Kwanini tuumie maovu ya watumishi tunaowaamini yanapoibuliwa?

Kalamu Nzito

JF-Expert Member
Aug 13, 2015
318
662
Hivi karibuni mitandao imeghubikwa na taarifa chafu za aliyekua kiongozi wa kanisa la SCOAN nchini Nigeria, Marehemu TB Joshua.

Watu wengi tulimuamini sana akiwa kama mtumishi wa Mungu. Lakini swali ni kwanini tuumie pale maovu ya mtumishi wa Mungu yanapoibuliwa kwenye jamii?

Inawezekana alifanya na pia inawezekana hakufanya hayo yanayozungumziwa. Tusiwe wepesi sana kutetea na zaidi tusiwe wepesi sana kuhukumu.

Sisi kama wakristo, mafundisho yanaagiza kuweka imani zetu juu ya YESU KRISTO pekee. Hatujaagizwa kuweka imani zetu juu ya watumishi. Watumishi ni binadamu tu nao wana mengi ya kibanadamu ambayo pasipo Roho Mtakatifu huwa wanaanguka kama tuangukavyo wengine.

Nakumbuka mwaka fulani video ya ngono ya mtumishi wa Mungu maarufu hapa Tanzania (sasahivi ni Mwanasiasa) ilivuja mitandaoni. Waumini wake walipambana sana kumtetea.

Waumini tunakua kama vichaa muda mwingine. Tunasahau kwamba huyo ni binadamu tu na ana tabia zake za asili ambazo zinaweza kulipuka muda wowote.

Hatupaswi kuwachukulia watumishi wa Mungu kama malaika. Hata malaika nao walikengeuka (kumbuka habari za Lucifer na malaika wenzake). Kama Lucifer kipenzi cha Mungu alikengeuka, hawa tunaowaita watumishi wao ni nani hata wasianguke katika dhambi?

Wanaosema kwamba kwanini hayakuibuliwa kipindi yupo hai, jibu ni jepesi tu. Kumbukeni taarifa hizi zimeibuka kutokana na shuhuda za wahanga. Isingekua rahisi kwa wahanga kuibuka na kuzungumza wakati mtawala wao alikua bado yupo.

TB Joshua alikua na nguvu na mamlaka hata kwa Serikali za nchi. Kwa Nigeria kanisa lake ni moja ya kivutio cha kuvuta watalii. Halafu unadhani ungeweza kusimama ukaongea mambo hasi juu yake serikali zikuache tu?

Jitihada za kufichua haya hazijaanza kufanyika 2024. BBC walijaribu kumtafuta mmoja wa kiongozi wa sasa wa kanisa la SCOAN na waliishiwa kujibiwa kwamba “Tuhuma kama hizo juu ya TB Joshua zipo tangu zamani na hakuna aliyeweza kuthibitisha”

Kwa kumalizia, kama nilivyoeleza awali. Hatuna uhakika kama alifanya au hakufanya. Pengine inaweza kuwa agenda tu ya kuliangusha kanisa. Ila katika haya yote tujifunze kwamba tunapaswa kumuamini YESU KRISTO pekee.
 
Hao BBC bila shaka wana lao jambo. Maana walianza na Kanisa Katoliki, na sasa wamehamia kwa marehemu Tb Joshua.
 
Hivi karibuni mitandao imeghubikwa na taarifa chafu za aliyekua kiongozi wa kanisa la SCOAN nchini Nigeria, Marehemu TB Joshua.

Watu wengi tulimuamini sana akiwa kama mtumishi wa Mungu. Lakini swali ni kwanini tuumie pale maovu ya mtumishi wa Mungu yanapoibuliwa kwenye jamii?

Inawezekana alifanya na pia inawezekana hakufanya hayo yanayozungumziwa. Tusiwe wepesi sana kutetea na zaidi tusiwe wepesi sana kuhukumu.

Sisi kama wakristo, mafundisho yanaagiza kuweka imani zetu juu ya YESU KRISTO pekee. Hatujaagizwa kuweka imani zetu juu ya watumishi. Watumishi ni binadamu tu nao wana mengi ya kibanadamu ambayo pasipo Roho Mtakatifu huwa wanaanguka kama tuangukavyo wengine.

Nakumbuka mwaka fulani video ya ngono ya mtumishi wa Mungu maarufu hapa Tanzania (sasahivi ni Mwanasiasa) ilivuja mitandaoni. Waumini wake walipambana sana kumtetea.

Waumini tunakua kama vichaa muda mwingine. Tunasahau kwamba huyo ni binadamu tu na ana tabia zake za asili ambazo zinaweza kulipuka muda wowote.

Hatupaswi kuwachukulia watumishi wa Mungu kama malaika. Hata malaika nao walikengeuka (kumbuka habari za Lucifer na malaika wenzake). Kama Lucifer kipenzi cha Mungu alikengeuka, hawa tunaowaita watumishi wao ni nani hata wasianguke katika dhambi?

Wanaosema kwamba kwanini hayakuibuliwa kipindi yupo hai, jibu ni jepesi tu. Kumbukeni taarifa hizi zimeibuka kutokana na shuhuda za wahanga. Isingekua rahisi kwa wahanga kuibuka na kuzungumza wakati mtawala wao alikua bado yupo.

TB Joshua alikua na nguvu na mamlaka hata kwa Serikali za nchi. Kwa Nigeria kanisa lake ni moja ya kivutio cha kuvuta watalii. Halafu unadhani ungeweza kusimama ukaongea mambo hasi juu yake serikali zikuache tu?

Jitihada za kufichua haya hazijaanza kufanyika 2024. BBC walijaribu kumtafuta mmoja wa kiongozi wa sasa wa kanisa la SCOAN na waliishiwa kujibiwa kwamba “Tuhuma kama hizo juu ya TB Joshua zipo tangu zamani na hakuna aliyeweza kuthibitisha”

Kwa kumalizia, kama nilivyoeleza awali. Hatuna uhakika kama alifanya au hakufanya. Pengine inaweza kuwa agenda tu ya kuliangusha kanisa. Ila katika haya yote tujifunze kwamba tunapaswa kumuamini YESU KRISTO pekee.
Umetiririka vizuri mno, ila mwishoni nikaona na wewe kama unatetea'flan kimtindo!

Mimi hupenda kusikiliza habari na kuanza kufuatilia mizania ya 'kubalansi' stori.

Nimesikiliza na kutazama documentary za BBC na kuniacha na maswali mengi na kushangaa namna ambavyo mashuhuda wengi toka sehemu mbali mbali wamejitokeza na kutoa tuhuma nzito dhidi yake.

Tukumbuke kuna habari zinazofanana na hizi kulihusu Kanisa katoliki miaka ya karibuni liliomba radhi kwa vitendo vya kifisadi na kifirauni vilivyofanywa na mapadre na maaskofu wake kwa watoto waliokuwa chini ya uangalizi wao miaka mingi iliyopita, lakini vikafumbiwa macho na kufichwa ili eti kulinda 'kulichafua kanisa'!

Kwa hiyo kwanza tukubaliane kuwa vitendo hivyo vipo na kufanywa na viongozi wa dini wanaoheshimika na kuaminika.

Nadhani kila mtu asikilize mwenyewe vizuri juu ya tuhuma mbali mbali zilizotolewa kumhusu huyo TB Joshua ili aweze kuzitafakari mwenyewe kwa utulivu.

Sasa tuje kwenye hoja yako:

Tuhuma zimetolewa kwamba 'alifanya'.

Cha msingi hapo ni kutafuta habari ya upande mmoja uliobaki nyuma ya tuhumba kama 'hakufanya'.

Inawezekana kweli hakufanya?

Ni vigezo gani vinavyomuondolea uwezekano wa 'kufanya'?

Wanaosema 'alifanya', kama lengo ni kumchafua, kwa nini wanamchafua mtu ambaye tayari alikwisha kufa, ni kwa faida gani na ya nani hasa?

Kwani watu waliohojiwa walikuwa wapo sehemu moja kusema walijipanga kusema uongo?

Utetezi wowote katika tuhuma kama hizi unatakiwa ujiridhishe kwa ushahidi usio na shaka juu ya 'hajafanya' na si kwa hisia, upambe ama ushabiki wa kidini.

Mimi nitabakia na 'alifanya' kichwani mwangu hadi pale wanaosema 'hakufanya' watakapokuja na uthibitisho wa kujitosheleza kuwa 'hakufanya' ili kuishinda hoja ya mashahidi wote waliojitokeza na tuhuma za kusema kuwa 'alifanya'.

Vinginevyo watetezi wa 'hakufanya' kwa bila uthibitisho wowote, nitawaweka kundi moja na lile kundi la waumini na washabiki wa Gwajiboy walioendeleza utetezi wao mpaka leo wa 'hajafanya' na hata baada ya kanda ya video kutoka na kusambaa kuonesha kuwa 'anafanya'.
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Back
Top Bottom