Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
- Thread starter
- #21
Highlander,sawa ni kweli unaamini hivyo,kuwa si kila walichofikiri wazee wetu wa kale kina makosa.Mimi pia nakubaliana na hapo kuwa sio vyote walikosea,tatizo langu ni kwenye hicho unachodai unaamini,tafsiri rahisi ya kuamini ni kukubali jambo bila ya kuwa na ushahidi,ukishakua na ushahidi inakua sio imani ni fact.Sasa sijui imani yako ikoje hapa.Kuamini kuna matatizo yake,unaweza kuamini hata kwenye jambo ambalo halileti maana.Na hili lako halileti maana,unawezaje humrithi mke wa kaka yako au kufanya nae ngono na ukaona ni sawa?Hii inaleta maana kweli?Pia suala la kufanya ngono na mwanamke zadi ya mmoja kwa wakati mmoja nao ni ujinga mwingine.Hivi imani ya kuamini mwanaume hawezi kuishi bila kuwa na wanawake wengi inatoka wapi?Tumechagua kutafuta namna ya kuhalalisha udhaifu wa kijinga matokeo yake tunatengeneza mila za hovyo tukidhani ni kuwa hornest!
Last edited by a moderator: