Kwanini Unaamini Mungu yupo?

Naaamini unachokisema...

Sababu ni wanatumia nguvu sana kulazimisha absence ya M/ Mungu...

Mara wakulazimishe mtu uwape evidence za uwepo wake, mara ajitokeze asijifiche, Mara kile ilimradi tu kujitoa ufahamu!

Mi toka nione dunia hii hakuna, narudia hakuna kiumbe hai kilichowahi hata tengeneza / umba "a mere fly" ...ilinilazimu kuamini kuna supreme power inacontrol beyond my knowledge!

Post sent using JamiiForums mobile app
Jibu hayo maswali ya mleta mada, acha kukimbia kimbiaa.
 
Mungu yupo ?
Anakaa wapi ?
Anakula chakula gani? ..majani,nyama au mchanganyiko tu
Ana umri gani ?
Analala na kuamka saa ngapi?
Huwa anaoga ?

Ukweli wa jambo haupatikani sababu tu linaungwa mkono na 99% ya watu...

Cha ajabu wanaomini uwepo wa Mungu ndo vinara wa maovu,kutukana,kuingia Jukwaa la Wakubwa(X) humu Jf,utapeli na wizi,unafiki,ugomvi,kukashifiana wao kwa wao(Waislamu V Wakristo) n.k
What a stupidity ?

Mimi naamini katika upendo na kutomfanyia mtu jambo baya ila siamini hili ni dhambi na lile siyo dhambi hivyo nakunywa pombe,nazini n.k sababu tu simkwazi au kumdhuru mtu

Maandiko si yameandikwa samehe 7 X 70 hivyo kama ni ya kweli basi tusio amini uwepo wake tutasamehewa hata 500 X 700,000

Shida ipo wapi ?
Huwez jibiwa hayo maswali na wafia dini zaidi ya kukuogopesha utapata laana
 
Kwa matendo yake makuu hadi sasa nipo na pumzi maana binadam ndicho kilichotushinda kumwekea binadam wa kutengeneza pumzi ambayo ndio uhai tulio nao la sivyo kuna watu wangekuwapo dunia hii hadi leo

Post sent using JamiiForums mobile app
usipo kuwa na pumzi ndo hayupo?
Wanao kufa nao vp?
 
Miongo mingi ilipita kabla ya binadamu kuwepo hali kukiwa na viumbe anuwai katika ardhi,mifumo ya viumbe,gelogia na kutegemeana kwao (heredity ) inaonesha kuwa yuko msimamizi na mastermind wa hii dunia.Lakini msimamizi wa dunia ambae ndie mmiliki anaiendesha dunia kwa utashi na mfumo wake aliopendezwa nao,na sio tupendavyo sisi.
Mifumo (ecosystem) inaonesha wazi ufundi na usanii Mkubwa wa muumba ambaye ndiye mungu,na hakuna mwingine aliyedai umiliki na uendeshaji wa ulimwengu.

Post sent using JamiiForums mobile app
Una ushahidi wa uandikacho?
 
Hayo maswali yako 5 ya juu ni kiboko!
Mimi huwa najiuliza kama kweli huyu Mungu yupo kama tunavyolazimishwa kuamini eti kwasababu tu hatujui chanzo chetu au labda ni kweli tumeumbwa kama wanavyodai, sasa huyu Mungu wanayemsema ye chanzo chake ni kipi??
Ametokea wapi?? Aliumbwa na nani??
Wana komaa kuuliza chanzo cha dunia na viumbe vyote, lkn hawajiulizi chanzo cha mungu.
Wanakuambia mungu hana chanzo alikuwepo tangu enzi? Jibu jepesi kwa swali gumu
 
Mungu yupo kwasababu hata shetani yupo angalia maovu na unyama unaofanyika kutokana na nguvu za giza then nguvu ya nuru ipo action and reaction are opposite but equal to each other
Nguvu za giza ndio zipi?
thibitisha uwepo wa shetan na mungu
acha porojo
 
Science still can't explain why living things die , why a dead body can't be brought into life again while some organs in a fresh dead body can be transplanted into a living body and continue to function as usual.., Absolutely there are several things beyond science!

Sent from my itel it1550 using JamiiForums mobile app
Kama sayansi haiwezi basi imani ndio kabisaaaa....haiwezi hata kumsaidia mtu anaeumwa jino.
 
SOMA
Ushauri Bora.

Unapoenda dukani kununua kitu chochote lazima uulize manual ya bidhaa hiyo ili ujue imetengenezwaje, inatumikaje, inatunzwaje nk.
Hata unapoenda kinunua mbegu ya mmea, kama una ka busara kidogo ni lazima uulizie manual ya hiyo mbegu ili uiamini na kuinunua.

Swali kwa nyie wenye busara

Je umewahi kuiulizia manual yako wewe binafsi ?

Kama hujawahi je zile bidhaa za dukani ni bora kupita wewe ?

Kama sivyo basi wewe utakuwa ni (ashakum sio matusi) mpumbavu sana, kwani unaulizia manual ya redio kaseti na unadharau kuulizia manual yako.

Ewe mwenye busara
Umeshawahi kuiona manual yako ?

Kama hujawahi nakuomba chonde chote anza kuitafuta nina uhakika utaipata, kama manual ya kiberiti inapatikana basi na yako ipo.

Ewe mwenye busara,
Itafute kwanza manual yako inayokuelezea wewe umetengenezwa na kampuni gani, umetengenezwaje (umbo lako), unadumu miaka mingapi, unahalibiwa na nini, unatumikaje nk.
Kama huijui manual yako mwenyewe vipi uiulizie manual ya Mungu ?

Ewe mwenye busara,
kama huijui manual inayokuelezea wewe binafsi basi usiisumbukie ya Mungu ambaye hujawahi kumwona.

Ewe mwenye busara,
ni jambo la ajabu kama vitu dhaifu vina manual, lakini wewe mwenye nguvu na hekima huna manual inayoeleza ASILI na HATIMA yako.

Ewe mwenye busara,
Kama hujawahi kuiona na kuisoma manual yako.
Ni upumbavu uliopindukia kama utajidai eti unaiulizia manua ya Mungu.
(ashakum sio matusi ila ni kuelimishana tu)

Uwe mwenye busara, kuanzia leo jiite mjinga ili uaze kuiulizia manual yako na kujisoma mwenyewe na kujitambua.

Mimi nina busara na ninaijua manual yangu.

BIBLIA TAKATIFU ni manual yangu.
Inaeleza wazi jinsi nilivyotengenezwa, chakua nitakacho kula, masharti nitakayozingatia ili niishi vizuri, umri wa miaka nitakayo ishi, miiko na makatazo ninayopaswa kuyakwepa kufanya, nitakavyo owa mke na kuzaa watoto, nitakavyozeeka, nitakavyo kufa, nitakavyofufuka, nitakavyo enda mbinguni, na huko nitaishi milele nk.

Ewe mwenye busara,
Nani alikuruhusu ule chakula unachokula, maji unayokunywa, mavazi unayovaa, miaka unayoishi, dawa unazokunywa nk ?

Hatima yako ninini baada ya kuzeeka ?

Ivi kifo ndio mwisho wako na busara zako zote hizo ?

Ha..ha...ha..ha...

Niambie Ewe mwenye busara,
Kama huijui manual yako utaijuaje manual ya Mungu ?

Ewe mwenye busara,
Kumbe inaoneka wewe ni mpumbavu uliyepindukia.
Hata mwenyewe hujijui kumbe..!

Usikate tamaa anza kuitafuta manual yako kwanza, muda bado upo, nakuhakikishia utaiona.

Ewe mwenye busara, wacha upumbavu.

Ewe mpumbavu.
Thibitisha mungu yupo!!
Acha ujinga
 
Sababu kuna mambo yametokea kwenye maisha yangu... kwa uwezo wa kawaida isingewezekana , ilitokea tu ajab yakawezekana.
mambo gani una amini kwa uwezo wa kawaida yazingewezekana?
Uwezo gani huo wa miujiza ambao yametibu matatizo yako?
 
Nafikir ungejibu maswali yake moja baada ya lingine.

Post sent using JamiiForums mobile app
Unaweza hata wewe kumsaidia kujibu maswali yangu.

Au hayajibiki? Ukiona hayajibiki basi umeshapata jibu.

Vipi wewe unaejidai tumbo lako, kinyeo chako lakini unashindwa kuzuwia mavi yasitoke ili usiende kushika mavi yako kwa makaratasi.

Au huna uwezo huo? Kama hauna, anao nani?
 
Ukitaka kujua kwamba mungu yupo jitathmini mwenyewe je upo duniani na chake nini? Basi ukipata jibu hicho chanzo cha wewe kuwepo duniani ndio mungu wako
 
Mungu yupo kwasababu hata shetani yupo angalia maovu na unyama unaofanyika kutokana na nguvu za giza then nguvu ya nuru ipo action and reaction are opposite but equal to each other
Usingekaa darasani kusoma sayansi... ungetoa wapi hayo ya actions and reactions?

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Usingekaa darasani kusoma sayansi... ungetoa wapi hayo ya actions and reactions?

Post sent using JamiiForums mobile app

Sasa boss si ndio maana Mungu akaturuhusu tusome ili akili zifunguke na tuzidi kumfahamu kwani ina maana mtu kama unaamni Mungu yupo ndio hutakiwi kusoma boss?
 
Unaweza hata wewe kumsaidia kujibu maswali yangu.

Au hayajibiki? Ukiona hayajibiki basi umeshapata jibu.

Vipi wewe unaejidai tumbo lako, kinyeo chako lakini unashindwa kuzuwia mavi yasitoke ili usiende kushika mavi yako kwa makaratasi.

Au huna uwezo huo? Kama hauna, anao nani?
Mbona unawaza kinyeo tu.... cha kwako kinatumiwa ndivyo sivyo ni nin??....

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom