Kwanini watu wananiogopa sana?

Kuwa mkimya na usiye na maneno mengi huwa ina-create nguvu fulani ambayo watu wengi wanashindwa kupingana nazo. Hii pia nimeiona kwa watu wachache na unaweza kuitumia kuwa-intimidate maadui zako
 
labda unafanana na mzee wa fyeeeekelea mbali
 
Umeongea kwa mafumbo lakini kwa mbali nakuelewa! Kuna muda nikikaa kwenye viti vya public au mahali popote public, baadhi ya watu wananikwepa wanaenda kukaa mbali na mimi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thanks mkuu, umeandika mambo mazito sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una hasira hasira za haraka haraka?, uko serious sana?, una tabia ya kujitenga tenga?, una tabia ya kuzira zira, bahiri sana? Mbea mbea? Una ringa na kujisikia saba? Una dharau? Angalia hapo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Mkuu pole sana, hakika watu wa namna hiyo wapo ingawa ni wachache, kwa kawaida kila mtu huwa anayo nguvu fulani ambayo ambayo huathiri mtu mwingine kitaalamu inaitwa "body magnetism (BM)" na zipo BM za aina mbalimbali mfano zipo za mvuto (charisma),za ushawishi,kuogopesha, kukubalika nk, sasa inaweza kutokea mtu fulani akawa na moja kati ya nguvu hizo ikajitokeza zaidi (prevail) kuliko zingine na hapa ndiyo case yako kwamba nguvu ya kuogopesha imejitokeza zaidi kuliko zingine.

Kwakuwa umejitambua basi jaribu kuwa karibu na watu (social), na jaribu kujenga tabasamu na ucheshi unapokuwa na watu kwa njia hii utakuwa unajaribu kuficha ile nguvu ya kuogopesha njia hii inaitwa (forced cover up) na ukiizoe njia hii utajenga tabia na hapo utakuwa umejitibu huo "ugonjwa wa kuogopesha", naita ugonjwa kwa sababu si kitu kizuri kuwa na kitu kinachoogopesha watu "involuntarily", isitoshe ni kitu ambacho hukujitakia. Pole sana mkuu.
 
Asante mkuu... ujumbe mzito huu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KUOGOPWA NA KUCHUKIWA, SIJUI NIFUNGUE UZI??

MIMI NI HIVI,

NIKIFIKA SEHEMU NAOGOPWA NA KUHESHIMIWA KUPITILIZA, HUKO USUKUMANI, WAZEE NA VIJANA WANANSALIMIA SHIKAMOO

WAKINIZOEA SANA, WANANIKOSEA HESHMA KWA UTANI MWIGI,
SIPENDI, UNAJUA WATU WAREFU HATUPENDI BAADHI YA MAUTANI, HASA YA KUSHIKANA NA KUPIGANA,

SEHEMU ZINGINE NACHUKIWA, UNAKUTA NAWEZA JINYENYEKEZA LAKINI MTU AKANITOLEA KAULI MBAYA,

INAWEZEKANA NDO NIMEFIKA TU KWA MARA YA KWANZA OFIS FULANI, MTU AKAANZA KUNIANGALIA KWA JICHO LA KISASI,

AKANIAMBIA HATA MANENO YA KUKWAZA,

KUNA SIKU HUKO DODOMA NILIKUWA NAUGUZA, KILA NIKIPITA GETINI HOSPITALI YA MKOA, WALINZI WANAFUNGUA GETI HUKU LUNDO LA WATU WAMEZUIWA GETINI,

JAMBO LINGINE NI KWAMBA WANAWAKE WANAPATA SANA SHIDA KUNIKATAA,



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni vyema sana kuwaogopa vichaa au yeyote ambao unahisi anaweza kuwa na tatizo LA akili. Nyie watu hata mkimdhuru mtu huwa hamna kesi kabisa. Acha wakuepuke mkuu. Uliza ndugu au wazazi wako kama wapo. Huenda ulishawahi kuugua kichaa na vyeti wamekutunzia wewe hujui ila wanaokuzunguka wanajua. Ndiomaana wanakuanya chief. Pole aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…