trachomatis
JF-Expert Member
- Jun 7, 2011
- 3,758
- 736
mh..
Mi nakumbuka kuvunjika mkono na kuwekewa P.O.P. mara 2.... Kwa mikono tofauti..
Mi nakumbuka kuvunjika mkono na kuwekewa P.O.P. mara 2.... Kwa mikono tofauti..
Mimi nakumbuka mchezo wa kuendesha baiskeli BMX na video game ya NINTENDO
1. Long tym ukidundwa na wenzako unakimbilia kuita mabro wako wakamrudishie au kumkamata mbaya wako nawe umrudishie,,
2.Nakumbuka ugomvi wa mtaa kwa mtaa mara nyingi chanzo mpira au kuchukuliana mademu
3. Nakumbuka tulitawaliwa na michezo zaidi mf. Soka, kuendesha matairi mabovu ya magari au ringi za baiskeli kitumbo wazi shati umelichomeka kwa nyuma kwenye kibukta
4. Sisi wa dar tushakula fimbo sana baada ya kutoroka kwenda kuogelea baharini tulikuwa tunalambwa chumvi, michanga kichwani au chupi zilikuwa zina kamfuko kwa mbele basi laazma mchanga ukutwe humo/no boxers them days
5. Mwalimu mnoko ilikuwa kudundwa a madenti kawaida enzi hizo watu wanamaliza la saba wakubwaaa sio siku hizi
6.Kindumbwedumbwe kila weekend mtaani
7. Kwenda kuangalia tv au movies kwa jirani mwenye nayo tena unakuwa mnyenyekevu kwenye hiyo nyumba.. Na ilikuwa watoto ambao kwao kuna tv wanaogopewa eti watakupa mapigo ya wakali wa muvi wa enzi hizo chuck noris,bruce lee, van dame na wengine
8. Tobo bao bwanaaaa dah
9. Shati la shule kulipiga pasi vyumbavyumba kama kashata kwa mgongoni obviously pasi ya mkaa ilihusika
10. Ukivaa viatu vya DH/ zile njumu za kitambaa shuleni ilikuwa unataniwa hadi ukome.
Ulikuwa wakishua wewe au wa end 90's
Mambo ya likizo hayo ukienda ushuani labda kwa aunt au hata ndugu wa mbali mwezi december au june ndo hayo mazagazaga unakutana nayo basi full ndalilo unatamani usiku usiingie!!!mimi uswazi nakumbuka nilikuwa bingwa wa kupiga kichuma au ngoma kubwa katika kula daku enzi za ramadhan!kula kula daku mpemba!!!sometimes nilikuwa naenda kama kinyago full masizi usoni!
Mnaikumbuka Raizon ngazi mbili, ngazi 3 ?
- Raba mtoni, pia nyumba Radio cassete National memory Q , ilionekana haina maendeleo.
- ikitambulika kijana anafanya kazi RTC au NMC na anataka kuoa basi wasichana mtaa mzima humtaka na anagombaniwa.
- ikifika saa 2 kasorobo usiku mnajikusanya kusikiliza RTD michezo mtangazaji Abdul Masoud (RIP) Taarifa habari Abdul Ngarawa, Jacob Tesha, Sekioni Kitojo. (wakati huo hapakuepo mwanamke mtangazaji aliyethubutu kusoma taarifa ya habari)
usisahau na busha..yaani unachomeka mpira wa makaratasi ndani ya kaptula juu umevaa gunia..nakumbuka tulikimbizana tokea mwembechai mpaka tandale usiku kugombania hela za kula daku...duh!!!!!zamani raha