edwinito
JF-Expert Member
- Dec 3, 2008
- 210
- 23
Kuna wimbo mmoja wa zilipendwa uliimbwa na bendi ya JWTZ (Jeshi la Wakurya Tangu Zamani???), una kibwagizo......."tuachane kwa wema mamaa, ili tukijakutana popote pale, tusalimiane, ikiwezekana turudiane (of course siyo TUKUMBUSHIANE!!!), cha kujiuliza je, mliachana mkiwa mnapendana? Au nini kilisababisha kutengana kwenu? Kuna rafiki yangu mmoja, yeye alikuwa bado anasoma sec. school, alikuwa na gf wake ambaye kuna siku alimwambia (rafikiangu), achague kusoma au waoane, jamaa akachagua kusoma!! Baada ya miaka kadhaa kupita, jamaa akiwa tayari ameoa na bibie ameolewa, walikutana na kuanza "KUKUMBUSHIA", jamaa wana miaka zaidi ya mitano BADO WANAKUMBUSHIA!!!!!