Kwanini wengi huishia kupata hasara kwenye kilimo?

Nebart Chalaji

Senior Member
Feb 15, 2013
143
192
Kilimo kimekuwa kikinadiwa na kupigiwa upatu na wahamasishaji wa aina mbalimbali hususani wale wanaosisitiza kulima kibiashara na kuwapa watu matumaini bila kuwadokeza vitu mhimu ambayo vitawasaidia kuepukana na hasara zinazoweza kuepukika.
Baadhi ya mambo ambayo huweza kusababisha hasara ni kama yafuatayo:
1.UFAHAMU DUNI JUU YA ZAO ANALOLIMA.
Mara nyingi wengi wetu hutaka kuanza kufanya kilimo bila kuwa na uelewa juu ya namna ya kulima,changamoto za magonjwa na wadudu na utatuzi wake na hivyo wengi hujikuta wanafika kati ya uhalibifu na utatuzi hakuna.
SULUHISHO.
Tafuta ufahamu kabla hujaanza ili angalau hata usiibiwe na wasimamizi.
2.UFAHAMU DUNI WA MASOKO.
Hapa wengi hukurupuka kwa sababu ya bei ya mwaka jana.Wengi wamepata hasara pia kwa kusikia zao flani linalipa na hata bila kufanya uchunguzi wa kina wanaishia kuambulia madeni ya mikopo na hasara za kupoteza nyumba zao.Lakini kama angetulia na kutafuta habari za kina juu ya soko la bidhaa hiyoo,huenda asingelima au kulima zao stahiki katika eneo husika.
3.USIMAMIZI MBOVU.
Usimamizi ndio kitu cha kwanza unachotakiwa kufanya kuwa imara sana,lakini imekuwa tofauti kwa watu wengi wanaoingia kwenye kilimo na hivyo kuambulia hasara au kupata mazao chini ya kiwango.Wengi wamekuwa wakiweka wasimamizi ambao kimsingi hawana utaalamu wala uzoefu wowote juu kilimo na hata kutopata utaalamu wa kilimo na hivyo madawa kupigwa under dosage na usimamizi mwingine wa chini ya kiwango na matokeo ni kuambulia hasara.
SULUHISHO.
msimamizi awe anauzoefu au uelewa juu ya kilimo na awe na uchungu na kazi yako vinginevyo utavuna mabua.
4.KILIMO CHA WHATSAAP.
Wengi wa wanaojiigiza kwenye kilimo wamekuwa wavivu kutembelea mashamba yao na hivyo kuishia kuagiza na kutumiwa picha za maendeleo ya zao kwa picha za whatsap.Hili limewaghalimu wengi na wamepata hasara kubwa sana,kwani wasimamizi huweza kutuma picha za mashamba ya watu wengine yenye hali nzuri na hivyo unapata moyo na kutuma pesa ambapo mwisho wa siku unaambulia majonzi.
SULUHISHO.
Kama huna muda wakutosha au msimamizi atayefanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa basi ni vema ukaahilisha.
5.KUTOTATHMINI GHARAMA ZA UENDESHAJI.
Hii pia ni ukurupufu unaopelekea hasara isiyo kifani kwani mtu anamtaji mdogo anataka kulima eneo kubwa na mwisho wa siku anashindwa kugharamia baadhi ya mahitaji kama madawa,mbolea na usimazimizi mwingine na matokeo yake ni kupata mazao ambayo hayarudishi hata mtaji wako.
SULUHISHO.
Kabla hujaanza kulima tafadhali hakikisha unapata taarifa za gharama kwa kina na kutoka kwa watu wanaoaminika.
KAMA KUNA MENGINE WAWEZA ONGEZA.
 
Mleta mada asante sana kwa kuwekea msisitizo vipengele hivyo vinavyoangusha wengi.

Kilimo ni shughuri ya kiuchumi kama biashara nyingine. Kwa anaetaka kufanya kwa tija lazima kujifunza mbinu za ujasilia mali nyingi iwezekanavyo. Mbinu hizo zitamsaidia kujua nini cha kulima, wapi soko, iwapo inalipa au hailipi.

Kilimo kukimudu ni mchakato sio eti kwa vile tu unamtaji, unashamba na soko lipo basi unakurupuka kulima eneo kuubwa kwa zao usilojua undani wake.

DAIMA inashauriwa unapoanza jambo lolote kwa mara ya kwanza anza kwa kiasi kidogo iwe ni robo au nusu ya robo ya mtaji ulionao. Hata kama u mzoefu wa zao unapoanza kulima eneo geni kwako anza na eneo dogo.....hii hukupa fursa ya kujifunza mengi usiyoyajua na ikitokea ukapata hasara hio huwa ni darasa kwako ukaweza kujisahihisha baadae kwa mtaji uliosalia. Kilimo kama umelenga kulima eneo kubwa ni budi upanue taratibu kwa kukua na sio kulipuka.....

Hata hivyo kuna wapo waliowahi kufanikisha kwa kutumia "Mexican style" ... unafanya jambo kwa mara ya kwanza kwa nguvu zote kabisa ikitokea kufaulu inakuwa kwa KISHINDO hasa gumzo la mitaani lakini na ikitokea kuanguka ni MWELEKA WA KARNE CHALI YA MENDE MTU hasimami tena !!! Na wengine hujinyonga....!

Kwa wanaoanza kulima zao fulani kwa mara ya kwanza nawashauri baada ya kuchagua zao la kulima wapoteze muda kutembelea wanaolima zao hilo wakajifunze kwao au wapate mwongozo toka kwao....ikiwezekana kwa vijana wanaweza hata kuomba ajira au kujitolea angalau msimu mmoja wa zao hilo kwa wakulima maarufu wa zao hilo utajifunza mengi sana sana na mbinu nyingi sana utazifahamu....ASANTENI WAJAMEN MM NI YULEYULE KUBOTA SIJUAGI KUANDIKA MANENO MACHACHE NIVUMILIENI......ntachangia tena kuhusu usimamizi eneo lingine pasua kichwa
 
sikuhizi kuna vilimo vya simu sasa hivyo ndo vinaletaga hasara watu wanalima kwa kuulizia tu na sio kwenda kwenye utendaji yaani mashambani
 
Tatizo lingine hata watoa elimu hawajawahi lima.wanafundisha kama walivyosoma kwenye vitabu huko shulen.ningekuwa waziri ningeamuru maafisa ugani wote wawe na mashamba yao binafsi.ili watu wajifunze kule. Ila wengi wao wana maduka ya pembejeo za kilimo.zikiwamo na feki humo humo.
 
Kutochukulia kilimo kama taaluma maalum, na hivyo kudhani yeyote anaweza kulima tu bila kushirikisha wataalamu wa zao husika. Ni kama vile uamue kufanya opareshen ya mgonjwa wako wakati ww siyo dokta, au ujenge ghorofa mwenyewe wakati ww siyo fundi/injinia.. hapo lazima utachemsha tu
 
Mleta mada asante sana kwa kuwekea msisitizo vipengele hivyo vinavyoangusha wengi.

Kilimo ni shughuri ya kiuchumi kama biashara nyingine. Kwa anaetaka kufanya kwa tija lazima kujifunza mbinu za ujasilia mali nyingi iwezekanavyo. Mbinu hizo zitamsaidia kujua nini cha kulima, wapi soko, iwapo inalipa au hailipi.

Kilimo kukimudu ni mchakato sio eti kwa vile tu unamtaji, unashamba na soko lipo basi unakurupuka kulima eneo kuubwa kwa zao usilojua undani wake.

DAIMA inashauriwa unapoanza jambo lolote kwa mara ya kwanza anza kwa kiasi kidogo iwe ni robo au nusu ya robo ya mtaji ulionao. Hata kama u mzoefu wa zao unapoanza kulima eneo geni kwako anza na eneo dogo.....hii hukupa fursa ya kujifunza mengi usiyoyajua na ikitokea ukapata hasara hio huwa ni darasa kwako ukaweza kujisahihisha baadae kwa mtaji uliosalia. Kilimo kama umelenga kulima eneo kubwa ni budi upanue taratibu kwa kukua na sio kulipuka.....

Hata hivyo kuna wapo waliowahi kufanikisha kwa kutumia "Mexican style" ... unafanya jambo kwa mara ya kwanza kwa nguvu zote kabisa ikitokea kufaulu inakuwa kwa KISHINDO hasa gumzo la mitaani lakini na ikitokea kuanguka ni MWELEKA WA KARNE CHALI YA MENDE MTU hasimami tena !!! Na wengine hujinyonga....!

Kwa wanaoanza kulima zao fulani kwa mara ya kwanza nawashauri baada ya kuchagua zao la kulima wapoteze muda kutembelea wanaolima zao hilo wakajifunze kwao au wapate mwongozo toka kwao....ikiwezekana kwa vijana wanaweza hata kuomba ajira au kujitolea angalau msimu mmoja wa zao hilo kwa wakulima maarufu wa zao hilo utajifunza mengi sana sana na mbinu nyingi sana utazifahamu....ASANTENI WAJAMEN MM NI YULEYULE KUBOTA SIJUAGI KUANDIKA MANENO MACHACHE NIVUMILIENI......ntachangia tena kuhusu usimamizi eneo lingine pasua kichwa
umenena mkuu kwa usahihi sana..ni bora watu wajifunze kwanza ili wasiishie kulaani kwamba kilimo si cha kuaminika.
 
Kutochukulia kilimo kama taaluma maalum, na hivyo kudhani yeyote anaweza kulima tu bila kushirikisha wataalamu wa zao husika. Ni kama vile uamue kufanya opareshen ya mgonjwa wako wakati ww siyo dokta, au ujenge ghorofa mwenyewe wakati ww siyo fundi/injinia.. hapo lazima utachemsha tu
kweli mkuu.
 
Tatizo lingine hata watoa elimu hawajawahi lima.wanafundisha kama walivyosoma kwenye vitabu huko shulen.ningekuwa waziri ningeamuru maafisa ugani wote wawe na mashamba yao binafsi.ili watu wajifunze kule. Ila wengi wao wana maduka ya pembejeo za kilimo.zikiwamo na feki humo humo.
Na hata maduka ya pembejeo za kilimo kama madawa ya wadudu na magonjwa wanaouza wengi hawana utaalamu na wanaishia kuwauzia wananchi dawa zisizo stahili au kuwashauli dosage tofauti na inavyohitajika...mwisho wa siku ni hasara kwa mkulima.
 
Kilimo kimekuwa kikinadiwa na kupigiwa upatu na wahamasishaji wa aina mbalimbali hususani wale wanaosisitiza kulima kibiashara na kuwapa watu matumaini bila kuwadokeza vitu mhimu ambayo vitawasaidia kuepukana na hasara zinazoweza kuepukika.
Baadhi ya mambo ambayo huweza kusababisha hasara ni kama yafuatayo:
1.UFAHAMU DUNI JUU YA ZAO ANALOLIMA.
Mara nyingi wengi wetu hutaka kuanza kufanya kilimo bila kuwa na uelewa juu ya namna ya kulima,changamoto za magonjwa na wadudu na utatuzi wake na hivyo wengi hujikuta wanafika kati ya uhalibifu na utatuzi hakuna.
SULUHISHO.
Tafuta ufahamu kabla hujaanza ili angalau hata usiibiwe na wasimamizi.
2.UFAHAMU DUNI WA MASOKO.
Hapa wengi hukurupuka kwa sababu ya bei ya mwaka jana.Wengi wamepata hasara pia kwa kusikia zao flani linalipa na hata bila kufanya uchunguzi wa kina wanaishia kuambulia madeni ya mikopo na hasara za kupoteza nyumba zao.Lakini kama angetulia na kutafuta habari za kina juu ya soko la bidhaa hiyoo,huenda asingelima au kulima zao stahiki katika eneo husika.
3.USIMAMIZI MBOVU.
Usimamizi ndio kitu cha kwanza unachotakiwa kufanya kuwa imara sana,lakini imekuwa tofauti kwa watu wengi wanaoingia kwenye kilimo na hivyo kuambulia hasara au kupata mazao chini ya kiwango.Wengi wamekuwa wakiweka wasimamizi ambao kimsingi hawana utaalamu wala uzoefu wowote juu kilimo na hata kutopata utaalamu wa kilimo na hivyo madawa kupigwa under dosage na usimamizi mwingine wa chini ya kiwango na matokeo ni kuambulia hasara.
SULUHISHO.
msimamizi awe anauzoefu au uelewa juu ya kilimo na awe na uchungu na kazi yako vinginevyo utavuna mabua.
4.KILIMO CHA WHATSAAP.
Wengi wa wanaojiigiza kwenye kilimo wamekuwa wavivu kutembelea mashamba yao na hivyo kuishia kuagiza na kutumiwa picha za maendeleo ya zao kwa picha za whatsap.Hili limewaghalimu wengi na wamepata hasara kubwa sana,kwani wasimamizi huweza kutuma picha za mashamba ya watu wengine yenye hali nzuri na hivyo unapata moyo na kutuma pesa ambapo mwisho wa siku unaambulia majonzi.
SULUHISHO.
Kama huna muda wakutosha au msimamizi atayefanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa basi ni vema ukaahilisha.
5.KUTOTATHMINI GHARAMA ZA UENDESHAJI.
Hii pia ni ukurupufu unaopelekea hasara isiyo kifani kwani mtu anamtaji mdogo anataka kulima eneo kubwa na mwisho wa siku anashindwa kugharamia baadhi ya mahitaji kama madawa,mbolea na usimazimizi mwingine na matokeo yake ni kupata mazao ambayo hayarudishi hata mtaji wako.
SULUHISHO.
Kabla hujaanza kulima tafadhali hakikisha unapata taarifa za gharama kwa kina na kutoka kwa watu wanaoaminika.
KAMA KUNA MENGINE WAWEZA ONGEZA.
Hesabu za Mezani ndio tatizo,
Watu wanakaa mezani wana calculate mazao ya shambani kama vile wana calculate hesabu za soda au bia,
Mtu anakuambia atakua na mashimo 4,000 ya mitikiti, kila shimo ataweka Mbegu 2 na kila Mbegu itatoa Matikiti ma 2, na kila tikiti atauza Tshs 1,000/=. Hakuna kitu kama hiki kwenye kilimo.
Hakuna formula maalumu ya ku-calculate mazao ya shambani.

Mbaya zaidi anaekuambia hivi ni mtu ambae hajawahi kulima hata siku moja. Akishamaliza calculation zake anaingia Shambani tena anaazna na Heka nyingi tu bila kua na Uzoefu. Mazao ya shambani hayanaga idadi maalum ya kuzaa hata ufanyeje.

Pili ni Kilimo cha Simu, maarufu kama Kilimo cha M-pesa. Mtu anajua kabisa hana muda, na baada ya kupigiwa "Hesabu za Mezani" anaingia kwenye Kilimo Kichwa kichwa. Shamba kwenyewe haendi, akiambiwa ni muda wa kupiga Dawa ye anatuma tu hela kwa Kibarua, akiambiwa mbolea hivyo hivyo.

Au hata Shambani kwenyewe anenda kwa ratiba maalumu, tuseme kila Sunday mpaka Vibarua wanajua ratiba zake zote za kuja Shamba. Hapo unamnufaisha tu Kibarua, lazima atapiga tu, labda awe sijui "mlokole" wa aina gani labda
 
Hesabu za Mezani ndio tatizo,
Watu wanakaa mezani wana calculate mazao ya shambani kama vile wana calculate hesabu za soda au bia,
Mtu anakuambia atakua na mashimo 4,000 ya mitikiti, kila shimo ataweka Mbegu 2 na kila Mbegu itatoa Matikiti ma 2, na kila tikiti atauza Tshs 1,000/=. Hakuna kitu kama hiki kwenye kilimo.
Hakuna formula maalumu ya ku-calculate mazao ya shambani.

Mbaya zaidi anaekuambia hivi ni mtu ambae hajawahi kulima hata siku moja. Akishamaliza calculation zake anaingia Shambani tena anaazna na Heka nyingi tu bila kua na Uzoefu. Mazao ya shambani hayanaga idadi maalum ya kuzaa hata ufanyeje.
wengi wanakimbia miji na wengine kuuziwa nyumba zao kwa sababu ya kilimo cha kwenye computer.
 
Dunia nzima hakuna wakulima wafanya kazi. Huwezi kuwa mfanyakazo then mkulima halafu uote kushindana na wakulima full wa hata hapo Kenya au South Africa au Zimbabwe.

Tuna wakulima.wachache mno na.wengi sio wakulima
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom