Kwenye hili,wazee walichemsha . . . . . . !!!!

Eiyer

JF-Expert Member
Apr 17, 2011
28,258
20,709
Kwa makabila mengine sina uhakika,lakini uchagani nina uhakika.Pia sijui kama jambo hili linafanyika hata leo.Ni kwamba,kwenye familia anapozaliwa kijana wa kiume,na jogoo akawa hapandi mtungi,au akawa hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito,kijana hutakiwa kuoa lakini inapohitajika mtoto,huitwa ndugu wa tumbo moja wa mume kisha kuingia na kukutana kimwili na mke wa kaka/mdogo wake na mtoto atakae patikana huhesabiwa wa mwenye mke!Ki ukweli hapa kwa mtazamo wangu wazee wa zamani walichemsha unless wanifafanulie kilichokuwa kinawafanya wasiwafundishe watoto wao wasijikubali.Ila sidhani kama jambo hili lipo siku hizi.Kama lipo nafikiri ni wakati wa kulipiga vita hata kwenye makabila mengine kwani ni udhalilishaji wa utu!Wewe unaonaje?Walikua sawa?
 
kaka wanataka kukudowea wa ubavu wako! kama halipandi kuwa mpole! ila nimewahi kusikia kuna biashara ya sperm, ina inaingizwa kwa mwanamke bila kuingiliwa.Hayo mabo ya mila za zamani sinahakika kama bado yapo tena labda wenzangu waje kufafanua
 
Walikuwa sawa kabisaaaa! Wewe unajua zamani LEVEL YA IGNORANCE, NA SEGREGATION ILIVOKUWA JUUU, Alafu mtu aonekane HANISI!!!!! SI ANGENYANYASIKA SANA KATIKA JAMII??? Angetengwaje!!!! Angebaguliwaje? Angedharauliwaje? Kwa kuona kuwa hilo swala litakuwa AIBU YAO WENYEWE WENYE UKOO WAKAONA WAMSITIRI NDUGU YAO!!!! Watu wa nje wanamuona bonge ya RIJALI MUAMINIFU!!! LOL! EVERY BODY IS HAPPY!!! KUFUNGUKA KASORO ZAKO MBELE YA HII JAMII YETU YA WANAFIKI SI JAMBO RAHISI!!!! Hata mimi kama nina ndugu hata na leo, NITAMUUNGA MKONO ACHEZE DILI LA KUSITIRI UTU WAKE!!!! NAUNGA MKONO HOJA!!!
 
Kumbe ndiyo maana watoto wengi wa kichaga ima hufanana na baba zao, wajomba hata babu zao! Hapa nimekupata. Kama ni hivyo basi kuna wachaga wengi jogoo hapandi mtumbwi. Na hili la mtu kutembea na kaka au mjomba unalisemeaje mwanangu? Maana kupitia hapa jamvini watu wengi walikuwa wakilaani ile tabia ya anko anko na kaka. Sina ushahidi wa hili ila nasikia wamachame na wapare wanaongoza kwenye kamchezo haka ambako twaweza kuita incest.
 
kaka wanataka kukudowea wa ubavu wako! kama halipandi kuwa mpole! ila nimewahi kusikia kuna biashara ya sperm, ina inaingizwa kwa mwanamke bila kuingiliwa.Hayo mabo ya mila za zamani sinahakika kama bado yapo tena labda wenzangu waje kufafanua

Kwa nini unadhani kila akiandikacho mtu kinamhusu?
 
Walikuwa sawa kabisaaaa! Wewe unajua zamani LEVEL YA IGNORANCE, NA SEGREGATION ILIVOKUWA JUUU, Alafu mtu aonekane HANISI!!!!! SI ANGENYANYASIKA SANA KATIKA JAMII??? Angetengwaje!!!! Angebaguliwaje? Angedharauliwaje? Kwa kuona kuwa hilo swala litakuwa AIBU YAO WENYEWE WENYE UKOO WAKAONA WAMSITIRI NDUGU YAO!!!! Watu wa nje wanamuona bonge ya RIJALI MUAMINIFU!!! LOL! EVERY BODY IS HAPPY!!! KUFUNGUKA KASORO ZAKO MBELE YA HII JAMII YETU YA WANAFIKI SI JAMBO RAHISI!!!! Hata mimi kama nina ndugu hata na leo, NITAMUUNGA MKONO ACHEZE DILI LA KUSITIRI UTU WAKE!!!! NAUNGA MKONO HOJA!!!

Unadhani unaweza ukahifadhi maji kwenye gunia?
 
Kumbe ndiyo maana watoto wengi wa kichaga ima hufanana na baba zao, wajomba hata babu zao! Hapa nimekupata. Kama ni hivyo basi kuna wachaga wengi jogoo hapandi mtumbwi. Na hili la mtu kutembea na kaka au mjomba unalisemeaje mwanangu? Maana kupitia hapa jamvini watu wengi walikuwa wakilaani ile tabia ya anko anko na kaka. Sina ushahidi wa hili ila nasikia wamachame na wapare wanaongoza kwenye kamchezo haka ambako twaweza kuita incest.

Sidhani kama upo sahihi hapo!
 
Kwa makabila mengine sina uhakika,lakini uchagani nina uhakika.Pia sijui kama jambo hili linafanyika hata leo.Ni kwamba,kwenye familia anapozaliwa kijana wa kiume,na jogoo akawa hapandi mtungi,au akawa hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito,kijana hutakiwa kuoa lakini inapohitajika mtoto,huitwa ndugu wa tumbo moja wa mume kisha kuingia na kukutana kimwili na mke wa kaka/mdogo wake na mtoto atakae patikana huhesabiwa wa mwenye mke!Ki ukweli hapa kwa mtazamo wangu wazee wa zamani walichemsha unless wanifafanulie kilichokuwa kinawafanya wasiwafundishe watoto wao wasijikubali.Ila sidhani kama jambo hili lipo siku hizi.Kama lipo nafikiri ni wakati wa kulipiga vita hata kwenye makabila mengine kwani ni udhalilishaji wa utu!Wewe unaonaje?Walikua sawa?

Hii mada ni safi. Mkuu Eiyer, makabila mengi katika Afrika mali ya mwanafamilia mmoja inakuwa mali ya familia nzima. Mila hii ina vijifaida vyake, lakini matatizo ni mengi. Mtizamo wa kijasiriamali utapendekeza mila hii ifutwe, kwani ukianzisha duka ujue ni la familia, na hii ni mbaya sana. Watakuja watu wakataka kula wasipopanda.

Lakini unaweza kuototeza mazuri ya mila hii pia, ninavyoona mimi, hasa pale itapohusu kwa mfano hili unalolisemea hapa. Mke wa mwanafamilia mmoja anakuwa mke wa familia. Uzuri unakuja wapi? Chukulia anapokufa mume. Tabia hii iliruhusu mke, watoto na majukumu yote ya yule mume aliyekufa yachukuliwe na mume wa karibu zaidi na marehemu. Of course hili linakuwa na sura mbaya kidogo enzi hizi za ukimwi kwa sababu moja ya majukumu hayo ilikuwa ni pamoja na kulala na mke wa marehemu kumuondolea ile shida ya kukosa mume. Lakini ukiliangalia kwa karibu, kama si ukimwi, mi kwa kweli sioni tatizo hapo! Unalea watoto na kila kitu cha marehemu.

Katika kabila yangu wazee walikuwa wanaombaa ridhaa ya Mke mkubwa wa mume aliyehai, lakini pia mke mfiwa alikuwa anapewa demokrasia ya kuchagua mwanamume anayemtaka kumrithi katika ukoo wa marehemu mume wake. Mfiwa alifanya uchaguzi kwa kumnywesha pombe togwa mke mkubwa wa mume aliyemchagua. Mke mkubwa akiwa amekubali kushea mume alikuwa anakubali kunywa lile pombe togwa analopewa na mke mfiwa. Wakinywa pamoja wanawake wanaokuwa pale chumbani saa hizo za usiku wanakuwa mashahidi kuwa wale kina mama wamekubali kushea mume.

Sasa nije kwenye mada yako: Mke wa ndugu yako amekuja kuongeza familia. Huu nadhani ndio mtizamo wa makabila mengi. Na kwa bahati mbaya, Mwafrika alimchukulia mke kama property ya mume. Pale juu tuliona mali za mwanafamilia mmoja ni mali za familia. Kwa hiyo basi, inakuwa sawa kusema mke ni mali ya familia iliyooa. Na ujue hapo kuwa familia zilikuwa zinaoza mabinti zao kwenye familia. Na hakuna kuvunja udugu huo wa familia mbili.

hili la mwisho nadhani utakuwa ni moja ya misingi ya kutaka mwenye kizazi katika watoto wa familia hiyo amtie mimba binti kwa maana ya kubaki katika familia iliyooa. Mi sioni tatizo hapo kwa kweli... Labda tu hofu ya wivu na hasira za yule asiyekuwa na kizazi. Lakini halo pengine si tatizo kwa sababu atakuwa anafanya kwa hiari kama lile la kuridhiwa katika kabila ya kwangu. Au we Eiyer unasemaje
 
Kumbe ndiyo maana watoto wengi wa kichaga ima hufanana na baba zao, wajomba hata babu zao! Hapa nimekupata. Kama ni hivyo basi kuna wachaga wengi jogoo hapandi mtumbwi. Na hili la mtu kutembea na kaka au mjomba unalisemeaje mwanangu? Maana kupitia hapa jamvini watu wengi walikuwa wakilaani ile tabia ya anko anko na kaka. Sina ushahidi wa hili ila nasikia wamachame na wapare wanaongoza kwenye kamchezo haka ambako twaweza kuita incest.
hao jogoo wanaopanda mitumbwi ni wa wapi ndugu?....huku kwetu wanapanda mitungi
 
ngoja waje wenyewe lol
kwani wewe sio mzee? lol

Kwa makabila mengine sina uhakika,lakini uchagani nina uhakika.Pia sijui kama jambo hili linafanyika hata leo.Ni kwamba,kwenye familia anapozaliwa kijana wa kiume,na jogoo akawa hapandi mtungi,au akawa hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito,kijana hutakiwa kuoa lakini inapohitajika mtoto,huitwa ndugu wa tumbo moja wa mume kisha kuingia na kukutana kimwili na mke wa kaka/mdogo wake na mtoto atakae patikana huhesabiwa wa mwenye mke!Ki ukweli hapa kwa mtazamo wangu wazee wa zamani walichemsha unless wanifafanulie kilichokuwa kinawafanya wasiwafundishe watoto wao wasijikubali.Ila sidhani kama jambo hili lipo siku hizi.Kama lipo nafikiri ni wakati wa kulipiga vita hata kwenye makabila mengine kwani ni udhalilishaji wa utu!Wewe unaonaje?Walikua sawa?
mwanaume kushindwa kuzalisha ni the worst nightmare for most us, hasa kijijini ambapo elimu ni ndogo na unyanyapaa ni mkubwa. ukisikia flani hasimamishi basi huyo mtu alikuwa anadharauliwa kupita maelezo. wazee walikuwa wanafanya hivo kulinda heshima ya ukoo na zamani hapakuwa na IVF, they did the best they could with the little resources they had.
 
Unadhani unaweza ukahifadhi maji kwenye gunia?

SASA JE! Mbona WANAUME KIBAO WANABAMBIKWA WATOTO NA WALA HAWASTUKI!!! SIRI YA KATA AIJUAE MTUNGI! UNALEA TU HUKU MKEO ANAJISEMEA MOYONI WE LEA TUUU ILA UNGEJUA NIMEKUCHAKACHUA KWA MBILIMBI!!!
 
Highlander,asante kwa mchango wako mzuri sana,ila kuna kitu ambacho huwa sikubaliani nacho.Kitu hicho ni kufanya maamuzi kwa sababu bandia.Mfano ulioutoa wa kukubali kumrithi mke kwa nyakati zile lakini ukakataa kwa nyakati hizi kwa sababu ya ukimwi hapo ndipo penye tatizo.Unafanya jambo,japokua ni sahihi lakini kilichokufanya ufanye ni chepesi ni bandia hakina uzito.Yaani kungekua hakuna ukimwi ungekubaliana na mila hii!Highlander,hivi binadamu mwenye akili timamu na anaefikiri kwa usahihi anaweza kumrithi mke au kulala na mke wa ndugu yake?This is insane.Sane people can't do such thing.Naomba mkuu unipe sababu zinazotosha kuhalalisha jambo hili!
 
Last edited by a moderator:
Mitumbwi na mitungi kwangu sawa tu mwanangu uzee tena. Nilimaanisha mitungi nisameheni baba yenu.
 
SASA JE! Mbona WANAUME KIBAO WANABAMBIKWA WATOTO NA WALA HAWASTUKI!!! SIRI YA KATA AIJUAE MTUNGI! UNALEA TU HUKU MKEO ANAJISEMEA MOYONI WE LEA TUUU ILA UNGEJUA NIMEKUCHAKACHUA KWA MBILIMBI!!!

Lara,suala la kulea mtoto asie wako sidhani kama linahusika hapa!
 
Lara,suala la kulea mtoto asie wako sidhani kama linahusika hapa!

Linahusika sana, hapo ni kukuonesha kuwa USIPOJUA MTOTO SI WAKO HUTOMBAGUA WALA KULETA VURUMAI KWA MKEO!! Na kwa mahanisi pia ilikuwa hivohivo JAMII AMBAVO HAIKUJUA KUWA YULE MTU NI HANISII ILIMPENDA, ILIMUHESHIMU, WALA HAIKUMBUGUDHI tofauti na ingejua ukweli!
 
Linahusika sana, hapo ni kukuonesha kuwa USIPOJUA MTOTO SI WAKO HUTOMBAGUA WALA KULETA VURUMAI KWA MKEO!! Na kwa mahanisi pia ilikuwa hivohivo JAMII AMBAVO HAIKUJUA KUWA YULE MTU NI HANISII ILIMPENDA, ILIMUHESHIMU, WALA HAIKUMBUGUDHI tofauti na ingejua ukweli!

Wewe unafikiri ni sahihi kumbagua mtu kwa kuwa hana uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito?
 
Highlander,asante kwa mchango wako mzuri sana,ila kuna kitu ambacho huwa sikubaliani nacho.Kitu hicho ni kufanya maamuzi kwa sababu bandia.Mfano ulioutoa wa kukubali kumrithi mke kwa nyakati zile lakini ukakataa kwa nyakati hizi kwa sababu ya ukimwi hapo ndipo penye tatizo.Unafanya jambo,japokua ni sahihi lakini kilichokufanya ufanye ni chepesi ni bandia hakina uzito.Yaani kungekua hakuna ukimwi ungekubaliana na mila hii!Highlander,hivi binadamu mwenye akili timamu na anaefikiri kwa usahihi anaweza kumrithi mke au kulala na mke wa ndugu yake?This is insane.Sane people can't do such thing.Naomba mkuu unipe sababu zinazotosha kuhalalisha jambo hili!


Naomba niwe muwazi katika hili Mkuu Eiyer, kwamba mchango wangu hapa kwa leo ni wa kiimani zaidi kuliko kuwa ya kielimu.

Mimi nimetokea kuamini kuwa si kila walichofikiri na kutenda babu zetu kilikuwa na makosa. Hili la kumzalisha mke wa kaka yako au mdogo wako ni moja katika hayo ambayo nataka kuyaunga mkono, sababu zikiwa hizo ambazo wachangiaji wengine wamezitoa pia.

Sasa kwenye hili la kurithi, hata kama ni katika hizi enzi za ukimwi, hebu chukulia kuwa huyu bwana anaerithi kwa bahati nzuri hana virusi, na ikatokea bahati nzuri kuwa mjane hana virusi; hivi kweli wewe Eiyer, pamoja na uwezo wako wote huo wa kufikiri huwezi kuona kwamba ina maana kubwa kwamba mjane asiingizwe kwenye hatari ya kutafuta kuridhishwa na watu baki huko mtaani, ambao pengine watakuwa si salama?

Haya. Huo ni mtazamo wa kuepusha kumwambukiza huyu mjane ukimwi kwa kumpa iliyo salama katika ukoo. Kumbuka pia kuwa kuna upande wa binadamu ambao si tofauti sana na wanyama, yaani kwamba kuna wanaume wanaweza kufanya wanawake hata watatu kwa siku bila kuchoka--kama jogoo lenye afya vile. Where is the problem!!!

Unajua Eiyer, binadamu ni mnyama mnafiki sana. Anaeza jifanya ana mmoja, lakini ile sirka yake ya mnyama dume inabaki palepale. Atapiga sehemu mbili mchana na usiku mke hatakaa ajue. Kwanini lisiwe tu wazi kikaeleweka. Hapo sasa ndo unakuja kujua kuwa Waafrika wa zamani hata kama tunawasimanga kuwa walikuwa na akili ndogo, lakini ingalau walikuwa wakweli, wawazi, na kwa kiwango kikubwa sana walikuwa waadilifu in their own way.

Let us be honest. Hivi kweli wewe Eiyer uwezi kupiga sehemu mbili tatu kutwa na hao wote wasijue kama umeshapiga sehemu? Be honest now..... Kwanini lisiwe tu wazi. Babu zetu walichagua kuwa honest. Kurithi mke wa mdogo wako au kaka yako mi navyoona ilikuwa sehemu tu ya kukiri kuwapo uwezo huo katika binadamu wa kiume lijali. Where is the problem?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom