LAAC yaagiza ukaguzi maalum stendi mpya ya Moshi Manispaa

Kisambusa

Member
Aug 8, 2022
27
16
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) imemuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalum kwenye ujenzi wa stendi ya Kimataifa iliyopo kata ya Mfumuni, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya maelezo ya mradi kujikanganya.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Seleman Zedi amesema hayo leo Ijumaa, Septemba 3, 2022 mara baada ya kamati yake kuchambua CAG, zinazoishia Juni 30, 2021.

“Baada ya mahojiano yetu na halmashauri ya Moshi, tumemwagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenda kufanya ukaguzi maalum kuhusu mkopo wa Tsh. 20 bilioni ambao manispaa ilikuwa imeingia mkataba na benki ya TADB,” amesema.

Amesema wameagiza ukaguzi maalum kwasababu ya mkanganyiko wa maelezo ya manispaa hiyo kwasababu mara ya kwanza walituambia waliingia mkataba na TADB kukopa Tsh. 20 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo.

Hata hivyo, Zedi amesema baadaye walipata barua ya zuio kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) wasipate huo mkopo lakini wakati huo huo ndani ya mkopo huo kulikuwa na Tsh. 378 milioni ambazo ni malipo ya mhandisi mshauri.



“Wametuambia wazuiwa wasiendelee na ule mkopo lakini hapo hapo wanatuambia, zile Tsh. 378 milioni yaani benki ya TADB walitoa fedha hizo kumlipa mhandisi mshauri ambaye anaitwa Digital Space Consultant,” amesema Zedi.

Amesema fedha hizo ni sehemu ya mkopo waliouomba na benki ya TADB, licha ya manispaa kusema walizuiliwa na Tamisemi kukopa fedha hizo Tsh. 20 bilioni.

“Tukaona iweje unatuambia fedha Tsh. 378 milioni ambazo ni sehemu ya mkopo wa Tsh. 20 bilioni ambazo zilizuiwa zilitolewa? Tumeagiza CAG akafanye ukaguzi kuhusu mkopo huo,” amesema ambaye ni Mbunge wa Bukene.

Amesema kwa maelezo ya manispaa, walisema walipeleka andiko Hazina kuomba Tsh. 20 bilioni kwa ajili ya mradi huo lakini walikubaliwa Tsh. 7 bilioni.

Hata hivyo, amesema hadi sasa wamepewa Tsh. 2 bilioni na kwamba fedha zilizokubaliwa ni ndogo sana kukamilisha mradi huo ambao unahusisha ujenzi wa hoteli katika eneo hilo.

Chanzo: Mwananchi
 
Ila bongo jamani. Miradi mingi ya hizo stand bei zake zilikuwa inflated karibia mara 80%. Yaani huwezi sema eti stand ya billion 7 ni ndogo, je unajenda nini???? Watanzania hakika tunachelewa sana kupata maendeleo
 
TOKA MAKTABA: 10 June 2020


Ujenzi Wa Stendi Ya Mabasi Moshi Mjini unakabiliwa na changamoto Mkondo Wa Maji unaoibua chemchem katika ghorofa ya chini ya ardhi katika ujenzi wa stendi hiyo.

Ametoa kauli hiyo leo baada ya kukutana na uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Moshi wakati akikagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Mhe. Jafo amesema kuwa kwa sasa maji yanapita katika eneo hilo lakini yakiwa yamepungua, huku wataalamu wakiendelea kutafuta ufumbuzi kwa maji kujaa yakitokea chini ya Ardhi.

Ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Moshi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo hasa katika ujenzi wa miradi ya kimkakati japokuwa mradi huo umekuwa na changamoto ya jengo kujaa maji kwa chini.

Aidha Mradi wa Stendi ya Mabasi Mkoani huo utagharimu shilingi bilioni 28 fedha ambazo zilitolewa na Serikali kwa Halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa Miradi ya kimkakati.

Wakati huohuo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Bw. Michael Mwandesi ameeleza kuwa mradi wa stendi ya mabasi umepata changamoto kubwa ya jengo kujaa maji chini jambo ambalo lilisababisha Halmashauri kusimamisha ujenzi kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa chanzo cha maji hayo.

Amesema mpaka sasa wataalam wameshafanya utafiti wa kina na imegundulika kuwa jengo hilo halijaathrika na maji hayo, kutokana na uimara mkubwa wa jengo hilo.

Source : Jafo aagiza wataalamu kufanya utafiti wa maji yaliyochini ya ardhi mradi wa Stendi ya Mabasi


21 June 2020
Moshi, Kilimanjaro
Tanzania

Wataalamu wa Jiolojia wafanya utafiti wa Chemchem mkoani Kilimanjaro​



Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Kurugenzi ya Huduma kwa Umma pamoja na Idara ya Jiologia kutoka Ndaki ya Sayansi Asili na Sayansi Tumizi, imeleta wataalamu wa maji ya ardhini ili kuisaidia Manispaa na Moshi kupima na kuangalia maji yanayotoka ardhini na kujaa kwenye makazi ya watu na katika mradi mpya wa Stendi maeneo ya Majengo. Msafara huo wa wataalamu unaongozwa na Dkt. Mona Mwakalinga- Mkurugenzi Huduma kwa Umma, Dkt. Simon Melekioly, Dr. Remigius Gama na Bwn. Majura Songo kutoka Idara ya Jiolojia.
Source : University of Dar es Salaam


23 September 2021

ONA..!! Kituo kipya cha mabasi kilichowekwa jiwe la msingi na WAZIRI MKUU


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi katika eneo la Ngangamfumuni, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

 
Hakukuwa na hata haja ya kujenga stendi mpya kwa Moshi, stendi iliyopo sasa japokuwa ilijengwa zamani kidogo lakini iko kisasa na inaweza kuendelea kutumika ikiwa itaboreshwa kidogo na kutumiwa ipasavyo. Mapungufu yaliyopo kwenye stendi ya sasa ni haya.....

1. Stendi kugeuzwa soko (stendi imejazwa biashara mbalimbali wakiwemo wamachinga, mama lishe, wauza mboga, matunda, wasafisha kucha nk)

2. Stendi kutumika kwa mabasi ya ndani ya mkoa badala ya kutumika kwa mabasi yanayoenda mikoa mbalimbali na nje ya nchi tu (kwa sasa karibu 80% ya eneo la stendi kumejazwa vipanya, Noah na Coaster zinazoenda ndani ya mkoa wa Kilimanjaro na mengine machache mkoa wa jirani wa Arusha).

3. Vyumba vyote vilivyopaswa kuwa office za makampuni ya mabasi ndio vimepangishwa wafanyabiashara. (Yaani stendi imekuwa mall ya kienyeji)

4. Eneo lote ambalo lilipaswa kuwa la kukaa wasafiri (waiting passenger/traveller area) ndio zimejazwa meza za wakatisha tiketi na wafanyabiashara.

5. Utitiri wa vibanda vya wafanyabiashara vilivyojazwa kuzunguka eneo lote la stendi.

6. Sehemu kubwa ya floor ya juu (ghorofa ya tatu?) haina matumizi (imekosa wapangaji?)

SULUHISHO.
-Ondoa vibanda vyote vya wafanyabiashara ndani au kuzunguka stendi.

-Ondoa meza zote na biashara zoe kwenye eneo la kusubiria/kukaa wasafiri.

-Vyumba vyote vya eneo la chini (ground floor) vipangishwe makampuni ya mabasi, wakatisha tiketi, ofisi za usimamizi wa stendi, wanausalama (polisi), huduma za dharula, Maulizo, Vyoo nk. Wafanyabiashara wengine kama migahawa/hoteli, maduka zipangishwe floor za juu.

-Stendi ibakie kutumiwa na mabasi ya mikoani tu, noah, vipanya na Coaster za usafiri wa ndani zitafutiwe eneo jingine na kama itashindikana basi upande mmoja wa stendi ndio utumike kwa usafiri wa ndani (kwa kuwa stendi ina pande mbili.)
 
LAAC wako

vizuri kuhusiana na jambo Hilo ni la kweli 378 million tsh zilipigwa na uongozi wa manispaa hiyo na majina ya waliopiga hizo tunayo TISS na Takukuru waje inbox tuwatajie majina Yao na vyeo vyao kamili,na mahali walipo. Mhusika wa wizi huu Mkubwa ni mtumishi ambaye Kwa Sasa(2022)ni mtumishi wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali ya Tanzania Advocate Deogratus Nyoni .
 
Stand ya Moshi iliyopo sio mbaya sana sema wameweka mbele wafanyabiashara zaidi kuliko wenye mabus ama wasafiri. Hata maeneo ya watembea kwa miguu yamekodishiwa wamachinga yaani ni soko sio stand.
 
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro anzia kazi hapo Kuna pesa nyingi zilipigwa na wakati Majaliwa anaitwa kwenda kuweka jiwe la msingi kwenye hiyo stand tulimuone huruma.
Watu washapaua nyumba zao na kufungua masuper market tayari
 
Moshi walikuwa na stendi nzuri sana, pengine ndio stendi ya kwanza kuwa na lami wakati huo...

Sijui kipi kiliwakumba na kutaka kujenga stendi mpya
 
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) imemuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalum kwenye ujenzi wa stendi ya Kimataifa iliyopo kata ya Mfumuni, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya maelezo ya mradi kujikanganya.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Seleman Zedi amesema hayo leo Ijumaa, Septemba 3, 2022 mara baada ya kamati yake kuchambua CAG, zinazoishia Juni 30, 2021.

“Baada ya mahojiano yetu na halmashauri ya Moshi, tumemwagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenda kufanya ukaguzi maalum kuhusu mkopo wa Tsh. 20 bilioni ambao manispaa ilikuwa imeingia mkataba na benki ya TADB,” amesema.

Amesema wameagiza ukaguzi maalum kwasababu ya mkanganyiko wa maelezo ya manispaa hiyo kwasababu mara ya kwanza walituambia waliingia mkataba na TADB kukopa Tsh. 20 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo.

Hata hivyo, Zedi amesema baadaye walipata barua ya zuio kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) wasipate huo mkopo lakini wakati huo huo ndani ya mkopo huo kulikuwa na Tsh. 378 milioni ambazo ni malipo ya mhandisi mshauri.



“Wametuambia wazuiwa wasiendelee na ule mkopo lakini hapo hapo wanatuambia, zile Tsh. 378 milioni yaani benki ya TADB walitoa fedha hizo kumlipa mhandisi mshauri ambaye anaitwa Digital Space Consultant,” amesema Zedi.

Amesema fedha hizo ni sehemu ya mkopo waliouomba na benki ya TADB, licha ya manispaa kusema walizuiliwa na Tamisemi kukopa fedha hizo Tsh. 20 bilioni.

“Tukaona iweje unatuambia fedha Tsh. 378 milioni ambazo ni sehemu ya mkopo wa Tsh. 20 bilioni ambazo zilizuiwa zilitolewa? Tumeagiza CAG akafanye ukaguzi kuhusu mkopo huo,” amesema ambaye ni Mbunge wa Bukene.

Amesema kwa maelezo ya manispaa, walisema walipeleka andiko Hazina kuomba Tsh. 20 bilioni kwa ajili ya mradi huo lakini walikubaliwa Tsh. 7 bilioni.

Hata hivyo, amesema hadi sasa wamepewa Tsh. 2 bilioni na kwamba fedha zilizokubaliwa ni ndogo sana kukamilisha mradi huo ambao unahusisha ujenzi wa hoteli katika eneo hilo.

Chanzo: Mwananchi

Eric Hamisi aliyetumbuliwa Bandari ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa MSCL.​

( Akiwa mtumishi wa TIB ambayo sasa ni TADB) Takukuru wanakusalimia baba.​

 

Eric Hamisi aliyetumbuliwa Bandari ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa MSCL.​

( Akiwa mtumishi wa TIB ambayo sasa ni TADB) Takukuru wanakusalimia baba.​

Hii tumbua tumbua huwa ni kusherehesha umma tu but on the background hainaga uhalisia
 
27 March 2024
Moshi, Kilimanjaro
Tanzania

MKANDARASI ASITISHA UJENZI WA STENDI MOSHI MJINI , HAJALIPWA MADENI


View: https://m.youtube.com/watch?v=lwatE1SBp0s
Ujenzi wa stendi ya kisasa ya Ngangamfumuni Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro umekwama kufuatia madeni anayodai mkandarasi kutolipwa ... amebainisha Meya mstaafu wa mji huo wa Moshi , Raymond Mboya (Chadema)
 
Back
Top Bottom