Kwanini watz tunatumia magari ya kifahari?

Malaria Sugu

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
2,653
264
INASEMEKANA NCHI NYINGI ZILIONDELEA KAMA jAPAN, DENMARK SEREKELI NA RAIA HUTUMIA GARI ZA BEI YA CHINI TOFAUTI NA TZ UTAONA MASHINGI, BMW , LAND CRUSER. KWNINI
 
Mkuu rahisi sana hiyo..miundo mbinu yetu mibovu..barabara hazifai vigari vidogo vinakwama lazima uwe na 4WD's
 
Wataalamu wanaita "conspicuous consumption" yaani kununua vitu ili uonekane shillingi hazikusumbui, na inakuletea ufahari fulani kwenye jamii.
Kuna jamii ambazo zinakumbwa na hili kuliko zengine.
 
Mkuu can you give a source ya unacho kisema? Maana umesema umesikia. Umesikia wapi na kwa nani? Kwa sababu nje kuna watu wana usafiri wa bei mbaya mpaka mengine haya patikani madukani bali kwa special order. So una linganisha wakina nani haswa? Maana hao wenye magari ya kawaida unayo yasema wanaweza wakawa watu wa kawaida na una walinganisha na watu wenye pesa zao bongo.
 
Mkuu rahisi sana hiyo..miundo mbinu yetu mibovu..barabara hazifai vigari vidogo vinakwama lazima uwe na 4WD's

kwa hiyo serikali haitengenezi barabara ili inunue mashangingi au inanunua mashaningi ili isitengeneze barabara.

Na mfano kutoka masaki kwenda posta darisalama kunahitaji shangingi.? Kutoka isamilo mwanza au kapripont kwenda Bomani kunahitaji shangingi?

viongozi wengi wanaona ni part ya status . waziri kuendeshwa kwenye RAAV4 au corolla. anaona kama madaraka yake yatapungua.
 
kwa hiyo serikali haitengenezi barabara ili inunue mashangingi au inanunua mashaningi ili isitengeneze barabara.

Na mfano kutoka masaki kwenda posta darisalama kunahitaji shangingi.? Kutoka isamilo mwanza au kapripont kwenda bomani kunahitaji shangingi?

Viongozi wengi wanaona ni part ya status . Waziri kuendeshwa kwenye raav4 au corolla. Anaona kama madaraka yake yatapungua.
yap.kama utatembelea china na india utaona hivyo
 
INASEMEKANA NCHI NYINGI ZILIONDELEA KAMA jAPAN, DENMARK SEREKELI NA RAIA HUTUMIA GARI ZA BEI YA CHINI TOFAUTI NA TZ UTAONA MASHINGI, BMW , LAND CRUSER. KWNINI
Sioni ubaya wowote mtu kuendesha gari ya gharama, ilimradi hilo gari anunue kwa pesa yake mwenyewe aliyotolea jasho.
 
Mkuu;

Wenzetu nje maisha yao yalishakuwa na tabu sana, akinunua shangingi atakula nini?bei za vyakula,kodi za nyumba ni ghari sana, pia na ushuru wa kumiliki gari nadhani mkubwa sana, umeme maji nk ni ghari sana.Kila kitu kule ni ghari sana.

Mimi nikiwa na shangingi, nikienda mbeya napakia gunia 2 za mchele kwa 60,000,kila moja maharage, na matunda pale chalinze ni bei poaa sana ni kuendesha na kununua na kugeuza,kodi ya nyumba ni 200,000 kwa mwezi.Matumizi yangu in general yatakuwa 300,000mpaka 400,000/tshs kwa mwezi, lakini kule matumizi ukiweka na gari esabia USD 2000, je wataweza.

Si kwamba walianza hivyo mwanzoni waliendesha mashangingi na wengi wakajisahau hakujenga, kwanza kujenga nje si rahisi kama huku, kupata miliki ya kiwanja ni wachache, hivyo maisha ni yakupanga nyumba, Tanzania ukiwa na kibanda chako kwanini usimiliki shangingi make matumizi kwa mwezi mpaka yakifikie hata USD 700 inabidi uwe mtumiaji sana, bado tuna haja ya kumiliki magari mpaka hapo baadae maisha yatakapokuwa magumu, things are chipi bwana here in TZ.
 
Mkuu rahisi sana hiyo..miundo mbinu yetu mibovu..barabara hazifai vigari vidogo vinakwama lazima uwe na 4WD's

Ni excuse isiyofaa. Kwanini wasitengeneza barabara. Na kwanini Jaji wa mahakama Kuu ambaye kazi anafanyia Dar es salaam tu na hatoki nje ya Dar lakini anatumia VX na GX. Kwanini Munadala pale UDSM ambaye umbali kotoka nyumbani hadi Kazini ni chini ka kilomita 7 na barabara si mbaya vileee lakini anatumia gari kama hilo?
 
masikini ndo wenye matumizi makubwa na ya kifahari kwa virasilimali vidogo sana wanavyopata kuliko matajiri na wenye uwezo.tazama hata kwenye aina za simu wale watu wenye kipato cha kawaida ndo wanahangaika na cjui blackbery na aina hizo ilihali hata nyumba amepanga lakini waweza kuta tajiri sana na nokia yake1100 ulimbukeni tu wa kimasikini bila kuangalia vipaumbele vya msingi ndo tatizo letu.
 
Back
Top Bottom