Kwenye hili wakristo mna la kujifunza

Kwenye hili wakristo mna la kujifunza

comrade_kipepe

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2019
Posts
6,447
Reaction score
11,505
Kuna jamaa muislamu kaoa ndoa moja simple sana yani, no mc, no mbwembwe!

Wakati wa saa moja kasoro ile kufuturu jamaa kaoa hapohapo, watu wametulia kwenye mkeka na vikombe vya uji wanajitafunia zao maandazi, shekhe aliefungisha ndoa kapigwa buku 5 tu ya maji.

Yani ndoa mpaka inakamilika haijazidi hata elfu 50.

Hawa jamaa kwa upande huu nawakubali sana.

Wakristo sasa utakuta ndoa inagharimu mamilioni.
 
Kuna jamaa mslamu kaoa ndoa moja simple sana yani, no mc, no mbwembwe!

Wakati wa sa1 kasoro ile kufuturu jamaa kaoa hapohapo, watu wametulia kwenye mkeka na vikombe vya uji wanajitafunia zao maandazi, shehe aliefungisha ndoa kapigwa buku5 tuu ya maji.

Yani ndoa mpaka inakamilika haijazidi hata elfu50.

Hawa jamaa kwa upande huu nawakubali sana.

Wakristo sasa utakuta ndoa inagharimu mamilioni.
Kupanga ni kuchagua
 
uzito wa ndoa kwenye Christianity ni tofauti kabisa na islam, ndoa ya islamic pia inavunjika mara moja wakati wowote ule, kama unaelewa Christianity kuna ubatizo, komunio na ndoa hizo ni hatua muhimu katika maisha ya Christian na ndiyo maana zote zina sherehe ubatizo una sherehe, komunio ina sherea na vilevile baba lao ndoa pia, hivyo ni tofauti kabisa, muslims hawana kitu kama hicho na ndoa kwa muslims ni kama haina maana sana kwa kuwa ndiyo maana inaweza kuvunjwa muda wowote ule na pia inaweza kufungwa hata na wanawake 4 siyo kitu special kwani kinaweza kurudiwa mara nyingi kwa muslims vs Christians ndoa ni hatua muhimu sana ktk maisha ya Christians na kwahali ya kawaida ni mara moja tu katika maisha ya mwanadamu, hivyo ndiyo maana Christians wanasherehekea na ndiyo maana ya maisha, watu wanaishi wakiwa na kumbukumbu ya ndoa yao ilivyokuwa wana album na picha nzuri za sherehe wanazitunza kama kumbu kumbu na hii yote ndiyo maana ya maisha, inaleta faraja.

fikiria ulishawahi labda kuangalia picha za graduation yako sekondari au hata chuo miaka iliyopita hauoni kama inaleta kumbu kumbu na furaha fulani kwamba ni ukurasa ktk maisha yako ambayo hauwezi kurudi tena ni tofauti kama hauna, hivyo hiyo ndiyo moja kati ya sabubu pia ya Christians kufanya ndoa kuwa siku muhimu kabisa ktk maisha yao kwani haitakuja kutokea tena, kwa hiyo ni sawa kusherehekea ...
 
Kuna jamaa mslamu kaoa ndoa moja simple sana yani, no mc, no mbwembwe!

Wakati wa sa1 kasoro ile kufuturu jamaa kaoa hapohapo, watu wametulia kwenye mkeka na vikombe vya uji wanajitafunia zao maandazi, shehe aliefungisha ndoa kapigwa buku5 tuu ya maji.

Yani ndoa mpaka inakamilika haijazidi hata elfu50.

Hawa jamaa kwa upande huu nawakubali sana.

Wakristo sasa utakuta ndoa inagharimu mamilioni.
Umasikini wako si wa wenzako
 
Kumekuwa na ndoa zinazofungwa kiislam ila sherehe yake inafanyika ukumbini huku bi arusi akivalia shela kama mkristo na bwana naye akivalia suti ila huko walikofungiwa ndoa na sheikh walivalia mavazi ya kiislam, ukumbini wakavalia kikristo. Huko ukumbini inafanyika sherehe ya gharama kubwa, watu wanakaa meza moja watano, vinywaji vya kila aina kabla ya msosi. Bufee ni ndefu, misosi ya kila aina mpaka inabidi tu uchague vya kula. Ni ufahari mtupu, mbwembwe ni nyingi. Cha ajabu huoni uislam ukumbini watu wamevalia kimagharibi wote
 
Back
Top Bottom