Kwanini wakandarasi wa kitanzania hawakui na kufikia kushindana ktk soko la nje?




sawa nakubaliana na wewe ila nchi hii inaweza kuendeshwa na watu wenye Elimu kama hiyo na sivyo mnavyofikiria
 
Nimekwishafanya miradi 6 hadi sasa. Na katika miradi yote nimekuwa nikifanya na makampuni ya nje. Kitu kilichonifanya nianze kuwaza kuhusu hili jambo ni namna ambavyo asilimia kubwa ya miradi inachukuliwa na wakandarasi wa nje. Ukiangalia watendaji katika miradi hiyo yote unakuta asilimia kubwa ni watanzania, kitu ambacho kinanishawishi kuona kwamba technical capability tunayo. Watu wa nje wanakuwa kwenye ngazi ya uongozi ambayo nayo ktk uzoefu wangu, ni wachache ambao unaweza kusema wametuzidi sisi. Mambo mengi tunajadiliana hadi kufikia kuamua tufanye nini, hivyo ktk masuala ya uongozi hatuko vibaya sana.

Nilifanya na kampuni moja nikiwa upande wa client, mambo niliyokutana nayo kutoka kwa wakandarasi wetu wanapoomba kandarasi inatia aibu. Unashindwa hata kuelewa kama watu hawa wanajua kuwa ukandarasi ni biashara na pia ni kazi inayohitaji taaluma fulani. Watu hawawezi hata kutengeneza unit price ambazo ni realistic. Bei zinawekwa tu na ukiomba breakdown ya rate zake hawezi kukupa!

Kuna wenye makampuni ya kitanzania ambao wanajua kuwa akisha saini mkataba basi ile pesa aliyosaini kwenye mkataba ni yake, hivyo haoni haja ya kumobilize resources kwa ajili ya kuanza uzalishaji site. Wanachoweza kufanya ni kutumia hizo pesa kwenye mambo mengine yasiyohusiana na mradi aliopewa.

Sasa kutokana na jinsi nilivyoona ktk maisha yangu ya kazi ndipo nilipotaka kujua uzoefu wa wadau wengine katika fani hii ya ukandarasi na kama kuna mambo mengine nisiyoyajua.

Ninachokifikiri ni kwamba, labda inabidi tuwe na utaratibu au sheria itakayoweka muongozo wa namna ya kuendesha kampuni na hasa za ujenzi. Utaratibu ambao utaweka mamlaka ya kila mtendaji ktk kampuni ili kuzuia wakurugenzi wasio wataalamu kuingilia maamuzi ya kitaalamu.

Nitaendelea baadae.....
 
Mtakuwa saa ngani nanyi mnafanya kazi bila viwango engineer wangu.
kaone pale mbezi stend mpya
kibao cha kuelekeza turn left/right kimeandikwa kwa mkono
kikasimikwa kwenye pipa lililojazwa mchanga, na waziri kabariki kituo.
barabara inawekwa kiraka leo kesho bonge la shimo limeshafumuka pale pale.
hivi kweli kwa kazi kama hizo mtakuwa kweli mkuu wangu.
 
Kwanza kabla ya kusaidiwa ni bora kujisaidia wenyewe kwanza....Jiulize kampuni inakua vipi?! Moja: Organically mbili: Inorganically.
Organically: kikubwa ni through reinvestment of profits into expansion...Kupata facilities zaidi ili kuongeza capacity na pia kuleverage..kutumia deni kuongeza mtaji
Inorgarnically: kushirikiana (JV au consortium), au kuungana, au acquisition....unaweza kuona jinsi PWC walivyopatikana
Sasa wewe kwa miaka kumi uliyokuwa unaoperate kampuni yako imeshakua kiasi gani....in terms of assets,Income, projects value etc, imekua vipi? na ni nini ur expansion strategy next 5 yrs....or medium n short term?!
Sasa kila mtu kama anataka akue yeye tu peke yake ni ngumu hivyo competition will have to correct that..but as u no in Tz competition is not that free or fair n in some cases not open
 
asante sana kwa kuongea ukweli mtupu. ili ni changamoto sana kwetu wa tz. nadhani shida yetu ni kukosa ileinyaoitwa kwa kimombo business acumen
 
Habari kiongozi.. natumai Research yako tayari imekamilika.. tunaomba utupe feedback kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…