Kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA?

Kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA?

Bado wauza kofia, bracelets na vinyago
Wauza bar
Vikundi vya ushangiliaji vya Simba na Yanga
Wachambuzi wa mpira
Wasusi na Saloon zinazopamba bibi harusi
Vinyozi
 
Ninajitahidi kuelewa ila nimeshindwa kabisa kuelewa kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA. Kama sherehe ni matukio ya sanaa inabidi hata BURIAL CEREMONIES nako wahusike pia. Wasajili wapishi, wachimba kaburi, na waendesha ibada za maziko.

kwangu mimi hii sheria ya BASATA kusajili hadi wapika keki ni ya kipumbavu zaidi kuwahi kutokea. Ikumbukwe hawa ma-DJ na wapika keki wengi wao wamesoma ila ajira ikawa ngumu ndo wakaamua kujitafuta kwa namna yao bila kuvunja sheria. Sasa mnakuja na sheria za kuwadhibiti badala ya kuwapa moyo kusonga mbele??!!!... mnavyowakatisha tamaa mnataka waende kuwa wahalifu?

Ninawasihi wabunge kufanyia marekebisho sheria hii ya kijinga ili kuzuia huu upuuzi wa BASATA unaoendelea.


Kwahiyo mkuu wewe unapinga wasilipe kodi?

Nilifikiri ungesema wapewe mashine za EFD watoe risiti
 
Kodi kila mahali mpaka sehemu ambazo kuchangia kodi ni kuzidi kumdidimiza mwananchi..!! Serikali haramu inapeleka mambo hovyo hovyo..!!
 
Kwahiyo mkuu wewe unapinga wasilipe kodi?

Nilifikiri ungesema wapewe mashine za EFD watoe risiti
Kuna sehemu nimesema wasilipe kodi? Ninajua kila kipato lazima kilipiwe kodi kwa mujibu wa sheria kupitia TRA. Kama muuza keki ana vigezo vya kulipa kodi basi alipe kupitia TRA kama wapishi wengine na sio BASATA. Keki ni chakula hakihusiani na sanaa.
 
Unapika keki? Mbona umekuwa mkali sana kwenye hili suala wakati kuna mambo mengi tu ya hovyo zaidi ya hili CCM wamekuwa wakifanya na hujawahi kusumbuka?
Mimi sijawahi pika keki na wala sijawahi fanya biashara yoyote inayohusiana na keki. Nimekuwa mkali kwa sababu hili jambo linaenda kuwaathiri vijana wengi wadogo wanaojitafuta.
 
Kuna sehemu nimesema wasilipe kodi? Ninajua kila kipato lazima kilipiwe kodi kwa mujibu wa sheria kupitia TRA. Kama muuza keki ana vigezo vya kulipa kodi basi alipe kupitia TRA kama wapishi wengine na sio BASATA. Keki ni chakula hakihusiani na sanaa.
Mapishi ni sanaa mkuu.

Ulizia wachaga wanavyohaha kupika chapati
 
Mimi sijawahi pika keki na wala sijawahi fanya biashara yoyote inayohusiana na keki. Nimekuwa mkali kwa sababu hili jambo linaenda kuwaathiri vijana wengi wadogo wanaojitafuta.
Funika domo lako wewe mama haukua mkali wakati hao vijana wadogo wanaojitafuta wakati wanapigwa risasi mpaka kufa ujifanye mkali kwa wapika keki matako ya bibi zako.
 
Kuna ubaya gani watu wanaopata mapato kulipa kodi ? Mbona Erythrocyte ulikuwa unaonekana mjanja na mjuzi wa mambo? Kweli nyinyi ndiyo wa kubeza kusanyo la kodi za Mcs na wapika keki?

Mfanyakazi wa Serikali anayelipwa Tsh 500,000 analipa PAYE. Sasa hawa ma Mcs wanaopata harusi 4 kwa mwezi kwa fee ya Tsh 1,000,000 on average kwa mwezi sawa na Tsh 4,000,000 kwa nini wasilipe kodi?

Mc DR Cheni anachaji Tsh 2,000,000 hivyo hapungui Tsh 8,000,000 kwa mwezi, bado mnailaumu Serikali isikusanye eneo hili??

Acheni upimbi bwana, siyo lazima mpinge kila kitu tu kwa vile hamumpendi Samia
 
Back
Top Bottom