Haya ni matokeo ya kukua kwa mabadiliko ya kijamii yaliogemea kwenye siasa za mlengo wa kushoto(leftism).
Mabadiliko haya yamekuja na negative impacts nyingi kuliko faida, na moja wapo ikiwa ni hili la kuwepo kwa sheria za mambo ya kifamilia ambazo ni kandamizi kwa mwanaume karibu sehemu zote duniani.
Katika juhudi za kuleta usawa wa kijinsia, wamejikuta hawaleti tena usawa katika ya mwanaume na mwanamke, bali wanageuza au wanahamishia msalaba wa mateso kutoka kwa mwanamke na kwenda kwa mwanaume.
Ndio maana tunasema dunia inatoka kwenye mfumo dume(partriachy) na kuingia kwenye mfumo jike(matriachy/gynocentrism).
Katika dunia hii ya sasa ya mfumo jike ndio tunaona karibu zote na taasisi zote mpaka serikali zimejikita kumwangalia mwanamke, na kumsahau kabisa mwanamke...
...ndio maana unaona hata kwenye sheria za ndoa na familia zinampendelea mwanamke na mtoto, mwanaume anageuzwa kuwa dispasable utility tu wa kutimiza matakwa ya mwanamke na mtoto.
Na hii imepelekea wanawake kugeuza mahusiano kuwa fursa, mtu anazaa na wewe kwa lengo la kujiingia pesa kupitia child support au anaolewa na wewe kisha muda mfupi baadae anakimbilia kufile divorce hili ajipatie mgao.