Jumong S
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 7,312
- 10,492
Nakumbuka 2010 pale Sinza kwa Remmy nilitokea kukutana na binti mrembo aliitwa Nusra. Aisee alikuwa mzuri haswa. Nilijikuta tu napata ujasiri wa kumkaribia na kumsalimu;
"Dada mambo vipi? Naitwa Jumong, wewe waitwa nani?" Akanijibu naitwa Nusra. Tuliongea mawili matatu akaondoka tukaplan kukutana after siku 3. Yes, niliamua kujipanga. Nikatungua suruali yangu ya kitambaa, pana kama kitambaa cha mashine huku nimevaa shati aina ya dogidogi, mikono kama kengere ya bomani. Chini nilivaa tafubuti za Fubu.
Siku ya tukio binti alipendeza haswaa ila hakukaa japo nusu saa na hata soda moja hakumaliza! Nilijitahidi kutia story nzuri ila wapi! Duh, niliumia sana! Siku nilipomtafuta kwa simu na kumuuliza why alinijibu kifupi tu, "nenda kajifunze namna ya kuvaa kwa wasabato wa mjini." hewala, kumbe siku ile mavazi ndo yalizingua?
Aisee, nakumbuka nilitumia karibu 70% ya mshahara kubadili style ya mavazi next month.
Brothers!
Mavazi nadhifu ni dawa ya mengi. Kuvaa nadhifu huficha umasikini na hukoleza mahusiano. I feel so comfortable katika uvaaji wangu nadhifu sasa! Hata kama unakipato kidogo, nunua mtumba, nenda kwa fundi wa mjini akutengenezee vazi la kisasa.
Sina hakika na sikumbuki nini kilitokea baada ya mabadiliko yangu kwa Nusra.
Popote ulipo Nusra, you were the cause of my looking smart!
"Dada mambo vipi? Naitwa Jumong, wewe waitwa nani?" Akanijibu naitwa Nusra. Tuliongea mawili matatu akaondoka tukaplan kukutana after siku 3. Yes, niliamua kujipanga. Nikatungua suruali yangu ya kitambaa, pana kama kitambaa cha mashine huku nimevaa shati aina ya dogidogi, mikono kama kengere ya bomani. Chini nilivaa tafubuti za Fubu.
Siku ya tukio binti alipendeza haswaa ila hakukaa japo nusu saa na hata soda moja hakumaliza! Nilijitahidi kutia story nzuri ila wapi! Duh, niliumia sana! Siku nilipomtafuta kwa simu na kumuuliza why alinijibu kifupi tu, "nenda kajifunze namna ya kuvaa kwa wasabato wa mjini." hewala, kumbe siku ile mavazi ndo yalizingua?
Aisee, nakumbuka nilitumia karibu 70% ya mshahara kubadili style ya mavazi next month.
Brothers!
Mavazi nadhifu ni dawa ya mengi. Kuvaa nadhifu huficha umasikini na hukoleza mahusiano. I feel so comfortable katika uvaaji wangu nadhifu sasa! Hata kama unakipato kidogo, nunua mtumba, nenda kwa fundi wa mjini akutengenezee vazi la kisasa.
Sina hakika na sikumbuki nini kilitokea baada ya mabadiliko yangu kwa Nusra.
Popote ulipo Nusra, you were the cause of my looking smart!