Kwanini wengi wanaopatana na wazazi na ndugu hudumaa kimaisha, wakati wanaowatupilia mbali ndugu huneemeka?

sijulikani

Member
May 15, 2014
52
89
Zamani kulikuwa na msemoa baba au mama ni baraka. Ukihusiana na baba au mama yako au ndugu zako ni baraka.

Lakini ukweli nilioutathmini katika maisha ni tofauti. Utakubaliana na mimi kwamba watu ambao wameendesha maisha yao huku wakiwa karibu sana na wazazi wao maisha yamewapiga na wengi wao hawajafaulu.

Wamejikita katika umasikini wa kutupwa. Hata kama si umasikini hawafiki kiwango cha maisha mazuri tunayoyaita "kutoboa".

Kinyume chake ni kwamba wale ambao ama waligombana na wazazi na wakaachana nao, au waligombana na ndugu kisha wakaachana nao, ndiyo wengi wamefaulu maisha. Wanakula vizuri, wanasomesha watoto wao vizuri, wanasafiri kwa magari yao vizuri na mambo kama hayo.

Hebu tutafakari na tujadili kwa undani tatizo hili, maana kuna tiatizo zito kwenye jamii yetu tunalificha kw apropoganda potofu. Bahati nzuri ni tatizo linamkuta kila mmoja wetu.

Huenda wazazi wetu na ndugu zetu asili yao ni ukorofi. Nahisi ukorofi wao usingekuwa tatizo kama jamii ingekuwa haiwaungi mkono wanapoonekana wamekorofisha. Lakini jamii nayo inajidanganya kuwaunga mkono na ndiyo maana mtu anapoamua kuwatupilia mbali wazazi na ndugu anajikuta maendeleo yake yanapanda wakati yule aliyebaki anawakumbatia anaishia kuporomoka kimaisha.

Mimi nadhani anaporomoka kimaisha kwa sababu aliishia kufurahisha jamii na kutozingatia ukwlei kwamba ndugu na wazazi ni wakorofi na wadumazaji wa maendeleo.

Naomba tujadili hili, naamini ni kansa iliyoko kwenye jamii inaogopa kujadiliwa.
 
Ndugu yangu wazazi wako ndiyo Mungu wako hapa chini ya jua,Mungu ndiye hupanga maisha ya binadamu,lizika na unachopata.

Mkuu,

Haya maneno tunayajua na ndiyo hutumika kunyamazisha hoja hii muhimu. Lakini hujanipa jibu la swali langu, kwa nini wanaokorofishana wengi wanainuka kimaisha na wanaowakumbatia wengi wanaporomoka kimaisha ukiachilia mbali few cases?

Lete majibu, maana itaelekea kushawishi kwamba kuachana nao ndugu na wazazi ndiko kufaulu maisha.
 
Mbina mimi napatana na wazazi wangu na ndugu zangu wote, cna bifu na mtu na bado kimaisha nmetusua?

Hujapoteza kipato chako ku-maintain huo uhusiano mzuri...

Yaani,ni kua,uhusiano wako wewe na hao ndugu zako haukugharimu gharama yoyote,ni urafiki mzuri tu usio na matatizo..Shida ya husiano zetu na ndugu zetu hapa Africa ni lazima usilipie kodi ndio shida...

Hivyo ni rahisi sana kukuta kipato chako karibu asilimia kubwa inaishia kwenye huo upuuzi,hivyo maendeleo yatakua hafifu kwako,ndio maana wakaksi wanaendelea zaidi ya wazembe wanaotoa kodi kubwa ku-maintain uhusiano na ndugu mbalimbali...
 
Tembelea uswahili uone hizo bifu za familia na maisha bado magumu

Kaka,

Na research yangu nimetembelea uswahili, yaani Mwananyamala, Magomeni, Kigogo, Yombo Dovya, Mabibo na maeneo kama hayo.

Shukrani kubwa kaka, usiishie hapo. Tujadili zaidi tuone ufumbuzi wa tatizo hili.
 
Hujapoteza kipato chako ku-maintain huo uhusiano mzuri...

Yaani,ni kua,uhusiano wako wewe na hao ndugu zako haukugharimu gharama yoyote,ni urafiki mzuri tu usio na matatizo..Shida ya husiano zetu na ndugu zetu hapa Africa ni lazima usilipie kodi ndio shida...

Hivyo ni rahisi sana kukuta kipato chako karibu asilimia kubwa inaishia kwenye huo upuuzi,hivyo maendeleo yatakua hafifu kwako,ndio maana wakaksi wanaendelea zaidi ya wazembe wanaotoa kodi kubwa ku-maintain uhusiano na ndugu mbalimbali...

Mkuu,

Umeiweka vizuri maana watangulizi wako kwenye huu uzi walikuwa wanataka kuiua hii mada. Na ninadhani ni haohao ndugu tegemezi.
 
Sikubaliani na hilo,ila ngoja niingia kwenye mada mojakwamoja.Wafuatao ni BAADHI ya watu waliofanikiwa kwa Fanta hapa Tz. Hebu tuangalie then tufanye ulinganifu na hoja yako.(kuangalia mahusiano na wazazi)
1) Bakhresa
2) Muhamed/ Mo
3) Mengi
4) Ally Mufuruki
5) Diamoond Platnum
6) Marais wetu wa awamu zote
7)Dongote
8) Trump
9) Putin
10) Billgateh
11)Abromo
12) Musukuma/ MB
Haya ni machache tu. Hebu nipe utafiti wako uliofanya
kwa uchache tu.
 
Kwamba ukigombana na wazazi,ndugu ndio unafanikiwa na ukielewana na wazazi ndugu hufanikiwi? Kila siku watu wanazungumzia familia bora na imara, leo wewe unatuambia mkigombana na kutengana ndio chachu ya mafanikio! Jf naipenda kila siku najifunza kitu kipya.
 
Mkuu,

Haya maneno tunayajua na ndiyo hutumika kunyamazisha hoja hii muhimu. Lakini hujanipa jibu la swali langu, kwa nini wanaokorofishana wengi wanainuka kimaisha na wanaowakumbatia wengi wanaporomoka kimaisha ukiachilia mbali few cases?

Lete majibu, maana itaelekea kushawishi kwamba kuachana nao ndugu na wazazi ndiko kufaulu maisha.
kikubwa kinachotokea kwa hawa wanaowatupa ndugu na wazazi ni kwamba hufuta kabisa matumizi(expenditure/spending) kwa ndugu zao na mara nyingi kama ni watu wa kipato saving yao huwa kubwa kuliko hawa ambao huwa wana ushirika na ndugu/wazazi,(baadhi ya cases)
 
Mkuu kama umegombana na wazazi au ndugu zako basi usifanye jf pa kujificha kwa kigezo cha research

Kugombana na yeyote katika maisha ndiyo ubinadamu, huwezi kuepuka kugombana. Na bahati nzuri hunifahamu jina na kama ni ndugu huwafahamu, hivyo it is not harmful.

Lakini si unaona majibu yanavyofululiza humu JF, maana yake ninachokisema kipo kwenye jamii, sikioni peke yangu.

Kumbuka tatizo la UKIMWI lilipoanza walioliongelea waziwazi mliwaita wajinga matokeo yake likaangamiza mnajuka kuanza kulipigia kelele wameshateketea vya kutosha.

Ingekuwa nimegombana mimi nisingeona ni tatizo. Majibu ya wengi humu yanaonyesha ni tatizo. Kama una majibu tuletee ili jamii ipate hamu ya kuishi karibu na ndugu zao, kuliko maneno ya kichinichini kwamba extended family ni mzigo halafu waziwazi mnajifanya mnawapenda kumbe mnafurahisha jamii.
 
Back
Top Bottom