Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Kwa makabila mengine sina uhakika,lakini uchagani nina uhakika.Pia sijui kama jambo hili linafanyika hata leo.Ni kwamba,kwenye familia anapozaliwa kijana wa kiume,na jogoo akawa hapandi mtungi,au akawa hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito,kijana hutakiwa kuoa lakini inapohitajika mtoto,huitwa ndugu wa tumbo moja wa mume kisha kuingia na kukutana kimwili na mke wa kaka/mdogo wake na mtoto atakae patikana huhesabiwa wa mwenye mke!Ki ukweli hapa kwa mtazamo wangu wazee wa zamani walichemsha unless wanifafanulie kilichokuwa kinawafanya wasiwafundishe watoto wao wasijikubali.Ila sidhani kama jambo hili lipo siku hizi.Kama lipo nafikiri ni wakati wa kulipiga vita hata kwenye makabila mengine kwani ni udhalilishaji wa utu!Wewe unaonaje?Walikua sawa?