Binafsi nikifikiria kifo napata hofu. Nawaza je hicho kifo kitasababishwa na nini? Je kitakuwa kifo cha maumuvi au itakuwa katika usingizi nisijue lolote? Kiukweli kifo kinatutatiza wengi. Hata pale tunaposema hatuopogi kifo bado tunakuwa na hofu kidogo tukiwazia kifo na namna kitakavyo tukia.
Nawaza pia namna wapendwa wangu watahuzunishwa na kifo changu. Wakikumbuka mambo mengi mazuri niliyofanya watajisikia vizuri sana lakini watajisikia huzuni kunikosa moja kwa moja. Mawazo yangu, fikra zangu, kazi zangu zitaishi lakini mwili wangu, vile nilivyokuwa nasemezana na wapendwa wangu, kusafiri pamoja, kula pamoja, kufanya kazi pamoja......hayo yote yananifanya niwaze mengi kuhusu kifo. Najua kifo kipo tu na kitatokea siku moja.....lakini hii haiondoi hofu yangu juu ya kifo.
Natamani sana kuishi milele.