Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Unakutana na watu Wana hali mbaya mno pale kanisani, wengine wagonjwa mno na hela hawana,

Halafu kama ni msomaji wa Biblia mzuri utagundua kanisa la akina Paulo halikuwa hivi, waliwajali mno masikini na waumini walalahoi. Halikuwa na ubaguzi.


Afu unakuja kuambiwa eti tumchangie mchungaji gari

Alaaaa huu ni upuuzi

Wajinga ndiyo waliwao boss[emoji38] though ni mchungu mno uhalisia huu

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
RC pombe si wanaruhusiwa kunywa au?

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Hizo hela za kumchangia gari mchungaji bora nikawape watoto yatima

Lasivyo bora nipigie bia
 
Mada imenigusa:

Mie sijaacha kwenda kanisani,ila nimepunguza kwenda🙏huku niliko naishi alone,huwa naenda mara moja moja hasa kwenye matukio,kama ekarist nk.

Ila nikirudi nyumbani nilikozaliwa nakukulia hasa likizo,huwa sikosi ibada kuanzia jpil hadi misa za wiki.

Nikienda watembelea wanangu mkoa wanaoishi,huwa mimi na wao hatukosi ibada kamwe🙏hata leo nimezungumza na mwanangu mchana,nikamuuliza kama alienda Chachi,akanambia ;ndio mama nilienda ibada ya watoto na tulifundishwa tuwe na utu na tusaidie wazazi.so utaona kwa upande wa watoto wako vizuri,na hata nikiwa nao nahitajidi wasikose ibada.

Tatizo mimi binafsi nahisi kupungukiwa na nguvu ya kuhudhuria ibada,ingawa nasali mara kwa mara.Nahisi ni changamoto za maisha zinaleta hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…