
Huwezi kujua kuwa dunia ina mambo mpaka likukute jambo....
 
Machungu ninayopitia anajua mungu pekee, na mwanangu àliepo tumboni, ndio màana naomba lolote baya juu yake nae aumie, japo haitofikia maumivu yangu hata theluthi
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…