Kwanini sisi Waafrika (Tanzania) ukweli huu tunaukwepa?

Inashangaza unajisifia Internet wkt nusu nzima ya watu wetu hawana chakula, Elimu, Maji safi ya kunywa, afya, I mean naweza kujuza kurasa hapa kuorodhesha matatizo ambayo yalipaswa yawe yamekwisha au kupungua kwa kiasi kikubwa kama tungewekeza muda wetu kufanya yale muhimu na yaliyo ndani ya uwezo wetu!

angalia sasa internet ilivyokua nuksi,

Elimu- kupitia internet unajifunza kwa walimu best, haijalishi unasoma shule ya kata au umesoma feza, kupitia internet unaweza ukajifunza kwa mwalimu best na ukawa na elimu bora kushinda mtu aliesoma shule ya mamilioni.

Afya- Hospitali nzuri kumuona tu daktari na kupewa ushauri unaweza ukaambiwa gharama zake ni mshahara wa mwalimu. ila kupitia internet napata ushauri wa ki Afya toka kwa madaktari nguli duniani, nchi zote kubwa marekani, uingereza, australia wana website za Taifa za afya ambazo zinaelekeza kutibu magonjwa mbali mbali na kutoa ushauri wa ki Afya kwa wananchi wao. Huduma anayopata mmarekani anapata mtanzania hiyo hiyo asante iende kwa internet.

chakula na maji - kupitia hio hio internet unajifunza mbegu bora za kulimia, watu wanaagiza mbegu na vifaa online na kulima kisasa kwa maelekezo ya online hii inasaidia kuongeza productivity na kusaidia kupunguza hio njaa, ukiwa serious unaweza ukalima sawa na mkulima wa marekani. same kwenye maji, kuna tips kibao online za kuyasafisha, jinsi ya kuyachimba kiurahisi etc

nenda mbele rudi nyuma internet itabakoa kuwa muhimu kwenye maendeleo.
 
Tunapenda sana kujilinganisha na wengine, na kutwa kusema kwa nini hatuko kama USA, EU au sijui Uchina na Ujapani, lkn kuna jambo moja huwa hatutaki kulikubali na huwa tunalificha chini ya kapeti kwenye kuliganisha kwetu, na ukiniuliza mimi sisi tuko unfair sana kwetu sisi wenyewe, nalo ni hili nitatoa mfano, Columbia University (USA) kilianzishwa mwaka 1750 vs University of Dar es Salaam (TZ yetu) kilianzishwa mwaka 1970!

Sasa linganisha na hapo ujue USA inaitwa ni New World hivyo sijataka kuongelea old world ya EU, ina maana graduate wa kwanza Colombia alitoka kwenye mwaka 1770 huko graduate wa kwanza TZ labda kwenye miaka 50' kama ukichukulia waliosomea Makerere, Nairobi & Co.

Martin Luther aliandika PhD thesis iliyojulikana kama 95 thesis iliyoibadilisha Dunia mwaka 1517, alipata PhD University huko Ujerumani mwaka 1512, linganisha na sisi!

Hamuoni kwamba mnafanya maisha yenu yawe magumu bila ya sababu kwa kulinganisha visivyolingana? Kama ni demokrasia TZ tumeanza hata kulijua hilo neno miaka ya 80' tena mwishoni wakati USA tangu 1700' huko wanajadiliana demokrasia, hivyo fanyeni lililo muhimu na lililo ndani ya uwezo wenu kwa sasa hayo mambo ya kutaka kuwa kama USA au sijui EU mtachanika msamba, USA ina miaka zaidi ya 300 wakati Tanzania chini ya 60!

Kwanza hata hao Afrika ya Kaskazini tu (Moroko, Aljeria, Tunisia &Co.) wametuzidi hata miaka 50 kwenye kila kitu kama human development, lkn unakuta mtu anasimama anaongelea USA, kuweni realistic acheni kujidanganya hakuna miujiza, ...
Mkuu una matatizo.Uchumi haulinganishwi kwa historia.
Sirilanka,india,Singapor heb soma histry na sasa hivi jiulize wapo wapi kiuchumi.Wachina waliteseka mpaka miaka ya 40s muhimu ni mipango tu na utumiaji mzuri wa rasilimali.Je unajua waarabu walikimbia east afrika kutafuta maisha mazuri na sasa hivi unajua wapo hali gani kiuchumi pamoja na jangwa walilonalo?Na je unajua kua zanzibar TVZ ilikua ni Tv ya kwanza ya Rangi nadhan Africa ama East Africa na sasa hivi wapo wapi kimiundo mbinu?
 
Mkuu una matatizo.Uchumi haulinganishwi kwa historia.
Sirilanka,india,Singapor heb soma histry na sasa hivi jiulize wapo wapi kiuchumi.Wachina waliteseka mpaka miaka ya 40s muhimu ni mipango tu na utumiaji mzuri wa rasilimali.Je unajua waarabu walikimbia east afrika kutafuta maisha mazuri na sasa hivi unajua wapo hali gani kiuchumi pamoja na jangwa walilonalo?Na je unajua kua zanzibar TVZ ilikua ni Tv ya kwanza ya Rangi nadhan Africa ama East Africa na sasa hivi wapo wapi kimiundo mbinu?


Siyo kweli na nimeshaliezea hilo, Singapore ni Wachina, na Wachina wana civilization tayari kwanza ya mwanzo klk hata Wazungu, Sri Lanka sijui chochote cha maana ktk huko!
 
Binafsi nimekuelewa sana mkuu na yeyote mwenye akili kubwa atakupata vyema.Kuna kitu kinaitwa universal laws utake usitake maendeleo ni hatua ambazo ni lazima uzipitie.

Africa tupo nyuma kwa sababu wazungu walituvunjia msingi wa hatua zetu za kimaendeleo.Hakuna maendeleo ya ku Surpass lazima utoke hatua moja kwenda nyingine.

Ulaya Leo wameendelea ila ukiangalia walikotokea enzi wanatumia steam engine lazima utakubali ni ujinga kujilinganisha nao.Unaweza ukamfikia aliye mbele ila utalazimika kukimbia kwa kasi kuliko yeye.
 
Mkuu una matatizo.Uchumi haulinganishwi kwa historia.
Sirilanka,india,Singapor heb soma histry na sasa hivi jiulize wapo wapi kiuchumi.Wachina waliteseka mpaka miaka ya 40s muhimu ni mipango tu na utumiaji mzuri wa rasilimali.Je unajua waarabu walikimbia east afrika kutafuta maisha mazuri na sasa hivi unajua wapo hali gani kiuchumi pamoja na jangwa walilonalo?Na je unajua kua zanzibar TVZ ilikua ni Tv ya kwanza ya Rangi nadhan Africa ama East Africa na sasa hivi wapo wapi kimiundo mbinu?
Mkuu huko umeenda mbali sana, njoo tu hapo kwa South Sudan soon watatupita, tatizo Barbarossa ni mfia chama.
 
Kama miaka 56 bado mnapigana na maadui 3 nadhani ni muda sasa wa kusema kuwa HAO MAADUI WAMESHINDA maana hawana hata silaha hao maadui but now ni 56 years!!! ni mda mrefu sana aiseee.
 
Hii ni gear ya wana ccm kuendelea kupumbaza wananchi ili itawale vizuri. Mbona kuna nchi nyingine tulipata Uhuru sawa na zimepiga hatua kubwa kimaendeleo kuliko Tz?!
 
Hii ni gear ya wana ccm kuendelea kupumbaza wananchi ili itawale vizuri. Mbona kuna nchi nyingine tulipata Uhuru sawa na zimepiga hatua kubwa kimaendeleo kuliko Tz?!


Zitaje hizo nchi halafu tulinganiishe historia zao!
 
Tatizo wengi wetu ndo tulivo hatufatilii historia tunafikiria juu juu tu then we put in action
 
Africa ilikuwepo kabla 1750 enzi za miji ya Kilwa Kivinje. Wazungu na waarabu waliwahi kusafiri baharini kwa shida zao wakaja kutawala Afrika. Lakini pia walikuja na maendeleo. Nchi zilizochelewa kupata uhuru ziliendelezwa zaidi. Kuna miji ya maana Afrika ya kusini kushinda hata baadhi ya miji iliyopo Ulaya na Marekani.

Hata hivi vya kupata uhuru ni mipango ya wakoloni. Baada ya vita kuu ya pili mataifa ya Ulaya yalikuwa na hali mbaya kifedha yakaona umuhimu wa kuachia baadhi ya makoloni.

Kilichoendelea ni kuandaliwa viongozi wa kiafrika watakaokuwa wanachukua maagizo kutoka Ulaya (ukoloni mamboleo)

Makoloni yaliyodumaa kama watoto yameendelea kujali kingereza na kifaransa kingi na yanaendelea kutawaliwa. Ndio hapo Bob Marley aliimba “emancipate yourself from mental slavery” - jikomboe kutoka utumwa wa akili. Hivi vya kuwasifia Singapore na Hongkong ni hili suala la kujikomboa kiakili.

Hatuwezi kupitia kila kitu walichopitia wazungu ndio tuendelee. Itabidi na sisi tukamate watumwa.

Tunatakiwa tuwe kitu kimoja tufanye yanayotufaa kwa maendeleo yetu.
daaahhh hii comment imeshiba inaafyaaa mnooo
 
Kama miaka 56 bado mnapigana na maadui 3 nadhani ni muda sasa wa kusema kuwa HAO MAADUI WAMESHINDA maana hawana hata silaha hao maadui but now ni 56 years!!! ni mda mrefu sana aiseee.
hahaaa...mkuu hawanaoni hata aibu narasilimali zote hizi tulizobalikiwa as taifa....bado anatokea mtu anatuambia tusubiri miaka 300 ijayo....katumwa huyu sio bure
 
Hapana haujanielewa labda, sijasema kwamba sitaki TZ au Afrika iwe na demokrasia, kwani hata sina uwezo huyo, demokrasia siyo swala la kuamua kwamba tunaitaka au hatuitaki bali ni huja tu, hujilazimisha na kujipenyeza wakati wake ukifika, na hailazimishwi, muda ukifika utaona hata TZ mashoga watadai haki ya kuoana, watoto watadai uhuru wa kwenda disko na kuwa girlfriend na haitajalisha kama mzazi anakubali au la, muda ukifika Watanzania watadai hizi tunazoziita haki kama EU, USA na kwingineko, lkn hatuwezi kuchukuwa njia ya mkato!

Ninachokipinga ni kujaribu kulazimisha jambo ambalo kwa sasa muda wake haujafika, hilo halitowezakana, hata ukiangalia kwenye doctrine ya neocons kama George Bush alitaka kupeleka demokrasia Uarabuni lkn matokeo yake ni mabaya kuliko hata kabla ya demokrasia, angalia Libya, Iraki na sasa Syria, hivyo maana yake ni kwamba haya mambo hayalazimishwi kwani muda ukifika hujilazimisha tu!
Yeah, Nimependa ulivyotolea mfano Bush Doctrine.
JF ni kisima cha maarifa, kimejaza watu wenye ujuzi na uelewa mbalimbali wa mambo.
 
Africa ilikuwepo kabla 1750 enzi za miji ya Kilwa Kivinje. Wazungu na waarabu waliwahi kusafiri baharini kwa shida zao wakaja kutawala Afrika. Lakini pia walikuja na maendeleo. Nchi zilizochelewa kupata uhuru ziliendelezwa zaidi. Kuna miji ya maana Afrika ya kusini kushinda hata baadhi ya miji iliyopo Ulaya na Marekani.

Hata hivi vya kupata uhuru ni mipango ya wakoloni. Baada ya vita kuu ya pili mataifa ya Ulaya yalikuwa na hali mbaya kifedha yakaona umuhimu wa kuachia baadhi ya makoloni.

Kilichoendelea ni kuandaliwa viongozi wa kiafrika watakaokuwa wanachukua maagizo kutoka Ulaya (ukoloni mamboleo)

Makoloni yaliyodumaa kama watoto yameendelea kujali kingereza na kifaransa kingi na yanaendelea kutawaliwa. Ndio hapo Bob Marley aliimba “emancipate yourself from mental slavery” - jikomboe kutoka utumwa wa akili. Hivi vya kuwasifia Singapore na Hongkong ni hili suala la kujikomboa kiakili.

Hatuwezi kupitia kila kitu walichopitia wazungu ndio tuendelee. Itabidi na sisi tukamate watumwa.

Tunatakiwa tuwe kitu kimoja tufanye yanayotufaa kwa maendeleo yetu.
Ahsante mkuu kwa comment yenye ujumbe hasa.
 
Kwa hiyo Azam iliyoanzishwa mwaka 2007 isijifananishe kabisa na Yanga iliyoanzishwa 1935?
 
hahaaa...mkuu hawanaoni hata aibu narasilimali zote hizi tulizobalikiwa as taifa....bado anatokea mtu anatuambia tusubiri miaka 300 ijayo....katumwa huyu sio bure


Ni wapi niliposema au nilipomwambia mtu asubiri? Nimesema hali halisi jinsi ilivyo kwanza hata hilo tu la kusema ,,rasilimali zote hizi" inaonyesha jinsi gani nilivyokuwa sahihi, sasa kwa nini hakuna maendeleo pmj na hizo Rasilimali? Na hii siyo TZ tu bali Kusini mwa Sahara kote ukiondoa AK, na kwa nini Aljeria, Libya (zamani) Rasilimali ziliwasaidia? Kwa nini kwetu ishindikane?
 
Kwa hiyo Azam iliyoanzishwa mwaka 2007 isijifananishe kabisa na Yanga iliyoanzishwa 1935?


Ndiyo unaweza kuwa ni mfano mzuri, lkn tofauti ni kwamba Azam atachukuwa Makocha, wachezaji ambao tayari walishapikwa na Yanga au Simba na kuwaleta Azam, lkn kama akianzia chini bila ya kufanya hivyo hawezi kumfikia Yanga, na ndicho nchi kama Australia, New Zealand, Kanada, USA au AK walivyofanya, waliozijenga hizo nchi ni Wazungu waliotoka Ulaya ambao tayari kulikuwa na maendeleo hivyo wakafanya tu skills transfer, hata waliotoa upendeleo maalumu wa masoko kwenye mama kwa mfano wauza manyoya ya kondoo ktk New Zealand walipata special treatment kwenye kuuza huko Ulaya lkn sasa sisi hatuwezi kuchukuwa Wazungu au Wajapani waje wafanye skills transfer kwa maana sisi siyo sehemu yao, hawawezi kukubali na wala siyo sehemu ya policy yao, hivyo ni lazima tujenge wenyewe kuanzia chini!

Wao iliwezekana kwa sababu hizo zilikuwa ni Makoloni ya Old World ina maana Ufaransa, Uingereza na wengineo walikuwa wanatuma watu kuwekeza huko!
 
Ni wapi niliposema au nilipomwambia mtu asubiri? Nimesema hali halisi jinsi ilivyo kwanza hata hilo tu la kusema ,,rasilimali zote hizi" inaonyesha jinsi gani nilivyokuwa sahihi, sasa kwa nini hakuna maendeleo pmj na hizo Rasilimali? Na hii siyo TZ tu bali Kusini mwa Sahara kote ukiondo AK, na kwa nini Aljeria, Libya (zamani) Rasilimali ziliwasaidia? Kwa nini kwetu ishindikane?
kama lengo lako lilikuwa nihili tuko pamoja mkuu....ila kama tunataka ustawi wa kiuchumi kama taifa kiujumla tunapaswa kuwaiga wale walioendelea zaidi nahili linapaswa kujikita zaidi ktk Yale mambo mazuri tu nayatakayoleta tija kwetu...nawasilisha hoja
asante
 
Labda mtoa mada angorodhesha ni hatua zipi tunatakiwa tuzipitie mpaka tufike walikofika walioendelea. Na pia awe muwazi tunawakimbilia wamarekani, wachina, waarabu au Ulaya. Kwa sababu hata nchi zilizoendelea hazikupitia hatua sawa kufikia maendeleo.
 
Ni upuuzi mtakatifu kusema ili tuendelee inatubidi kupitia hatua walizopita walioendelea.

Hii hatua tunayopitia sasa wenzetu hawakuipitia. Wamarekani na waingereza walitegemea misaada ya nje kwenye bajeti zao?

Kwa kila shilingi moja ya msaada na mkopo tunayochukua tunalipa shilingi 2 kwenye riba, fedha chafu (money laundering) na ukwepaji kodi wa makampuni ya nje. Chukulia tu kodi wanayodaiwa Acacia kwa miaka 10, je haizidi misaada ya nchi tuliyopokea kwa miaka kumi?


Ndio maana namkubali sana Magufuli!
 
Back
Top Bottom