Kwanini tende zinahusishwa na Uislamu?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Tende ni kati ya matunda ninayoyapendelea sana. Nilianza kuyatumia kwa kuvutiwa na ladha yake, sikujali sana faida zake kiafya, na wala sikuwa nikizifahamu.

Ni hivi karibuni, tena kupitia nyuzi za humu Jamii Forum, nilifahamu kuwa tende si tunda lenye ladha nzuri tu, bali pia lina faida lukuki kiafya.

Lakini kuna taarifa zilizonishangaza! Kuna watu wanachukulia tende kama chakula cha Waislamu, tena cha wakati wa mfungo wa Ramadhani. Kwa nini watu wamekuwa na mtazamo huo?

Mimi nafahamu, kama sikosei, kuwa Waislamu hupendelea pia kula wali, mihogo, viazi vitamu, n.k. kipindi cha Mfungo. Itakuwa ni sahihi kusema kuwa mihogo na viazi ni chakula cha Waislamu?

Nimeangalia mtandaoni. Tende zinalimwa nchi kadhaa za Asia na zisizo za Asia. Kote huko zinalimwa kwa ajili ya Waislamu?

Hizi ni baadhi ya nchi zinazolima tende: SAUDI ARABIA, IRAN, MOROCCO, MISRI, ISRAEL, CHINA, MAREKANI, QATAR, NIGER, PALESTINA, ALGERIA, OMAN, UNITED ARAB EMIRATES, ALBANIA, MEXICO, SPAIN, UNITED STATES OF AMERICA, CAMEROON, KENYA, BENIN, COLOMBIA, n.k.

Sijaona popote palipoandikwa kuwa tende ni kwa ajili ya Waislamu!

Watu wanaovumisha kuwa tende ni chakula cha Waislamu wana nia gani? Wanataka kuwakosesha wasio Waislamu virutibisho vinavyopatikana kwenye tende?
 
Tende ni kati ya matunda ninayoyapendelea sana. Nilianza kuyatumia kwa kuvutiwa na ladha yake, sikujali sana faida zake kiafya, na wala sikuwa nikizifahamu.

Ni hivi karibuni, tena kupitia nyuzi za humu Jamii Forum, nilifahamu kuwa tende si tunda lenye ladha nzuri tu, bali pia lina faida lukuki kiafya.

Lakini kuna taarifa zilizonishangaza! Kuna watu wanachukulia tende kama chakula cha Waislamu, tena cha wakati wa mfungo wa Ramadhani. Kwa nini watu wamekuwa na mtazamo huo?

Mimi nafahamu, kama sikosei, kuwa Waislamu hupendelea pia kula wali, mihogo, viazi vitamu, n.k. kipindi cha Mfungo. Itakuwa ni sahihi kusema kuwa mihogo na viazi ni chakula cha Waislamu?

Nimeangalia mtandaoni. Tende zinalimwa nchi kadhaa za Asia na zisizo za Asia. Kote huko zinalimwa kwa ajili ya Waislamu?

Hizi ni baadhi ya nchi zinazolima tende: SAUDI ARABIA, IRAN, MOROCCO, MISRI, ISRAEL, CHINA, MAREKANI, QATAR, NIGER, PALESTINA, ALGERIA, OMAN, UNITED ARAB EMIRATES, ALBANIA, MEXICO, SPAIN, UNITED STATES OF AMERICA, CAMEROON, KENYA, BENIN, COLOMBIA, n.k.

Sijaona popote palipoandikwa kuwa tende ni kwa ajili ya Waislamu!

Watu wanaovumisha kuwa tende ni chakula cha Waislamu wana nia gani? Wanataka kuwakosesha wasio Waislamu virutibisho vinavyopatikana kwenye tende?
Hata vilemba na kanzu siyo mavazi ya waislamu, tatizo waislamu wanaupenda Uarabu, unaweza kwenda msikitini kuswali ijumaa ukiwa umevaa suti wala hamna shida yoyote.

Unaweza kwenda msikitini umelipuka pamba vile utakavyo wala haina shida yoyote, lakini mwislamu haliziki bila kuvaa mavazi ya Waarabu mikanzu na misuli.

Hata mjadala huu wa bandari na DP world ukiwahesabu wachache wanaotetea ukiacha wale waliokula rushwa hawa wengine wanatetea kwa sababu ya mahaba yao kwa Waarabu tu na wala hawana hoja yoyote.
 
Kisa na mkasa ni IGA ya DPW, jumlisha MOU ya TEC gawanya na Chuo Cha TANESCO Kwa BAKWATA. Hapo tende ni kipeuo tu kwenye hiyo equation
Huu mlinganyo mgumu sana. Sijaambulia chochote.
 
Hata vilemba na kanzu siyo mavazi ya waislamu, tatizo waislamu wanaupenda Uarabu, unaweza kwenda msikitini kuswali ijumaa ukiwa umevaa suti wala hamna shida yoyote.

Unaweza kwenda msikitini umelipuka pamba vile utakavyo wala haina shida yoyote, lakini mwislamu haliziki bila kuvaa mavazi ya Waarabu mikanzu na misuli.

Hata mjadala huu wa bandari na DP world ukiwahesabu wachache wanaotetea ukiacha wale waliokula rushwa hawa wengine wanatetea kwa sababu ya mahaba yao kwa Waarabu tu na wala hawana hoja yoyote.
Ukimfuatilia Dr zakir yule kumkuta kavaa kanzu ni nadra sana ....


Unajua nn? kuna kitu kinaitwa sunnah yaani sio lazima ila unafuata yale ya mtume aliyofanya ...Mfano hizo tende mtume kama unajua enzi zake zilikuwa zinalimwa sana kwenye jamii yao wa waarabu sasa yeye alikuwa akitumia kufungulia(Ramadhan) ,basi hili tunda likawa kama kikokotezo yaani watu wanaiga ,haina shida kuiga ila mtizamo wa watu wanachukulia kweny dini ila mtu yeyote anaweza kula.

Kufuata sunnah ni njema sana ila unatakiwa kuwa na uelewa ili usilazimishe jambo maana sunnah ni bora ila sio lazima.

Jamii inatakiwa kusoma sana ili kutambua mambo ila mi nasali na suti mara kibao na hata wengi tunasali hivyo maana ni maeneo ya makazi wala hamna tatizo zote ni nguo .
 
Hata vilemba na kanzu siyo mavazi ya waislamu, tatizo waislamu wanaupenda Uarabu, unaweza kwenda msikitini kuswali ijumaa ukiwa umevaa suti wala hamna shida yoyote.

Unaweza kwenda msikitini umelipuka pamba vile utakavyo wala haina shida yoyote, lakini mwislamu haliziki bila kuvaa mavazi ya Waarabu mikanzu na misuli.

Hata mjadala huu wa bandari na DP world ukiwahesabu wachache wanaotetea ukiacha wale waliokula rushwa hawa wengine wanatetea kwa sababu ya mahaba yao kwa Waarabu tu na wala hawana hoja yoyote.
Kwenye suala la mavazi, nafikiri ni suala la utamaduni zaidi kuliko Imani. Namfahamu muhubiri mmoja wa Kikristo kutoka nchini India, yeye vazi lake kuu ni kanzu bila kujali kama yupo kwao India au ugenini Marekani.
 
Mi binafsi si muislam, napenda tende sana, huwa natamani ziwepo muda wote zinakouzwa nikanunue. Sina mipaka ya kula vyakula vinavyodhaniwa ni vya dini fulani. Hata suala la mahusiano ya kimapenzi sina mipaka, nikimpenda binti wa kiislam naye akinipenda imetoka hiyo, mwendo ni mapenzi motomoto. Avae kiislam aende msikitini poa tu, ninachojali ni utu na heshima. Imani ya dini hainuhusu
 
Hayo ya kuvaa kanzu yaliniponza ,bwana bwana si nilinunua kanzu yangu swaafi na kibaraghashia kama muuza alkasusu mashuhuri basi wife si kwa kununa kule kwa madai yake kuwa nimepata mwanamke muislam ndio najipendekeza huko😂
 
Hata vilemba na kanzu siyo mavazi ya waislamu, tatizo waislamu wanaupenda Uarabu, unaweza kwenda msikitini kuswali ijumaa ukiwa umevaa suti wala hamna shida yoyote.

Unaweza kwenda msikitini umelipuka pamba vile utakavyo wala haina shida yoyote, lakini mwislamu haliziki bila kuvaa mavazi ya Waarabu mikanzu na misuli.

Hata mjadala huu wa bandari na DP world ukiwahesabu wachache wanaotetea ukiacha wale waliokula rushwa hawa wengine wanatetea kwa sababu ya mahaba yao kwa Waarabu tu na wala hawana hoja yoyote.

Wanakuja na silaha kali za moto, jiandae mkuu

images (12).jpeg
 
Tende ni kati ya matunda ninayoyapendelea sana. Nilianza kuyatumia kwa kuvutiwa na ladha yake, sikujali sana faida zake kiafya, na wala sikuwa nikizifahamu.

Ni hivi karibuni, tena kupitia nyuzi za humu Jamii Forum, nilifahamu kuwa tende si tunda lenye ladha nzuri tu, bali pia lina faida lukuki kiafya.

Lakini kuna taarifa zilizonishangaza! Kuna watu wanachukulia tende kama chakula cha Waislamu, tena cha wakati wa mfungo wa Ramadhani. Kwa nini watu wamekuwa na mtazamo huo?

Mimi nafahamu, kama sikosei, kuwa Waislamu hupendelea pia kula wali, mihogo, viazi vitamu, n.k. kipindi cha Mfungo. Itakuwa ni sahihi kusema kuwa mihogo na viazi ni chakula cha Waislamu?

Nimeangalia mtandaoni. Tende zinalimwa nchi kadhaa za Asia na zisizo za Asia. Kote huko zinalimwa kwa ajili ya Waislamu?

Hizi ni baadhi ya nchi zinazolima tende: SAUDI ARABIA, IRAN, MOROCCO, MISRI, ISRAEL, CHINA, MAREKANI, QATAR, NIGER, PALESTINA, ALGERIA, OMAN, UNITED ARAB EMIRATES, ALBANIA, MEXICO, SPAIN, UNITED STATES OF AMERICA, CAMEROON, KENYA, BENIN, COLOMBIA, n.k.

Sijaona popote palipoandikwa kuwa tende ni kwa ajili ya Waislamu!

Watu wanaovumisha kuwa tende ni chakula cha Waislamu wana nia gani? Wanataka kuwakosesha wasio Waislamu virutibisho vinavyopatikana kwenye tende?
Hata mimi nashangaa kwani hata kahaba maarufu wa kwenye Biblia ni "Tamari" ambalo tafsiri yake ni tende.

Tena ni kahaba aliyehusishwa, ndani ya biblia, kuwa ni katika chanzo zhanzo cha uzazi wa Yesu.
 
Tende ni kati ya matunda ninayoyapendelea sana. Nilianza kuyatumia kwa kuvutiwa na ladha yake, sikujali sana faida zake kiafya, na wala sikuwa nikizifahamu.

Ni hivi karibuni, tena kupitia nyuzi za humu Jamii Forum, nilifahamu kuwa tende si tunda lenye ladha nzuri tu, bali pia lina faida lukuki kiafya.

Lakini kuna taarifa zilizonishangaza! Kuna watu wanachukulia tende kama chakula cha Waislamu, tena cha wakati wa mfungo wa Ramadhani. Kwa nini watu wamekuwa na mtazamo huo?

Mimi nafahamu, kama sikosei, kuwa Waislamu hupendelea pia kula wali, mihogo, viazi vitamu, n.k. kipindi cha Mfungo. Itakuwa ni sahihi kusema kuwa mihogo na viazi ni chakula cha Waislamu?

Nimeangalia mtandaoni. Tende zinalimwa nchi kadhaa za Asia na zisizo za Asia. Kote huko zinalimwa kwa ajili ya Waislamu?

Hizi ni baadhi ya nchi zinazolima tende: SAUDI ARABIA, IRAN, MOROCCO, MISRI, ISRAEL, CHINA, MAREKANI, QATAR, NIGER, PALESTINA, ALGERIA, OMAN, UNITED ARAB EMIRATES, ALBANIA, MEXICO, SPAIN, UNITED STATES OF AMERICA, CAMEROON, KENYA, BENIN, COLOMBIA, n.k.

Sijaona popote palipoandikwa kuwa tende ni kwa ajili ya Waislamu!

Watu wanaovumisha kuwa tende ni chakula cha Waislamu wana nia gani? Wanataka kuwakosesha wasio Waislamu virutibisho vinavyopatikana kwenye tende?
Sasa wao wenyewe huwa wanasema chao so tumewaachia
 
Hata mimi nashangaa kwani hata kahaba maarufu wa kwenye Biblia ni "Tamari" ambalo tafsiri yake ni tende.

Tena ni kahaba aliyehusishwa, ndani ya biblia, kuwa ni katika chanzo zhanzo cha uzazi wa Yesu.
Sasa hii inahusiana nini na tende alafu huyo tamari yuko kitabu gani embu tupe rejea
 
Nje ya mada kidogo, Kondoo pia ni mnyama wa waislamu? Kuna jamaa yangu kanambia hana soko kwa sababu za kiimani, kuna ukweli wowote??

Mimi ninapenda niwafuge, ila nilikatishwa tamaa. Nikaachana nao. Hapa Kyela kuwaona ni nadra sana.
 
Hata mimi nashangaa kwani hata kahaba maarufu wa kwenye Biblia ni "Tamari" ambalo tafsiri yake ni tende.

Tena ni kahaba aliyehusishwa, ndani ya biblia, kuwa ni katika chanzo zhanzo cha uzazi wa Yesu.
Ni kweli kuwa tafsiri ya Tamari ni Tende, lakini Tamari wa kwenye Biblia hakuwa kahaba.

Tamari uliyemtaja ni anayeelezewa kwenye Mwanzo 38:6-30.

Tamari alikuwa mamaye Peresi, ambaye katika uzao wake ndipo Yesu alikuja kuzaliwa.
 
Nje ya mada kidogo, Kondoo pia ni mnyama wa waislamu? Kuna jamaa yangu kanambia hana soko kwa sababu za kiimani, kuna ukweli wowote??

Mimi ninapenda niwafuge, ila nilikatishwa tamaa. Nikaachana nao. Hapa Kyela kuwaona ni nadra sana.
Kivipi mkuu? Kwamba Waislamu wanitimia au hawaitumii?

Nafikiri, nyama ya kondoo na mbuzi hazitofautiani sana kwa ladha, ingawa watu wengi wanapendekea ya mbuzi.

Kuna baadhi ya watu hawapendi nyama ya kondoo, wanadai huwasababishia majipu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom