Kwanini Tanzania tulikuwa upande wa Biafra (Nigeria)?

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Kwa utambulisho Biafra ni jina la eneo ambalo lilitaka kujitenga na nchi ya Nigeria, ambapo kwenye miaka ya 60' lilianzisha (Biafra) jaribio kubwa lililopelekea vita kubwa kutokea kati yake (Biafra) na nchi ya Nigeria ambapo mwishowe nchi ya Nigeria ilifanikiwa kuishinda Jamhuri ya Biafra na kuiunganisha tena na nchi ya Nigeria!

Lakini kilichonifanya niandike Mada hii ni ushiriki wetu kwenye ile vita ambapo sisi kama nchi tulichukuwa upande wa Biafra na nchi yetu ilikuwa ni moja kati ya nchi chache zilizoitambua Jamhuri ya Biafra kama Dola kamili, sasa ni kwa nini? Kuna anayefahamu sababu za nchi yetu kuitambua Jamhuri ya Biafra au kuwa upande wa Biafra na siyo upande wa Nigeria?
Kwa maana nifahamuvyo ni kwamba sisi chini ya Mlm.Nyerere sisi tulikuwa ndiyo wapiga debe wa Muungano wa Afrika (Pan -Africanism) sasa iweje tuwe upande wa watu wanaotaka kujitenga (Biafra) na siyo upande wa wanaotaka kuungana (Nchi ya Nigeria)?
 
Sera ya Tanzania ya mambo ya nje enzi za Mwl. iko wazi. Nikuulize ni kwanini Tanzania ya Nyerere ilikuwa upande wa Palestina dhidi ya Israel? Sababu ni ile ile iliyoifanya Tz ya Mwl kuwa pamoja na ZANU-PF Vs Ian Smith; ANC Vs Makaburu; n.k. kwamba "tutakuwa upande wa wanaoonewa".
 
Nadhani pia tuliunga mkono POLISARIO..

kambarage alikuwa mwanamapinduzi yule
 
Pamoya na kuwa SIELEWI sababu, nnachokumbuka ni kuwa Nigeria ilipata uhuru Oktoba Mosi 1960. Kabla ya kuwa Jamhuri Oktoba Mosi 1963. Viongozi wake wakuu walikuwa: Dr. Nnandi Azikiwe (Kama Gavana Mkuu baadae Raisi na Alhaji Sir Abubakari Tafawa Balewa, kama Waziri Mkuu (Mtendaji Mkuu wa serikali ila baada ay kuwa Jamhuri, akawa chini ya Raisi, hivyo akawa na madaraka kidogo).....
 
Kwa utambulisho Biafra ni jina la eneo ambalo lilitaka kujitenga na nchi ya Nigeria, ambapo kwenye miaka ya 60' lilianzisha (Biafra) jaribio kubwa lililopelekea vita kubwa kutokea kati yake (Biafra) na nchi ya Nigeria ambapo mwishowe nchi ya Nigeria ilifanikiwa kuishinda Jamhuri ya Biafra na kuiunganisha tena na nchi ya Nigeria!

Lakini kilichonifanya niandike Mada hii ni ushiriki wetu kwenye ile vita ambapo sisi kama nchi tulichukuwa upande wa Biafra na nchi yetu ilikuwa ni moja kati ya nchi chache zilizoitambua Jamhuri ya Biafra kama Dola kamili, sasa ni kwa nini? Kuna anayefahamu sababu za nchi yetu kuitambua Jamhuri ya Biafra au kuwa upande wa Biafra na siyo upande wa Nigeria?

Nadhani kuna mada kama hii humu, nadhani ilikuwa na jina la Zitto kama mwanzilishi wa mada, hebu ipekue kwani ilijadiliwa kwa kirefu sana
 
Kwa utambulisho Biafra ni jina la eneo ambalo lilitaka kujitenga na nchi ya Nigeria, ambapo kwenye miaka ya 60' lilianzisha (Biafra) jaribio kubwa lililopelekea vita kubwa kutokea kati yake (Biafra) na nchi ya Nigeria ambapo mwishowe nchi ya Nigeria ilifanikiwa kuishinda Jamhuri ya Biafra na kuiunganisha tena na nchi ya Nigeria!

Lakini kilichonifanya niandike Mada hii ni ushiriki wetu kwenye ile vita ambapo sisi kama nchi tulichukuwa upande wa Biafra na nchi yetu ilikuwa ni moja kati ya nchi chache zilizoitambua Jamhuri ya Biafra kama Dola kamili, sasa ni kwa nini? Kuna anayefahamu sababu za nchi yetu kuitambua Jamhuri ya Biafra au kuwa upande wa Biafra na siyo upande wa Nigeria?

Nakumbuka miaka ya 70 nikiwa mdogo sana nikiwa sekondari vidato vya chini kabisa ila kuna mwalimu mmoja kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam aliandika thesis yake on that...na alinipa nikasoma sitaki kumtaja kwani anaweza akafahamika... Tuliitambua Biafra kwa kuwa Mwalimu (Nyerere) alikuwa na sera ya kuwatetea wanyonge...picha iliyojengwa ni kuwa Waigbo (tukiwaita Waibo) wa East Nigeria walikuwa wanaonewa na Wahausa na Wafulani na kutengwa kwa kuwa ni wasomi...ndivyo tulivyokuwa tunaelezwa...Ivory Coast pia iliitambua Biafra na nchi nyingine moja ya Afrika, nimeisahau na labda ni Guinea ya Sekou Toure...Basi wakati huo tukiwa wadogo na tuko vidato vya chini kabisa Radio Tanzania ilikuwa inatangaza kwenye taarifa ya habari habari nyingi za Biafra na yule kiongozi wao Colonel Odumegwu Ojukwu...Tulikuwa tunaelezwa kuwa Waibo walikuwa wanauawa sana kwa kuonewa...Habari ile nilikuwas naifuatilia sana na miji mingi mikubwa ya Biafra nilikuwa naifahamu,...Owerri, Onitsha, Port Harcourt na kadhalika...Nigeria ya wakati huo yaani Federal Government au serikali ya shirikisho ilikuwa inaongozwa na General Yakubu Gowon...Vita vile vilikuwa ni vibaya mno, tulikuwa tunaonyeshwa picha za Waibo wanaokufa kwa njaa huko maporini wanakimbia vita wakiwa wamekondeana huwezi kuamini kuwa ni binadamu na hasa watoto...yaani nakumbuka tulikuwa tunatokwa na machozi...picha zenyewe hazikuwa za rangi zilikuwa black and white...lakini ziikuwa zinatuingia sana...kitendo kile cha kuitambua Biafra kilituweka katika wakati mgumu na Nigeria...aliyekuja kurejesha uhusiano kidogo nakumbuka alikuwa ni General Obasanjo aliyetembelea Tanzania nadhani mwaka 1977 hivi...otherwise hata wakati wa vita kati yetu Tanzania na Uganda, nadhani Nigeria walimuunga mkono Amin kwasababu ya chuki dhidi yetu kwa suala la Biafra...Nigeria ilichukia sana tulipoitambua Biafra kwa kuwa wakati wa maasi ya Jeshi letu miaka ya 1960 ni jeshi la Nigeria lililokuja kuweka amani baada ya Waingereza waliozima uasi kuambiwa waondoke...
 
Mbona mwaka wa 1960 Tanzania ilikuwa sio nchi/taifa?

Bali ilikuwa ni koloni la mwingereza / Mjerumani
Vita Kati ya Nigeria na jimbo la Biafra vilianza mnamo 6 July 1967 na kuisha 15 January 1970. Huku Nigeria ikishinda na kudhibiti jimbo hilo. Biafra ilikuwa ikiungwa mkono na Ufaransa, Tanzania, Ureno, Afrika kusini, Ivory Cost, Gabon, Zambia, Uhispania
 
Vita Kati ya Nigeria na jimbo la Biafra vilianza mnamo 6 July 1967 na kuisha 15 January 1970. Huku Nigeria ikishinda na kudhibiti jimbo hilo. Biafra ilikuwa ikiungwa mkono na Ufaransa, Tanzania, Ureno, Afrika kusini, Ivory Cost, Gabon, Zambia, Uhispania
.........Naam! Yaani kwa hili la Biafra, Tanzania tukawa "upande mmoja" na "Maadui zetu" Makaburu na Wareno (ambao mpaka wakati huo walikuwa wanazikalia kwa mabavu Msumbiji, Angola nk). Kwa nchi zingine za Kiafrika, Maraisi wao walikuwa: Zambia Kenneth Kaunda, Ivory Coast Felix H. Boigy na Gabon Leon M'ba. (Sina shaka kumbukumbu yangu imekaa vema).
 
.........Naam! Yaani kwa hili la Biafra, Tanzania tukawa "upande mmoja" na "Maadui zetu" Makaburu na Wareno (ambao mpaka wakati huo walikuwa wanazikalia kwa mabavu Msumbiji, Angola nk). Kwa nchi zingine za Kiafrika, Maraisi wao walikuwa: Zambia Kenneth Kaunda, Ivory Coast Felix H. Boigy na Gabon Leon M'ba. (Sina shaka kumbukumbu yangu imekaa vema).
.........Naam! Yaani kwa hili la Biafra, Tanzania tukawa "upande mmoja" na "Maadui zetu" Makaburu na Wareno (ambao mpaka wakati huo walikuwa wanazikalia kwa mabavu Msumbiji, Angola nk). Kwa nchi zingine za Kiafrika, Maraisi wao walikuwa: Zambia Kenneth Kaunda, Ivory Coast Felix H. Boigy na Gabon Leon M'ba. (Sina shaka kumbukumbu yangu imekaa vema).
Kawaida mkuu, maana mwl.alishawahi kusema kwamba "whites in southern of Africa are better than those in northern" ,ijapokuwa walikuwa makaburu na waingereza na wareno maharamia, Lon akaona kwamba walikuwa bora kuliko waarabu wa kaskazini.
 
Waigbo walikua wanaonewa sana na walikufa wengi sana lilikua jimbo la biafra kutaka kujitenga, nimepata kuisoma historia hii, ngoja nitakubushia tena.
 
Kwa utambulisho Biafra ni jina la eneo ambalo lilitaka kujitenga na nchi ya Nigeria, ambapo kwenye miaka ya 60' lilianzisha (Biafra) jaribio kubwa lililopelekea vita kubwa kutokea kati yake (Biafra) na nchi ya Nigeria ambapo mwishowe nchi ya Nigeria ilifanikiwa kuishinda Jamhuri ya Biafra na kuiunganisha tena na nchi ya Nigeria!

Lakini kilichonifanya niandike Mada hii ni ushiriki wetu kwenye ile vita ambapo sisi kama nchi tulichukuwa upande wa Biafra na nchi yetu ilikuwa ni moja kati ya nchi chache zilizoitambua Jamhuri ya Biafra kama Dola kamili, sasa ni kwa nini? Kuna anayefahamu sababu za nchi yetu kuitambua Jamhuri ya Biafra au kuwa upande wa Biafra na siyo upande wa Nigeria?
Kwa maana nifahamuvyo ni kwamba sisi chini ya Mlm.Nyerere sisi tulikuwa ndiyo wapiga debe wa Muungano wa Afrika (Pan -Africanism) sasa iweje tuwe upande wa watu wanaotaka kujitenga (Biafra) na siyo upande wa wanaotaka kuungana (Nchi ya Nigeria)?
sio kwasababu nigeria walijifanya kumsapoti Kambona?
 
Nakumbuka miaka ya 70 nikiwa mdogo sana nikiwa sekondari vidato vya chini kabisa ila kuna mwalimu mmoja kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam aliandika thesis yake on that...na alinipa nikasoma sitaki kumtaja kwani anaweza akafahamika... Tuliitambua Biafra kwa kuwa Mwalimu (Nyerere) alikuwa na sera ya kuwatetea wanyonge...picha iliyojengwa ni kuwa Waigbo (tukiwaita Waibo) wa East Nigeria walikuwa wanaonewa na Wahausa na Wafulani na kutengwa kwa kuwa ni wasomi...ndivyo tulivyokuwa tunaelezwa...Ivory Coast pia iliitambua Biafra na nchi nyingine moja ya Afrika, nimeisahau na labda ni Guinea ya Sekou Toure...Basi wakati huo tukiwa wadogo na tuko vidato vya chini kabisa Radio Tanzania ilikuwa inatangaza kwenye taarifa ya habari habari nyingi za Biafra na yule kiongozi wao Colonel Odumegwu Ojukwu...Tulikuwa tunaelezwa kuwa Waibo walikuwa wanauawa sana kwa kuonewa...Habari ile nilikuwas naifuatilia sana na miji mingi mikubwa ya Biafra nilikuwa naifahamu,...Owerri, Onitsha, Port Harcourt na kadhalika...Nigeria ya wakati huo yaani Federal Government au serikali ya shirikisho ilikuwa inaongozwa na General Yakubu Gowon...Vita vile vilikuwa ni vibaya mno, tulikuwa tunaonyeshwa picha za Waibo wanaokufa kwa njaa huko maporini wanakimbia vita wakiwa wamekondeana huwezi kuamini kuwa ni binadamu na hasa watoto...yaani nakumbuka tulikuwa tunatokwa na machozi...picha zenyewe hazikuwa za rangi zilikuwa black and white...lakini ziikuwa zinatuingia sana...kitendo kile cha kuitambua Biafra kilituweka katika wakati mgumu na Nigeria...aliyekuja kurejesha uhusiano kidogo nakumbuka alikuwa ni General Obasanjo aliyetembelea Tanzania nadhani mwaka 1977 hivi...otherwise hata wakati wa vita kati yetu Tanzania na Uganda, nadhani Nigeria walimuunga mkono Amin kwasababu ya chuki dhidi yetu kwa suala la Biafra...Nigeria ilichukia sana tulipoitambua Biafra kwa kuwa wakati wa maasi ya Jeshi letu miaka ya 1960 ni jeshi la Nigeria lililokuja kuweka amani baada ya Waingereza waliozima uasi kuambiwa waondoke...
Kumbe watanzania tumezaliwa na DNA za unafki ndani mwetu.
 
Back
Top Bottom