Kweli watu wema bado wapo

Kuna binti alimuelekeza vibaya kituo cha kuchuka mzee mmoja,yule mzee alikua anaenda ubungo stend na binti anaenda tegeta alipomueleza ashuke kumbe sio kituo basi gari likapitiliza mpaka terminal ya simu 2000 binti akapanda gari ya tegeta mzee akajitwika mizigo yake anarudi ubungo kwa miguu,akiwa ndani ya bus huku mvua inanyesha akamuona yule mzee akielekezwa njia ya rahisi kurudi ubungo,binti akamuomba dereva asimamishe gari akashuka akamkodia pikipiki ndo nae akapanda gari nyngine.Naamini WEMA BADO WAPO.
 
Vitu kama hivyo ukidhulumu utapata tabu sana. Chunga sana amana uliyoachiwa halafu mhusika amekufa....aaah warudishie tu ndugu zake hata kama alikupa mkiwa wawili tu.
 
Mwaka 2012nikiwa musoma mjini, j, mosi saa nne tukipanda mlima wa Kilimanjaro na washikaji zangu watatu. Mara line ya voda ikapokea 650,000/=.nikawaonyesha washikaji tukaenda kutoa fasta. Tukiwa kwa wakala moyo ukauma usiibe,ujui ilitumwa kwa kazi gani? Wewe mkristo kuwa shaidi wa wa injili, nikaailisha kutoa. Lafiki zangu wakaja juu tukatofautiana nilipoailisha kuzitoa. Ilipofika j, tatu nikapokea CM, samahani nilikosea kutuma pesa ijumamosi nikajua niliemtumia kazipata. Ila kanipigia Leo hajapata ndio nacheki naona nilikosea. Tafadhali niludishie nusu ya pesa kwani nilikuwa namtumia mwanafunzi yuko bukoba. Mimi ni Mchungaji wa kanisa la kiroho niko Arusha, wewe uko wapi? Nikamjibu niko musoma mjini. Ata pesa izo nimechangiwa na waumini kijana yuko high school. Nikamjibu niko kwenye bus naenda Mwanza, CM ina arati chaji inaisha, nikifika Mwanza saa Saba nitakutumia zote ila Sina ela kwenye CM ivyo watakata ya kutumi....... CM ikazima!!!. Baada ya masaa mawili nilikuwa Mwanza nikachaji CM kisha nikamtumia PESA 645,000/=. Mara akapiga cm akashukulu kisha akaniambia bwana Mungu wa Israeli akaulinde uchumi wako. Baada, ya wiki tatu nilimtumia Mke wangu PESA ya kodi ya nyumba huko Dodoma. Niliituma siku ya ijumaa shilingi 900,0000/= nikiwa musoma mjini. Jioni yake tuliwasiliana na wife tukapiga story mbili tatu, akuulizia tena kodi nami nikaamiñi alipata PESA. Jumapili pia tuliwasiliana akuniuliza PESA ya kodi nami sigusii nikijua alishalipia. Ijumatatu saa nne akaniulizia kodi!! Nikamwambia mbona nilituma!!, sijapata mie, nilituma ijumaa!. Nikakuta nilikosea kwani nilitumia CM ya Android isio na Batan. Nikaamua kumpigia niliemtumia, akapokea nikamueleza nilikosea kutuma PESA ijumaa. Akasema nilipokea PESA ijumaa kwa namba hii unayotumia, nikawa nangojea unipigie ila ukupiga CM wikendi nzima!. Ivyo niko ofisini muda huu na niko bize, nitakutumia saa Saba muda wa lunch. Kwani uko wapi wewe? Akaniuliza, nikajibu niko musoma mkoa wa Mara. Daah, niko Lindi nachingwea Mimi!! Subili lunch time. OK. Saa Saba na robo PESA ikawa imeludishwa imekatwa ya Kitumb tu!!! Dunia waaminifu wapo.
 
Nilikua nimekaa siku moja sina hili wa lile, basi kuna bi dada mmoja nilikua nimesahau ata kama niliwahi kumtongoza, hamadi napigiwa simu niende nikapewe papuchi, kweli wanawake wema bado wapo.
Aisee that's the greatest WEMA of all
 
Nilikua nimekaa siku moja sina hili wa lile, basi kuna bi dada mmoja nilikua nimesahau ata kama niliwahi kumtongoza, hamadi napigiwa simu niende nikapewe papuchi, kweli wanawake wema bado wapo.
Kwa kizazi hiki unadhani kuna chakushangaa hapo
 
daaaahh kama pepo kweli IPO..kama tunavyoambiwa...bhasi huyo Tayari kesha wekewa makaI take huko...
hayo mambo ya ardhi achana NAyO kabisa. watu wanauwana daily kwaajili ya ardhi..lakini huyo kawatafuta duuhhh...
 
Me nimedhurumu mtu gari aina ya LEXUS SUV na pesa taslimu milioni 20, hakuna watu " WEMA " siku hizi kuna watu " ZARI "
 
Mwaka 2010 Nilimfanyia kazi ya Mageti Jamaa mmoja Mkazi wa Mbeya sehemu moja inaitwa Sayi hakunilipa hela yote kwa sababu ambazo sikuwahi kuzijua kupindi kile maana ilibakia sh.400,000 Nilipiga cm mpaka nikakata tamaa nikafuta namba yake maisha yakaendelea Mwezi ulioisha Nikiwa pale kariakoo Nimepigika na huu Usawa wa Mjomba nilipigiwa Cm namba Ngeni baada yakupokea aliniambia za siku nyingi Fundi nami nikamjibu Nzuri akaniuza uko wapi nikamwambia nipo Ofisini Akasema Ofisini kwako nimepasahau njoo unifuate niko hapa Mtaa wa Narung'ombe nikaenda kusema kweli sikuamini macho yngu Alikua ni yule jamaa Tukaenda mpaka Ofisini Baada ya salaam akaingia mfukoni na kutoa milioni moja kisha akasema "Samahani sana kijana Wngu kipindi kile nilifukuzwa kazi nikayumba kimaisha nisamehe pia Chukua hiki kidogo" Ahsante sana Asulwise mpaka leo siamini kabisa

duuuuhhhh nimoyo wanamna gani huo...huyo Jamaa anamoyo wa dhahabu aiseeee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom