Kwetu Kakola na Msalala

Kwetu Kakola na Msalala

Habari za muda huu wadau..?
Napenda kuwaleteen japo kidogo taarifa fupi kuhusu maendeleo katika wilaya yetu ya msalala na kijiji cha kakola.
Licha ya kuwa ni wilaya yenye uwekezaji mkubwa katika sekta ya madini namaanisha uwepo wa kampuni kubwa ya uchimbaji wa dhahabu inayomiliki mgodi wa bulyanhulu.maendeleo katika maeneo haya hasa kijiji cha kakola ni masikitiko makubwa,kwamba mpaka leo miaka takriban 19 ya uwekezaji bado hali si shwari.
Leo sitazungumzia yote hayo nataka kugusia kidogo swala zima la miundombinu ya barabara zinazoingia nakutoka hapa kakola ambapo ndo hasa mgodi huu mkubwa upo.kijiji hiki kinapakana na mkoa wa geita kwa upande mmoja na wilaya ya kahama kwa upande mwingine.kutoka pande zote hizo mbili kuja hapa hazizidi kilomita 78.
Barabara zote hizi zina hali mbaya kwakweli ikilinganishwa na thamani ya rasilimali za madini zilizopo eneo hili.aibu zaidi ni kuwa tuna wabunge wetu wawili(mbunge wa jimbo la msalala na mbunge wa nyang'wale) ambao kimsingi ndio wawakilishi wetu lakini hatuoni msaada wao katika hili.hasa huyu mbunge wa msalala hatumuoni kabisa akitembelea jimboni kwake mpaka siku za kampeni zikisogea ndio huonekana.
Juzi nilipata kutembelea wilayani msalala nikitokea hapa kakola,hali niliyoikuta ilikua mbaya na aibu sana katika barabara hii.
Na hizi ni picha ambazo zmetoka katika maeneo kadhaa ya barabara hii.


Tusaidiane kuwakumbusha hawa ndugu zetu kuwa hayo madaraka ni dhamana na mungu atawauliza siku ya mwisho.
kutoka Kahama,kwenda kakola,mpaka Geita,barabara ni mbaya sana,migodi hii,ingekuwa kilimanjaro,hizi barabara zingekuwa na taa kabisa
 
Nilikuwepo.... ilifanyika karibu na portable water plant.... NDO TUKAPEWA MAKAVU LIVE NA MKAPA KWAMBA WATANZANIA TUACHE WIVU KWA WAWEKEZAJI...

Na John bwana alivyokuwa anajipendekeza kwa wazungu, balaa
Hatari sana......
Maisha haya.....
 
Baada ya Kiwango kufariki, pale paliharibika kutokana na usimizi m-bovu.
R.I.P Kiwango
Na kuna mwingine alifariki akiwa anaendesha gari, mack II nadhani. Alikuwa anatoka kahama na kwamba alishinda kesi akalewa na mwishowe aliingia chini ya body ya lori iliyokuwa juu ya mapipa mitaa bugarama nadhani
 
Na kuna mwingine alifariki akiwa anaendesha gari, mack II nadhani. Alikuwa anatoka kahama na kwamba alishinda kesi akalewa na mwishowe aliingia chini ya body ya lori iliyokuwa juu ya mapipa mitaa bugarama nadhani
Marehemu Kidiku, alikua na dada yake aliitwa Pondo na kaka yake mwingine aliitwa Mnyama, wote walikua Security Department.
Kidiku alikua ndio kwanza amemchumbia Jane aliekua security reception, na alifariki akiacha wamezaa mtoto mmoja na Jane.
R.I.P Kidiku....
 
Marehemu Kidiku, alikua na dada yake aliitwa Pondo na kaka yake mwingine aliitwa Mnyama, wote walikua Security Department.
Kidiku alikua ndio kwanza amemchumbia Jane aliekua security reception, na alifariki akiacha wamezaa mtoto mmoja na Jane.
R.I.P Kidiku....
Yeah.. Jane namkumbuka sana....That was very sad kwa kweli
 
Huyu mbunge wa msalala ni aibu kuona bado anaendelea na ataendelea kuongoza maana inadhihirisha ni jinsi gani wasukuma walivyo vi........
 
Mnanikumbusha mbaali Sana. Nilikua na Bibi pale Segese. Ntobo. Kahama. Kagongwa na Isaka. Wasukuma hawajui NO. 2000 ...2004
 
Kakola ilitakiwa kuwa mbali sana kimaendeleo pengine kuliko Shinyanga, Geita na hata Kahama kulingana na historia yake ya kuwa na rasilimali nyingi hasa dhahabu ambapo Karibu kila upande kuna mining camps sio Bulyanhulu tu hata Nyangalata, Nyakagwe na vimaeneo vingine vingi tu leo ukienda Kakola pale hata Zahanati hakuna, hata kituo cha polisi hakuna, maji hakuna. Kakola itaendelea kufanya drama ya kuchagua viongozi wanaojali matumbo yao mpaka lini?

Jamii ya Kakola ibadilike, iwakatae viongozi wajinga wasiojielewa hata wawe wanatoka chama gani kwani hakuna badiliko la maana waliloleta labda kukiondoa kigenge cha wavuta bange kule shule ya msingi hilo ndio pekee nawapongeza.
 
Nakuna migodi midogomidogo ya wachimbaji wadogo kama vile nyangalata,usulwangili,nyakagwe,kaloe n.k kodi selikali wanachukua tena mtu akihila ndo wanabana sana eti kuna asilimia wanachukua lakini hamna maendeleo yeyote
Kuhila ndio nini mkuu.
 
Kabla haijaitwa Barrick......
Ilikua ikiitwa Kahama Mining Cooperation Limited (KMCL).
Hapa ndipo nilipo shuhudia alicho pewa mkapa kama zawadi siku ya ifunguzi wa uzalishaji.
Ufunguzi huu nakumbuka ulifanyika ndani ya moja ya ghala la kuhifadhia madawa wakatiule likiwa bado jipya........
Na kisha baada ya Mkapa kupewa kile kilicho itwa zawadi...... Nakumbuka kilifungashwa na mmoja wa wakubwa wa kitengo cha ulinzi kwa jina la John Bwana, na kisha aliibeba zawadi ile kwenye sanduku madhubuti (safe box)...... Haooooo wakalipeleka kwenye uwanja wa ndege pale Bulyanhulu, tena zawadi ile ikiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Miaka hiyo nlkuwa mtoto nilikuwa mtoto, nlkuwa naona gari zinaijia wafanyakazi asbh hlf jioni zinawarudisha kijijini, zilikuwa hizi gari kubwa za mchanga tulikuwa tunaziita skansika, wafanyakazi wengi walikuwa wanakaa kwny gesti mbili hivi, moja ilikuwa inaitwa Rose
 
Nimekumbuka siku nilipo ng'oa mzigo pale kibasini, kisha nikaenda kupanda nao DASH-8..... Mzigo hauja pandisha majini..... .... Ilibidi ndege igeuke na kutua kwa dharura huku wakidhani kwamba ndege imetekwa....
Na hapo ndipo ilipo anzia sheria ya kwamba..... Yeyote anae taka kumpandisha mdada kwenye ndege ya kampuni, lazima athibitishe kwamba ni mkewe....
Hatari sana DASH-8......
Hahahha kumbe ninwewe duuuh..sku hiz dash haipo buana.
 
kutoka Kahama,kwenda kakola,mpaka Geita,barabara ni mbaya sana,migodi hii,ingekuwa kilimanjaro,hizi barabara zingekuwa na taa kabisa
Kwahyo kumbe na sisi watu wa kanda ya ziwa ni tatizo..
 
Back
Top Bottom