watu wakisema Ureno ni masikini wana compare na watu kama USA, UK, France etc ila compare na sisi wala sio wenzetu wale.
hizi ni data za pato la mtu mmoja mmoja toka benki ya dunia
-GDP per capita ya Tanzania dola 879
-GDP per capita ya Ureno ni dola 19,813
hivyo unaona utajiri wa mtu mmoja mmoja ni zaidi ya mara 20 ya Tanzania, gape ni kubwa sana. Tuangalie nchi tajiri za kiAfrica.
-south Africa ni dola 5273
-Egpty ni dola 3514
-Nigeria ni 2178
hivyo hata nchi tajiri za ki Africa hazina hata nusu ya uwezo wa kifedha wa mtu mmoja mmoja wa ureno.
tuangalie Nchi tajiri za ulaya
-Uk gdp per capita ni 39,900 usd
-Norway ni 70,812 usd
-france ni 36,854 usd
-italy ni 30,527 usd
hivyo ukiangalia mabwa wakubwa wengine utaona portugal ni masikini compare na nchi kubwa za ulaya.