Kweli Mungu hana upendeleo?

Kweli Mungu hana upendeleo?

Kama Mungu alimpa Shetani uhuru wa kuchagua kati ya wema na ubaya, kisha shetani yeye akajichagulia ubaya,
Sasa kwanini aadhibiwe ikiwa alipewa uhuru wa kuchagua?

Je, huo ni uhuru au ni kulazimishwa kuchagua wema?

Mfano: Nikikwambia nakupa offer uchague kati ya kahawa na chai, kisha nikakwambia ukichagua chai nitakukata mshahara,
Je, hapo nimekupa uhuru wa kuchagua au nimekulazimisha kuchagua kahawa ili usikatwe mshahara?
Mfano wako wa kahawa na chai haufanani na suala la uhuru wa kimaadili.
Katika mfano wako, mtu anakupa chaguo lakini anakutishia adhabu ya kiholela ili akulazimishe upande fulani. Hapo kweli uhuru unapungua.

Lakini katika uhalisia wa maadili, kinachotokea si tishio la kiholela bali ni matokeo yanayolingana na uchaguzi wenyewe. Uhuru wa kuchagua hauondoi uwepo wa matokeo.

Fikiria mfano wa moto.
Mtu ana uhuru wa kuuweka mkono wake kwenye moto au kuuepuka. Hakuna anayemlazimisha kuuweka mkono wake, lakini akiweka mkono wake kwenye moto ataungua. Kuungua huko si kulazimishwa; ni matokeo ya asili ya kitendo chake.

Au fikiria mkulima anayepanda mbegu.
Ana uhuru wa kupanda mahindi au kupanda miiba. Lakini hawezi kupanda miiba halafu akavuna mahindi. Matokeo yanafuata aina ya mbegu aliyochagua kupanda.

Vivyo hivyo katika maisha ya jamii. Mtu ana uhuru wa kusema ukweli au kusema uongo. Lakini akizoea kusema uongo, polepole watu watapoteza imani naye. Hilo si adhabu ya kiholela; ni matokeo ya uchaguzi wake mwenyewe.

Kwa hiyo uhuru wa kweli unaambatana na uwajibikaji. Kama uchaguzi wote ungekuwa na matokeo sawa, basi mema na mabaya yasingekuwa na tofauti ya kweli. Wema usingekuwa na thamani, na ubaya usingekuwa na uzito wowote.

Ndiyo maana kuwepo kwa matokeo ya uchaguzi hakumaanishi kulazimishwa kufanya wema. Kunamaanisha kwamba uchaguzi wa viumbe una uzito wa kweli.

Na katika mpangilio huo mkubwa wa uhai, sheria na maadili, mwanadamu anapotafakari kwa kina huona hekima iliyowekwa ndani ya uumbaji. Hapo ndipo hutambua kwamba utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa yote na Mwenye hekima isiyo na mwisho.
 
Mkuu hizi mada zingekuaga na Tija sana kama tungekuwa tunajadili kwa hoja zinazofuafa mtiririko wa mantiki.

Mfano: Kusema kwamba Mungu ni mwenye Upendo na Huruma usio na kifani maana yake ni Mungu mwenye Uwezo Mkubwa wa kuzuia Maumivu na Mateso, lakini pia huchukizwa na kuona Mateso na Maumivu.

Kwa mantiki hiyo ni kwamba alipaswa kuzuia mateso na maumivu kwa zaidi ya Asilimia 90.

Sasa inakuaje huyo Muumba anazuia maumivu na mateso kwa asilimia 1 na kuacha maumivu na mateso yaendelea kwa Asilimia 99, Hiyo ni Failure Rate ya 99%.

Majibu yalipaswa kuwa hivi?

1. Sijui kama kuna Muumba Mwenye Huruma na Upendo.

2. Muumba alifanya kazi yake akamaliza akapotelea kusikojulikana na haingilii chochote kinachoendelea duniani.

3. Hakuna Muumba mwenye Upendo na Huruma, wala Muumba mwenye Uwezo. Ulimwengu ulikuwapo na utaendelea kuwapo ukijendesha kwa njia zake.

4. Licha ya kwamba hakuna uthibitisho juu ya Muumba, sisi tumeamua kuwa submissive (wanyenyekevu) juu ya Imani zetu juu ya Muumba.

Science doesn't prove or disprove the existence of a CREATOR, but it can help in investigation of OUR common Religious Beliefs.
 
Kwenye Kutoka anasema yeye ni mwenye wivu eeh!?

Sasa unakua Mungu halafu unakuwa na wivu tena halafu mamluki huwaambii kitu kuhusu huo ushubwada wa Mungu na dini zao. Huyo unaemhisi hayupo, hajawahi kuwepo na hatokuwepo
 
Kwenye Kutoka anasema yeye ni mwenye wivu eeh!?

Sasa unakua Mungu halafu unakuwa na wivu tena halafu mamluki huwaambii kitu kuhusu huo ushubwada wa Mungu na dini zao. Huyo unaemhisi hayupo, hajawahi kuwepo na hatokuwepo
Unaweza ukatuelezea huo wivu wa Mungu ukoje?
 
Acha tumlaumu Shetani

Mfano wako wa kahawa na chai haufanani na suala la uhuru wa kimaadili.
Katika mfano wako, mtu anakupa chaguo lakini anakutishia adhabu ya kiholela ili akulazimishe upande fulani. Hapo kweli uhuru unapungua.

Lakini katika uhalisia wa maadili, kinachotokea si tishio la kiholela bali ni matokeo yanayolingana na uchaguzi wenyewe. Uhuru wa kuchagua hauondoi uwepo wa matokeo.

Fikiria mfano wa moto.
Mtu ana uhuru wa kuuweka mkono wake kwenye moto au kuuepuka. Hakuna anayemlazimisha kuuweka mkono wake, lakini akiweka mkono wake kwenye moto ataungua. Kuungua huko si kulazimishwa; ni matokeo ya asili ya kitendo chake.

Au fikiria mkulima anayepanda mbegu.
Ana uhuru wa kupanda mahindi au kupanda miiba. Lakini hawezi kupanda miiba halafu akavuna mahindi. Matokeo yanafuata aina ya mbegu aliyochagua kupanda.

Vivyo hivyo katika maisha ya jamii. Mtu ana uhuru wa kusema ukweli au kusema uongo. Lakini akizoea kusema uongo, polepole watu watapoteza imani naye. Hilo si adhabu ya kiholela; ni matokeo ya uchaguzi wake mwenyewe.

Kwa hiyo uhuru wa kweli unaambatana na uwajibikaji. Kama uchaguzi wote ungekuwa na matokeo sawa, basi mema na mabaya yasingekuwa na tofauti ya kweli. Wema usingekuwa na thamani, na ubaya usingekuwa na uzito wowote.

Ndiyo maana kuwepo kwa matokeo ya uchaguzi hakumaanishi kulazimishwa kufanya wema. Kunamaanisha kwamba uchaguzi wa viumbe una uzito wa kweli.

Na katika mpangilio huo mkubwa wa uhai, sheria na maadili, mwanadamu anapotafakari kwa kina huona hekima iliyowekwa ndani ya uumbaji. Hapo ndipo hutambua kwamba utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa yote na Mwenye hekima isiyo na mwisho.
Kusema kwamba mfano wangu wa kahawa na chai hauendani, hiyo ni Cognitive bias.

Tutatumia mfano unaoutaka:

Mtu mwenye uwezo wa kuoa wake watano na ana uwezo wa kuwahudumia wote bila shida, akichagua kuwaoa, atachomwa moto, kulingana na vitabu vyenu.

Hivyo atalazimika kuoa mmke mmoja (ukristo) au wanne (islam) ili aepuke adhabu ya Mungu ilihali uwezo na nia ya kuoa zaodi anayo.

Je, huo ni uhuru wa kuchagua au kulazimika kuchagua?

Na, maadili yanapotea wapi hapo, ikiwa mtu mwenye resources, nguvu, akili na uwezo, akichagua kuoa wake wa5, 6,7....?
 
Kusema kwamba mfano wangu wa kahawa na chai hauendani, hiyo ni Cognitive bias.

Tutatumia mfano unaoutaka:

Mtu mwenye uwezo wa kuoa wake watano na ana uwezo wa kuwahudumia wote bila shida, akichagua kuwaoa, atachomwa moto, kulingana na vitabu vyenu.

Hivyo atalazimika kuoa mmke mmoja (ukristo) au wanne (islam) ili aepuke adhabu ya Mungu ilihali uwezo na nia ya kuoa zaodi anayo.

Je, huo ni uhuru wa kuchagua au kulazimika kuchagua?

Na, maadili yanapotea wapi hapo, ikiwa mtu mwenye resources, nguvu, akili na uwezo, akichagua kuoa wake wa5, 6,7....?
Ndugu yangu,

Kwanza, uhuru wa kuchagua haujawahi kumaanisha kufanya chochote bila mipaka.
Kila mfumo wa maadili na kila jamii huweka mipaka fulani. Mtu anaweza kuwa na gari lenye uwezo wa kukimbia sana, lakini sheria inaweka kikomo cha mwendo.
->Hapo hatusemi hana uhuru wa kuendesha gari, tunasema uhuru wake unaendana na utaratibu unaolinda ustawi wa wote.

Pili, hoja yako imejikita kwenye uwezo wa mtu binafsi, ana rasilimali, ana nguvu, ana nia.
->Lakini haijaangalia upande wa pili wa jambo, athari kwa wengine na mpangilio wa jamii.
Ndoa si suala la uwezo wa mwanaume peke yake; ni mfumo unaohusisha haki, wajibu, na ustawi wa watu zaidi ya mmoja. Ndiyo maana mifumo ya maadili huweka mipaka ili kulinda usawa na haki.

Tatu, kama tunajadili kwa mantiki ya kweli, lazima tuulize swali la msingi:
Je, uwezo wa kufanya kitu unamaanisha kwamba kitu hicho ni sahihi kimaadili?
Mtu anaweza kuwa na nguvu ya kumdhuru mwingine, anaweza kuwa na fedha za kuwanyonya wengine, au mamlaka ya kuwakandamiza walio dhaifu. Lakini ukweli kwamba ana uwezo huo hauifanyi tabia hiyo kuwa sahihi.

Hapo ndipo tunatambua kwamba maadili hayajengwi juu ya uwezo wa mtu kufanya jambo, bali juu ya kanuni zinazolinda haki, heshima na ustawi wa wote.

Kwa hiyo hoja ya msingi si kwamba mtu analazimishwa kuchagua, bali kwamba uhuru wa mwanadamu unaambatana na uwajibikaji na mipaka ya maadili.
->Bila mipaka hiyo, jamii ingeongozwa na nguvu ya mwenye uwezo zaidi badala ya haki na usawa.

Karibu Mkuu
 
Mkuu hizi mada zingekuaga na Tija sana kama tungekuwa tunajadili kwa hoja zinazofuafa mtiririko wa mantiki.

Mfano: Kusema kwamba Mungu ni mwenye Upendo na Huruma usio na kifani maana yake ni Mungu mwenye Uwezo Mkubwa wa kuzuia Maumivu na Mateso, lakini pia huchukizwa na kuona Mateso na Maumivu.

Kwa mantiki hiyo ni kwamba alipaswa kuzuia mateso na maumivu kwa zaidi ya Asilimia 90.

Sasa inakuaje huyo Muumba anazuia maumivu na mateso kwa asilimia 1 na kuacha maumivu na mateso yaendelea kwa Asilimia 99, Hiyo ni Failure Rate ya 99%.

Majibu yalipaswa kuwa hivi?

1. Sijui kama kuna Muumba Mwenye Huruma na Upendo.

2. Muumba alifanya kazi yake akamaliza akapotelea kusikojulikana na haingilii chochote kinachoendelea duniani.

3. Hakuna Muumba mwenye Upendo na Huruma, wala Muumba mwenye Uwezo. Ulimwengu ulikuwapo na utaendelea kuwapo ukijendesha kwa njia zake.

4. Licha ya kwamba hakuna uthibitisho juu ya Muumba, sisi tumeamua kuwa submissive (wanyenyekevu) juu ya Imani zetu juu ya Muumba.

Science doesn't prove or disprove the existence of a CREATOR, but it can help in investigation of OUR common Religious Beliefs.
Mkuu, nakubaliana na wewe kwamba mjadala wa aina hii unahitaji kufuata mtiririko wa mantiki na utulivu wa kufikiri. Hilo ni jambo jema sana.

Hata hivyo, kuna sehemu katika hoja yako inayohitaji kutazamwa kwa makini.
->Unasema kwamba kama Muumba ana upendo na uwezo mkubwa basi angepaswa kuondoa mateso kwa zaidi ya asilimia 90, na kwa kuwa hilo halionekani basi kuna “failure rate ya 99%”. Lakini tatizo la kwanza hapa ni kwamba hakuna kipimo cha kisayansi kilichothibitisha asilimia hizo. Ni makadirio ya kihisia. Uhalisia wa dunia haupimwi kwa takwimu za aina hiyo.

Pia mara nyingi tunahesabu mateso kwa uzito mkubwa, lakini hatujali mema yanayotokea kila siku.
Kila siku mabilioni ya watu wanaendelea kuishi, wanapendana, wanasaidiana, watoto wanazaliwa, wagonjwa wanapona na jamii zinaendelea kujengwa. Hivyo picha ya dunia si ya mateso pekee.

Jambo lingine muhimu ni kwamba sehemu kubwa ya mateso duniani yanatokana na matendo ya wanadamu wenyewe.
->Vita, dhuluma, ubinafsi na tamaa za kibinadamu mara nyingi ndizo chanzo cha maumivu mengi tunayoyaona. Hivyo kabla ya kusema Muumba ameshindwa kuzuia mateso, ni haki pia kuuliza mwanadamu anatumiaje akili, rasilimali na uhuru alionao.

Kuhusu sayansi, nakubaliana na kauli yako kwamba sayansi haiwezi kuthibitisha wala kukanusha moja kwa moja uwepo wa Muumba. Sayansi inaeleza jinsi ulimwengu unavyofanya kazi, lakini swali la kwa nini ulimwengu upo kabisa na kwa nini sheria zake zinaruhusu uhai linabaki kuwa eneo la tafakuri pana zaidi.

Kwa hiyo mawazo uliyoeleza, kwamba labda Muumba hayupo au aliumba kisha akaacha ulimwengu ujiendeshe, ni mitazamo inayoweza kujadiliwa. Lakini si hitimisho la lazima la mantiki.
Wapo pia wanaoona mpangilio wa ajabu wa ulimwengu, uwiano wa sheria zake na uwezekano wa uhai kama dalili ya hekima iliyo juu zaidi.

Mwisho wa yote, mwanadamu anapotazama ukubwa wa ulimwengu na mipaka ya maarifa yake, hutambua kwamba uelewa wake ni mdogo kuliko mpangilio wa uumbaji. Hapo ndipo tunanyenyekea na kukiri kwamba utukufu, sifa zote njema, hekima na uwezo usio na mwisho ni wa Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na ardhi, Mmiliki wa uhai na Mjuzi wa kila jambo. Kwake ndiko zinaporudi sifa zote njema na utukufu milele.

Karibu Mkuu.
 
Back
Top Bottom