Mzee Sitta aliwahi kusema ukiamua kuwa mwanasiasa lazima uwe na ngozi ngumu siyo ukigushwa kidogo na kuchubuka unaanza kulalamika, hata ukilalamika hawataacha kukushambulia. Zitto ni mtu maalaufu kuondoka Chadema ni wimbi amabalo haliwezi likapita kimya kimya, wale ambao hawako upande wake watamfanyia vitimbi na wale walio upande wake watamsifu na kumtetea. Ni jambo la kawaida katika siasa. Yeye pamoja na wale walioupande wake wanapashwa kuwa na ngozi ngumu, siyo kulalamika kwa kila jambo analokutana nalo, yatatokea tu, ndiyo siasa hizo, fainali ya hayo yote ni Oktoba 2015.