Katika pitapita zangu nilikutana na Bwana mmoja akanisimulia kisa hiki: siku moja bwana huyo alichukua bibi akaenda naye chemba akiwa na gari lake walipofika maeneo yao ya kujidai bwana yule alipaki gari yake pale, kwa bahati mbaya sana wapambe wakamfuata mkewe na kumwambia wamemuona maeneo hatari mumewe na kwa ushahidi aenda pale atakuta gari limepaki. Mkewe kwa kiwewe mguu na njia hadi eneo husika na kweli alilikuta gari la mumewe kwa hasira akaona asiondoke akae hapo hapo karibu na gari ili mumewe akitoka amnase.
Kwa bahati nzuri yule Bwana alipotaka kutoka tu akamuona mkewe na akapata wazo la kumuita fundi wa gari lake na kumueleza kisa chote na kumuomba yule fundi amfuate pale na afanye ajuavyo aingie mle ndani na kuchukua funguo ya gari lile na kutoka nalo. fundi alifanikiwa akachukua funguo na kuondoka na gari. Mama akabaki na butwaa asijue la kufanya na kurudi nyumbani.
Jioni mama akamsimulia mumewe kuwa ana bahati sana kwani alijua yeye ndiye amepaki gari pale kumbe lilikuwa na fundi. Mumewe kusikia hivyo ilibidi awe mkali na kumchapa vibao mkewe eti kwanini anajifunza tabia hiyo mbaya. Nilisikitika na kumuuliza kwanini uliamua kumpiga wakati unajua ni kweli ulikuwa na makosa? Yule Bwana akanijibu hiyo ndiyo njia mbadala niliyotumia ili asiwe na tabia ya kusikiliza maneno ya watu hasa ukizingatia uzinzi siweze acha.
Hivi uonevu huu kwa kina mama ndani ya ndoa utaisha lini?
Kwa bahati nzuri yule Bwana alipotaka kutoka tu akamuona mkewe na akapata wazo la kumuita fundi wa gari lake na kumueleza kisa chote na kumuomba yule fundi amfuate pale na afanye ajuavyo aingie mle ndani na kuchukua funguo ya gari lile na kutoka nalo. fundi alifanikiwa akachukua funguo na kuondoka na gari. Mama akabaki na butwaa asijue la kufanya na kurudi nyumbani.
Jioni mama akamsimulia mumewe kuwa ana bahati sana kwani alijua yeye ndiye amepaki gari pale kumbe lilikuwa na fundi. Mumewe kusikia hivyo ilibidi awe mkali na kumchapa vibao mkewe eti kwanini anajifunza tabia hiyo mbaya. Nilisikitika na kumuuliza kwanini uliamua kumpiga wakati unajua ni kweli ulikuwa na makosa? Yule Bwana akanijibu hiyo ndiyo njia mbadala niliyotumia ili asiwe na tabia ya kusikiliza maneno ya watu hasa ukizingatia uzinzi siweze acha.
Hivi uonevu huu kwa kina mama ndani ya ndoa utaisha lini?