Kwanini TSH inashuka dhidi ya Dollar/KSH, Exchange rate, Deni la Taifa?

Kwanini TSH inashuka dhidi ya Dollar/KSH, Exchange rate, Deni la Taifa?

🤣 🤣 dogo lala tu unaongea pumba! enhe ulivotengeneza fx pesa transactions za wateja ulikua unazituma kwa nan 🤣
nitafte nikufunze jinsi wanavyofanya kazi uko nje. Sio hii ya kuajiriwa unafanya mifumo inavyosema
 
Kada usitake nifunguke nisije kukamatwa kwa kusambaza taarifa zisizo faa za taasisi. Kafatilie Viongozi wa FXpesa Sauzi na google treasury boardkenya 2022 utanikuta
1751140974637.png

kaangalie viongozi wa fx pesa utaniona 🤣 🤣 🤣 , uko confident kuongea pumba
 
Kada usitake nifunguke nisije kukamatwa kwa kusambaza taarifa zisizo faa za taasisi. Kafatilie Viongozi wa FXpesa Sauzi na google treasury boardkenya 2022 utanikuta
labda nkufundishe kitu dogo, hakuna mtu yeyote anaweza kufanya trading ya currencies bila Benki kuu, na endapo utaenda kutrade unafanya kitu kinaitwa SPOT means unaweka cash halisi benki kuu na sio kwa sababu unataka kufanya trading bali kwa kua unamiliki firm, wanashika pesa on your behalf alafu wanakutafutia mwingine anaezitaka
 
central bank zote zinaendeshwa the same same, znatumia mfumo unaitwa contra accounts inside hakuna pesa yoyote ipo deposited kazi yake ni kubeba kitu kinaitwa Negative assets, hata leo mtu akikutumia pesa kutoka nje hakuna pesa inasafirishwa inahesabika tu kama negative asset
kuna Financial action task force FATF wana monitor large some of money zinazoingia Central bank na zilipotoka. Ili kuzia money laundry hii unaojua au unakaa kufanya kazi za kuajiriwa kama mkataba inavyosema
 
Sas mkubwa nianze kuweka tena pesa bank kutoka nje ya nchi wakati najua kuna Financial action task force FATF wana monitor large some of money zinazoingia Cenyral bank na zilipotoka. Uwa hatuachi trace
Sasa ndo umeongea nn apo?
 
Mkuu huwezi kuelewa. Siku ikitokea unataka kutumiwa pesa ndefu kutoka nje ya nchi nitafute iwe ya halali au isiwe ya halali ntakusaidia kusafish vitabu uonekane legit au ukitaka kuanzisha Biashra inayohusiana na miamala ya kifedha connction ninazo za vibali na Team ya ku code interface.

Chukua fomu ugombee kisha kopa deni uone kazi ninayofanya kukusafishia vitabu


mfano. Kama hapo mtapewa visababu vingi muamini lakini kuna wachche wanauelewa mchezo mzima. Escape the matrix be open minded
unaelewa ata unachoongea 🤣
 
stakehigh mkuu BOT naomba uchambuzi wako hapo #52. Na kwa nini mpka leo Paypal imeshindwa kukubaliwa kufanya kaz Tz
 
Wachumi mnakaribishwa kwa michango.........

Tutatumia shiling ya kenya KSH, Dollar na TSh ili kupata uelewa wa jambo ili
Tujue kwanini shilling ya nchi fulani ina nguvu kuliko nyingine, Exchange rate ya pesa nani uamuapia Deni la Taifa.

Moja kwa moja kwenye Point.
Tuanze kwa kujua mchakato wa thamani ya pesa ya nchi fulani inapatwaje.
Ili kupata thamaniya fedha ya nchi fulani parameter hizi huusika pamoja na hesabu za kiuchumi na muelekeo wa soko kidunia kwa siku io
Ili kuipata thamani ya pesa ya nchi fulani vifuatavyo ( parameters) uangaliwa ( ni kama point ukudanywa kwa kila parameter) unaweza kuona nchi flani inakusanya point nyng kuliko nyingne kwnye kigezo hiki

1 Hali ya kiuchumi ya ndani nchi apa purchasing power au uwezo wa kifedha katika shughli za kiuchumi nchini

2 Masharti na vigezo vilivyowekwa dhidi ya wawekezaji wa ndani na nje. Apa wanaangalia interest ya investors wa nje kama wana wez kuwekez nchi ili pato la nchi liongezeke.
KWa uhalisia kenya hapa wana masharti mepesi na nafuu kwa investor wa nje kuliko Tz. Ndo maana kenya ndoinaitwa business Hub of East africa
( japo nchi hio imekua shamba la bibi kwa wageni ntaeleza baadae)
Pia swala la Diaspora na nguvu yake inaingia hapa kwani wanauwezo wa kuja kuwekeza ndani ya nchi. Tz tuna idadi ndogo ya diaspora kwani wao wana acces na dollar na wanauwez wa kuajiri na kutengenez fursa nchini

3 RAsilimali za nchi husika = madini, mbuga, Ardhi, bandari = apa tunaangalia exploitation ambayo inatija na inayoleta faida kwa taifa
Apa tutaona Rasilimali nyingi za kenya zime kuwa exploited kwa uwekezaji kuliko za TZ ambapo bado kuna rasilimali nyingi hazijaguswa bado. Ndo maanaa ya kusem kenya ni shamba la bibi japokuw return inapatikan

4 mapato na makusanyo ndani ya nchi ili kupata GDP

5 hali ya Kiusalama kama vita, Kisiasa pia uchaguz

6 maisha ya wananchi = kuanzia hali ya juu mpka chini bila kujali Matabaka

7 Shughuli za uwekezaji na maedndeleo yanayofanywa nchini kuanzia miundombinu afya.....nk

8 .Uongozi bora na vngine vingi....

Vyote hivi vikikusanywa na kuchakatwa matokeo ndo tunaipa shillingi au pesa ya nchi fulani THAMANI na hpo bdo haijapata thamani kidunia

( kwa hivyo tajwa unaweza kupambanua na wewe pesa ya nchi gani ina thamani kuliko ipi kwa kui score point kwa kila parameter)
.
Kabla ya kwenda kwenye Exchange rate . Utaona kwenye hzo parameter tukianza kuchanganua KSh inakua na Thamani kuliko Tsh na hapo bdo Tsh haijaenda soko la kidunia la Exchange rate ili kupata thamani yake kidunia.

Unaweza kuona nchi kama South Sudani pesa yao ina thamani kuliko Tsh na wamepata uhuru majuzi hii ni kutokana na parameter hizi wana population ndogo pia rasilimali zao kama Uchimbaji wa mafuta unaleta pato kubwa la taifa ambapo ina ipa shillingi yao thamani na point kubwa ata kabla kwenda kupata thamani kwenye exchange rate dhidi ya kipimio ambacho ni Dollar

Ishu ya exchange rate ni nyingine twende huko

Utangulizi ...
Zamani Kipimo ili pesa flani ipate thamani yake kidunia cha exchange rate kipimio kilikua dhahabu Au Gold . Ndipo walipoona kua dhahabu ni kubwa na nzito (Bulky) hivyo itaftwe fedha ya karatasi itakayo kua mbadala ndipo wamarekani wakaona iwe Dollar. Sababu zpo nging kwanini ikawa dollar lakini ni maono makubwa ya marekani ambapo waliona ikiwa Dollar wataendelea kuwa taifa kubwa kiuchumi na lenye ushawishi mkubwa kidunia kwani wao ndo watakua wazalishaji wa dollar

Turudi...

Baada ya kwisha kuipata Thamani ya pesa ya nchi flani kwa kuzingatia parameter zote tajwa hapo juu BASI
Pesa hio inapelekwa kwenye Soko la kifedha la kidunia ili kupata thamani ya pesa hio kidunia kumbuka Dollar ndo kipimio

( mchakato uwa ni uleule kama wa Wazee wa meta trade 4/5 au Forex au wanaolijua soko la Hisa. Wallstreet)

APo tuseme TSh ishapata thamani basi inaingia ili ipate thamani yake kidunia dhidi ya dunia ( kulingana na zile parameter tajwa kule juu mwanzo basi Dollar 1 itathaminishwa kulingana na parameter zote zile tajwa hapo juu ndo thamani hio ya 2600 inapatikana baada ya mahesabu mengi kiuchumi kufanywa kuzingatia sales na trades na siku hio apa kinachopatikana ni exchange rate na sio Thamani ya shillingi. Thamani inatoka kwenye parameter.

Ndo unaona 1 Dollar ni sawasawa na 2600Tsh. Ni kuendana na soko la siku iyo.. ila siku uchumi ukiendelea nchini na parameter zote zikafikiwa basi thamani ya shilling Tsh itaonekana. Na hapo huenda ikashuka hata 1500

Au niseme hivi nchi kama UAE wao wanaendelea vizuri kiuchumi ukizingatia parameters (pato la nchi + parameters wana score kubwa) ndo maana pesa yao inathamani lakini TZ ni kama maendeleo kiuchumi ukichukua parameters mfano pato laifa bado lipo palepale ndo maana ata Tsh haipandi thamani.

Kwa vile Marekani ndo wanaomiliki na kuchapisha dollar na ndo inayo tumika kama exchage rate. Kuna kipindi Dollar ndo inashuka na sio kumaanisha shillingi imepanda.
shilling
Mfano kipindi cha uchaguzi marekan mwaka jana ecxchage rate ilikua 1 dollar ni sawa na 2800 Tsh apa Wanasia wengi walianza kusema eti Tsh imepanda dhidi ya dollar kuwa ni shillingi yetu na uchumi unakua BALi uhalisia ni kuwa shughuli za Kisiasa na uchaguzi zilizo kua zinaendelea marekani ndo ilifnya Dollar kushuka thamani kwani fedha nyingi zilichapishwa na kuingia kwenye mzunguko ili kuakikisha shughuli za kampeni na uchaguzi zinakwendwa vizuri. Ila baada ya uchaguzi hali ya exchage rate ikarudi kama kawaida. Hapo gunajifunza zile parameter kule juu zinavyoweza pia kua athiri soko La Exchange Rate

Note: Echange rate uathiriwa na parameter tajwa hapo juu pia u tegemea na siku husika
Exchange rate vary with parameter mentioned and varies in time

Zingatia Parameter, ziwe kichwani tunapoingia kwenye deni la taifa.

Deni la Taifa
ni pesa ambazo nchi ukopa kwa shughuli za kimaendeleo nchini.
Wanao kopesha pesa hzi ni world bank, IMF, nchi fulani, na taasisi za kifedha

Unaweza kusema kwanini benki kuu wasichapishe pesa ziingizwe kwenye mzunguko ili uchumi uongezeke au ili tusikope.
Kumbuka ni hesabu za kichumi ndo hutumika khipa thamani fedha kwa kuzingatia parameters.
Pesa zikichapishwa na kuingizwa kwenye mzunguko zita athiri parameters na point au thamani ambayo shillingi inakua nayo kabla hata kwenda kwenye soko la exchange rate kidunia

Uhalisia pesa hizo zitaingia mtaani na watu watazitumia kwa wingi na kusababisha mfumuko wa bei kumbuka supply and demand vitu vitapanda bei kwani wafanyabiashara wataona wateja wanapesa ( ndo maana hata siku hizi ongezeko la mshahara ni kimyakimya)

Chamsingi hapa jua kuna machakato wa kihesabu za kiuchumi pia parameter ambazo uwa kama kichujio ili kupata thamani ya pesa ya nchi husika

Turudi kwenye deni.
Kama ilivyo kwa kila mkopeshaji. Wakopeshaji tajwa hapo juu wao pia uwa na masharti yao utaskia ili niwape kiasi hicho cha fedha ni lazima mkubali ucshoga mchini mwenu. Au lazima mkubali chanjo hizi au ugonjwa huu upo. Au lazima mruhusu uwekezaji huu au mniruhudu niwekeze nchini mwenu mnipe badndari niiendeshe
Comes with a price kipindi cha Covid bila kukubali chanjo na ugonjwa ulikua hupati fedha za kukopa


Hivi majuzi nchi ya nigeria imeamua kulipa madeni yote ya nchi na ikawa haidaiwi ili ianzishe mifumo mipya ya kiuchumi nchini.

Kukopa sio kosa bali pesa hizo unazipeleka wapi. Kama ni kwenye shughuli za uwekezaji nchini kama ujenzi wa miundombinu kama baranara, shule, hospitali. Kama apa kwetu deni limeongezeka ila pesa uenda tukasema zimeishia kujenga bwawa ila tukitaka taaarifa rasmi ya feha hizo zilienda wapi ndo tunakosa. Huko sipo . Turudi kwenye mada yetu

Mfano tunao nchini kenya ambapo Kasongo alikubali mkopo wa fedha ili ajenge miundombinu kutoka nchi ya Saudia ambapo alipewa masharti ya kukubali bandari yake iwe route ya kusaidia kusambaza siraha kwenda nchi ya sudani na kushirikiana na kiongozi wa nchi uyo ambae inasemekana analeteleza machafuko sudan.

Maoni yangu apa

Inabidi nchi ione jinsi ya kutumia rasilimali zake vizuri kama vle madini ili mwekezaji anapo kuja faida ipatikane ukijumuisha na kodi na mapato yanayopatina nchi iwe kujiendesha na mapato ya ndani na sio kukopa kisa pato la ndani fedha zake haziwezi jitosheleza kujenga miundombinu ivyo inatulazimu tukope.
Pia serkal iwajibishwe kwa kutoa taarifa zote za wapi fedha zilizokopwa zilipopelekwa. Accountability na transparency ndo changamoto Tz viongozi wanajisahau wanajiona miungu watu na sio wafanyakazi walioteuliwa kuwafanyia kazi na kuwawakilisha wananchi

Turudi kwenye mstari...

Hivi mnaonaje Nchi ikope fadha alaf watu wapewe mitaji na wenye mawazo wa biashara na uwekezaji wapewe pesa ili tuongeze mapato ya nchi. Hapo tutakua tunaimalisha thamani ya shillingi na uchumi kuliko kukopa na kwenda kujenga na miundombinu wakati mapato ya ndani ya mchi yanazidi kudidimia. Nawasilisha

Hvyo niseme Ongezeko la deni la taifa li Reflect Mapato ya ndani ya nchi au project husika pia Accountability na Transparency iwepo

Mfano umekopa Millioni moja umeenda kununua ndege ambayo kwa mwaka inakuingizia laki 6 hii haileti maana, ni mikopo isio na tija ni bora aletwe muwekezaji aje na ndege kuwekeza nchi au fedha hizo wapewe vijana waliomaliza vyuo wakakosa ajira mtaji wajiajiri na wale wa mitaani wajikwamue kisha tutafute njia kuwakata kodi. Apa uchumi utakua shillingi Tsh itapanda thamani na deni la taifa pesa zitakua zinatumika ipasavyo.

Macho yote tuitupie Nigeria kwani ni moja ya nchi isio kua na deni. Je wataendeleaje kukuza uchumi....

Tuachie kwa hapo kwa sasa.
Moderator uzi huu ni wa kutoa elimu kuhusiana na mada husika na kama kuna sehemu ina mu Offend mtu mu i Edit kuliko kufuta uzi mzima.
Uchumi hauwezi kutengamaa kama kuna kiongozi mkuu na genge lake lote nguvu zao zote wameziwekeza kwenye siasa na sio utendaji
 
Back
Top Bottom