Kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA?

Kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA?

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
19,415
Reaction score
40,260
Ninajitahidi kuelewa ila nimeshindwa kabisa kuelewa kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA. Kama sherehe ni matukio ya sanaa inabidi hata BURIAL CEREMONIES nako wahusike pia. Wasajili wapishi, wachimba kaburi, na waendesha ibada za maziko.

Kwangu mimi hii sheria ya BASATA kusajili hadi wapika keki ni ya kipumbavu zaidi kuwahi kutokea. Ikumbukwe hawa ma-DJ na wapika keki wengi wao wamesoma ila ajira ikawa ngumu ndo wakaamua kujitafuta kwa namna yao bila kuvunja sheria. Sasa mnakuja na sheria za kuwadhibiti badala ya kuwapa moyo kusonga mbele??!!!... mnavyowakatisha tamaa mnataka waende kuwa wahalifu?

Ninawasihi wabunge kufanyia marekebisho sheria hii ya kijinga ili kuzuia huu upuuzi wa BASATA unaoendelea.


1774083091231.png
 
Zile keki Zina manenoooo... Nyingine hadi kiziwi anaweza kusikia!

Kwenda BASATA ni too much! Nadhani kuwe na chombo huru ambacho kinaweza ku overruns kila sekta. Kuwe na Baraza la Maadili. Lishughulikie mambo yote kuhusu Maadili ya Taifa na kutoa elimu kwa Wananchi.
 
Ninajitahidi kuelewa ila nimeshindwa kabisa kuelewa kwanini wapika keki wasajiliwe na BASATA. Kama sherehe ni matukio ya sanaa inabidi hata BURIAL CEREMONIES nako wahusike pia. Wasajili wapishi, wachimba kaburi, na waendesha ibada za maziko.

kwangu mimi hii sheria ya BASATA kusajili hadi wapika keki ni ya kipumbavu zaidi kuwahi kutokea. Ikumbukwe hawa ma-DJ na wapika keki wengi wao wamesoma ila ajira ikawa ngumu ndo wakaamua kujitafuta kwa namna yao bila kuvunja sheria. Sasa mnakuja na sheria za kuwadhibiti badala ya kuwapa moyo kusonga mbele??!!!... mnavyowakatisha tamaa mnataka waende kuwa wahalifu?

Ninawasihi wabunge kufanyia marekebisho sheria hii ya kijinga ili kuzuia huu upuuzi wa BASATA unaoendelea.


View: https://www.instagram.com/p/DWHLp-Rj70B/?igsh=YndwODRsdDYzbzE5

tunataka mapato kila kona ya inchi
 
Zile keki Zina manenoooo... Nyingine hadi kiziwi anaweza kusikia!

Kwenda BASATA ni too much! Nadhani kuwe na chombo huru ambacho kinaweza ku overruns kila sekta. Kuwe na Baraza la Maadili. Lishughulikie mambo yote kuhusu Maadili ya Taifa na kutoa elimu kwa Wananchi.
Keki zinavunja maadili?
 
Kinachowa-cost ni fake life.

Mpishi wa keki mteja kampa order amtengenezee keki siku ya kuifata anakuja na Harrier Tako La nyani mpishi anaomba apige nayo picha anairusha kwenye mtandao wabunge wenyewe ndiyo kama hao akina baba level elimu kisoda wakimuona kwanini wasipeleke muswada bungeni kwamba nayo ni biashara inayolipa vizuri?
 
Zile keki Zina manenoooo... Nyingine hadi kiziwi anaweza kusikia!

Kwenda BASATA ni too much! Nadhani kuwe na chombo huru ambacho kinaweza ku overruns kila sekta. Kuwe na Baraza la Maadili. Lishughulikie mambo yote kuhusu Maadili ya Taifa na kutoa elimu kwa Wananchi.
Maadili ya Taifa ni yapi?
 
Back
Top Bottom