Kwanini taa za kuongoza magari Tabata Baracuda haziwashwi licha ya Barabara kuwa na magari mengi?

Aug 31, 2022
54
99
Kwa takriban mwaka mmoja sasa tangu Barabara ya Tabata kuelekea Vingunguti ikamilike kwenye matengenezo, lakini bado Taa za kuongoza Magari hazitumiki katika eneo la Baracuda hali inayoongeza Foleni nyakati za Asubuhi na Usiku.

Kama hazikuwa na maana kwanini zilijengwa na bila shaka kwa gharama kubwa na kupoteza Fedha za walipa Kodi? na cha ajabu bado Trafiki wanasimama pale kwaajili ya kuongoza Magari wakati Taa zipo na hazifanyi kazi

Hebu mamlaka zitwambie nini kinakwamisha taa hizo kuwashwa ili ziongoze Magari katika njia Panda hiyo inayopitisha Magari ya Chang'ombe, Vingunguti, Segerea na Tabata.
 
Back
Top Bottom