Kwanini sisi Waafrika (Tanzania) ukweli huu tunaukwepa?

Ni upuuzi mtakatifu kusema ili tuendelee inatubidi kupitia hatua walizopita walioendelea.

Hii hatua tunayopitia sasa wenzetu hawakuipitia. Wamarekani na waingereza walitegemea misaada ya nje kwenye bajeti zao?

Kwa kila shilingi moja ya msaada na mkopo tunayochukua tunalipa shilingi 2 kwenye riba, fedha chafu (money laundering) na ukwepaji kodi wa makampuni ya nje. Chukulia tu kodi wanayodaiwa Acacia kwa miaka 10, je haizidi misaada ya nchi tuliyopokea kwa miaka kumi?


Ndio maana namkubali sana Magufuli!


Hakuna mahali niliposema kwamba tunahitaji msaada ili tuendelee, na kwanza hiyo misaada iko kwa ajili hiyo kutupumbaza ili tuendelee kuamini hatuwezi kujisimamia bila ya Muzungu, bali nimesema kuna hatua ni lazima tuzipitie kama jamii bila ya hivyo hakuna mahli tutaenda, na kuna kila ushahidi wa hilo unaonekana kila mahali!
 
Binafsi nimekuelewa sana mkuu na yeyote mwenye akili kubwa atakupata vyema.Kuna kitu kinaitwa universal laws utake usitake maendeleo ni hatua ambazo ni lazima uzipitie.

Africa tupo nyuma kwa sababu wazungu walituvunjia msingi wa hatua zetu za kimaendeleo.Hakuna maendeleo ya ku Surpass lazima utoke hatua moja kwenda nyingine.

Ulaya Leo wameendelea ila ukiangalia walikotokea enzi wanatumia steam engine lazima utakubali ni ujinga kujilinganisha nao.Unaweza ukamfikia aliye mbele ila utalazimika kukimbia kwa kasi kuliko yeye.
Kwa hiyo lazima na sisi tuanze na steam engine kwanza ili tusiwe tumeruka?
 
Kwa hiyo lazima na sisi tuanze na steam engine kwanza ili tusiwe tumeruka?


Hapana, tuanze na kwanza hata tu kujenga Taifa, sasa hivi karne ya 21 bado hata hatujui kama Wamasai ni wamasai kwanza au Watanzania, ni Wachaga kwanza au Watanzania, sasa kama hata hatujui tofauti ya Kabila na Taifa patriotism itatoka wapi? Bila ya partiotism hakuna maendeleo!
 
Hakuna mahali niliposema kwamba tunahitaji msaada ili tuendelee, na kwanza hiyo misaada iko kwa ajili hiyo kutupumbaza ili tuendelee kuamini hatuwezi kujisimamia bila ya Muzungu, bali nimesema kuna hatua ni lazima tuzipitie kama jamii bila ya hivyo hakuna mahli tutaenda, na kuna kila ushahidi wa hilo unaonekana kila mahali!

Sasa wakati unapitia hizo hatua mzungu utamuweka wapi na anadai madeni yake, na bado unakopa. Je hao walioendelea walipitia hatua hii ya kudaiwa?
 
Kwa hiyo lazima na sisi tuanze na steam engine kwanza ili tusiwe tumeruka?
Huo ni mfano tu ila lengo lilikuwa ni lazima tutengeneze msingi wa uhakika ili kitu tunachokitamani kitokee na hiyo inachukua miaka mingi sana.

Binafsi hata mimi huwa naona si vizuri kujilinganisha na walioendelea katika mambo mengi(sio yote).Ipo siku tunaweza kuja kuwafikia na kuwapita ikiwezekana ila tutatakiwa kukimbia kwa kasi kuliko wao.
 
Huo ni mfano tu ila lengo lilikuwa ni lazima tutengeneze msingi wa uhakika ili kitu tunachokitamani kitokee na hiyo inachukua miaka mingi sana.

Binafsi hata mimi huwa naona si vizuri kujilinganisha na walioendelea katika mambo mengi(sio yote).Ipo siku tunaweza kuja kuwafikia na kuwapita ikiwezekana ila tutatakiwa kukimbia kwa kasi kuliko wao.
"Wakati wao wanatembea sisi tunataka tukimbie" kwa sababu wao walishakimbia, sisi tunapaswa kukimbia kwa sababu tumesharahisishiwa mambo mengi! Asilimia kubwa ya Tools tunazozihitaji zipo tayari! Hatuhitaji miaka 40 ya kuvumbua umeme tena! Kwa nini tusikimbie? Hatuhitaji kumsubiri mvumbuzi wa steam engine azaliwe! Formula zipo all over the shelves! Nini cha kutusubirisha? Sioni
 
Ebu jiulize wakati tunaanza kutumia smartphone wenzetu walikua wapi na sisi tulikua wapi.?kwa mantiki yako inabidi tusubiri miaka zaidi ya 200 ijayo ndipo tuanze kutumia smartphones na haiwezekani
huyo anamung'unya tu maneno lengo lake tuwasifie waarabu anashindwa tu tuanzie wapi
 
Ni kweli kwamba nchi zao zilianza zamani sana na kwa namna yoyote hakuwezi kuwa na fair comparison kati yetu na wao kwa mambo mengi. lakini hatuwezi kukwepa ukweli kwamba maendeleo tuliyonayo sasa hivi si yale tuliyotakiwa kuwanayo kama tungekuwa tuna institution na uongozi unaopenda maendeleo ya wananchi. tatizo letu kubwa ni ubinafsi, anayepewa uongozi hajali maslahi mapana ya taifa mwisho wa siku rushwa na ufisadi wa mali ya uma vinasababisha tunashindwa kuendelea. chukulia mfano mdogo tu serikali inatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule say vyumba 10 vya madarasa lakini utakuta pesa hiyo inaliwa kuanzia juu mpaka chini kwa mkuu wa shule matokeo ya vinajengwa vyumba vitano vibovu. sasa je kama kwa mwaka ulitakiwa ujenge vyumba kumi ukaishia vitano si maana yake maendeleo ambayo ungefanya mwaka mmoja unafanya miwili na zaidi.

huo ni mfano mdogo tu lakini madudu yapo kila sector, afya madini fedha na uchumi kila kona mambo hayo yapo. hatahivyo sisi tunaweza kuendelea at a faster rate kuliko wao walivyoendelea namaanisha kwamba inatuchukua muda mchache kupata maendeleo waliyoyapata kwa miaka mingi kwa sababu ya teknolojia iliyopo sasa hivi. mfano mdogo tu ni china ambayo iliweza kuondoa takliban watu million 800 from poverty for just less 40 years sasa hivi china urban poverty ni almost zero. hivyo muda wa miaka 50 nchi inaweza kufanya remarkable economic changes kama itaamua kweli kweli.

binafsi nadhani ili tuwekuendelea lazima tuzingatie mambo yafuatayo kama taifa
1. institution, iwepo mifumo ya active kiserikali na kisheria inayo wawajibisha viongozi ama wafanyakazi waliopewa dhamana ya kusimamia rasilimali na miradi ya maendeleo ya taifa wanaoshindwa kutimiza majukumu yao ama wanaofanya ubadhilifu wa mali ya uma. hili linawezekana kwa kuwa na katiba SIO MPYA tu bali pia imara inayoendana na mabadiliko ya nyakati tulizonazo.
2. Nchi iwe na national vision, ambalo kiongozi yoyote aneingia madarakani ana work along it. sio kila mwanasiasa anakuja na ya kwake anayoyataka leo kilimo kwanza kesho viwanda. tuwe na lengo kwamba in 10yrs, 20yrs, 50yrs nk tunataka kuachive nini kama taifa.
3.nchi iwekeze sana katika elimu science na teknolojia. siku huwezi kuendelea katika ulimwengu wa sasa kama hujawekeza kwenye teknolojia. utabakia mkiani tu ambapo utanunua kila kitu kutoka nje. tuwe na wataalam wetu wenye uwezo katika sector ya afya uandisi biashara uchumi nk
 
Tanzania tuwekeze kwenye kilimo tu. Walete makitu kama haya mengi.
c468a33506375eb15e008e6ca19579df.jpg

Tuboreshe ufagaji uwe wa kisasa.
db4855dd59b0e965fe007a7c7d3a8e7b.jpg


Watu washibe. Watu wenye njaa hawawezi kutengeneza ndege. Wenzetu walipiga vita njaa kwa kutumia watumwa. Sisi tutumie mashine. Lilimwe shamba la mahindi Ruvu mpaka Moro halafu tuone kama kuna mnafiki atakaepiga mbiu Tanzania kuna njaa. Hao wachina mnaowasifia mmeona mashamba yao?
 
Ni kweli kwamba nchi zao zilianza zamani sana na kwa namna yoyote hakuwezi kuwa na fair comparison kati yetu na wao kwa mambo mengi. lakini hatuwezi kukwepa ukweli kwamba maendeleo tuliyonayo sasa hivi si yale tuliyotakiwa kuwanayo kama tungekuwa tuna institution na uongozi unaopenda maendeleo ya wananchi. tatizo letu kubwa ni ubinafsi, anayepewa uongozi hajali maslahi mapana ya taifa mwisho wa siku rushwa na ufisadi wa mali ya uma vinasababisha tunashindwa kuendelea. chukulia mfano mdogo tu serikali inatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule say vyumba 10 vya madarasa lakini utakuta pesa hiyo inaliwa kuanzia juu mpaka chini kwa mkuu wa shule matokeo ya vinajengwa vyumba vitano vibovu. sasa je kama kwa mwaka ulitakiwa ujenge vyumba kumi ukaishia vitano si maana yake maendeleo ambayo ungefanya mwaka mmoja unafanya miwili na zaidi.

huo ni mfano mdogo tu lakini madudu yapo kila sector, afya madini fedha na uchumi kila kona mambo hayo yapo. hatahivyo sisi tunaweza kuendelea at a faster rate kuliko wao walivyoendelea namaanisha kwamba inatuchukua muda mchache kupata maendeleo waliyoyapata kwa miaka mingi kwa sababu ya teknolojia iliyopo sasa hivi. mfano mdogo tu ni china ambayo iliweza kuondoa takliban watu million 800 from poverty for just less 40 years sasa hivi china urban poverty ni almost zero. hivyo muda wa miaka 50 nchi inaweza kufanya remarkable economic changes kama itaamua kweli kweli.

binafsi nadhani ili tuwekuendelea lazima tuzingatie mambo yafuatayo kama taifa
1. institution, iwepo mifumo ya active kiserikali na kisheria inayo wawajibisha viongozi ama wafanyakazi waliopewa dhamana ya kusimamia rasilimali na miradi ya maendeleo ya taifa wanaoshindwa kutimiza majukumu yao ama wanaofanya ubadhilifu wa mali ya uma. hili linawezekana kwa kuwa na katiba SIO MPYA tu bali pia imara inayoendana na mabadiliko ya nyakati tulizonazo.
2. Nchi iwe na national vision, ambalo kiongozi yoyote aneingia madarakani ana work along it. sio kila mwanasiasa anakuja na ya kwake anayoyataka leo kilimo kwanza kesho viwanda. tuwe na lengo kwamba in 10yrs, 20yrs, 50yrs nk tunataka kuachive nini kama taifa.
3.nchi iwekeze sana katika elimu science na teknolojia. siku huwezi kuendelea katika ulimwengu wa sasa kama hujawekeza kwenye teknolojia. utabakia mkiani tu ambapo utanunua kila kitu kutoka nje. tuwe na wataalam wetu wenye uwezo katika sector ya afya uandisi biashara uchumi nk


Hivyo vitu vyote ulivyovitaja haviji ndani ya miaka 60, nchi zote ambazo zimeweza kujenga hiyo mifumo zilianza zamani sana, isitoshe unapolaumu viongozi wetu unafanya kosa lile la kusahau kwamba Viongozi wetu hawajatoka Sayari nyingine bali ni mimi na wewe, wamekulia na kulelewa mazingira yetu hivyo wanachokifanya Mtanzania yoyote yule aliyezaliwa na kulelewa hapa pia angefanya!

Usione nchi zimesimama ukafikiri imetokea tu, hapana, wametoka mbali, tena sana!
 
Tanzania tuwekeze kwenye kilimo tu. Walete makitu kama haya mengi.
c468a33506375eb15e008e6ca19579df.jpg

Tuboreshe ufagaji uwe wa kisasa.
db4855dd59b0e965fe007a7c7d3a8e7b.jpg


Watu washibe. Watu wenye njaa hawawezi kutengeneza ndege. Wenzetu walipiga vita njaa kwa kutumia watumwa. Sisi tutumie mashine. Lilimwe shamba la mahindi Ruvu mpaka Moro halafu tuone kama kuna mnafiki atakaepiga mbiu Tanzania kuna njaa. Hao wachina mnaowasifia mmeona mashamba yao?


Kuweka Picha kila mtu anaweza, ingekuwa rahisi hivyo basi kusingekuwa na nchi masikini Dunia hii!
Ni sawa na kupiga Picha ya mjengo Masaki na kusema kila Mtanzania ajenge mjengo kama Huu!
 
Hivyo vitu vyote ulivyovitaja haviji ndani ya miaka 60, nchi zote ambazo zimeweza kujenga hiyo mifumo zilianza zamani sana, isitoshe unapolaumu viongozi wetu unafanya kosa lile la kusahau kwamba Viongozi wetu hawajatoka Sayari nyingine bali ni mimi na wewe, wamekulia na kulelewa mazingira yetu hivyo wanachokifanya Mtanzania yoyote yule aliyezaliwa na kulelewa hapa pia angefanya!

Usione nchi zimesimama ukafikiri imetokea tu, hapana, wametoka mbali, tena sana!

Waarabu wa Dubai hata shule hawakusoma wametoka mbali ya wapi?
 
Kuweka Picha kila mtu anaweza, ingekuwa rahisi hivyo basi kusingekuwa na nchi masikini Dunia hii!
Ni sawa na kupiga Picha ya mjengo Masaki na kusema kila Mtanzania ajenge mjengo kama Huu!

Kwani hela ya kununua hayo makitu hakuna. Nenda Japan utayakuta yamedoda Kibaha mpaka Chalinze yanauzwa kwa mnada. Lakini wabongo wanaenda kununua corolla na RAV 4 tu za kuhonga mabibi. Na serikali inanunua na magari ya wabunge. Sijawahi kuona nchi yenye watu wana akili mavi kama Tanzania.
 
Hivyo vitu vyote ulivyovitaja haviji ndani ya miaka 60, nchi zote ambazo zimeweza kujenga hiyo mifumo zilianza zamani sana, isitoshe unapolaumu viongozi wetu unafanya kosa lile la kusahau kwamba Viongozi wetu hawajatoka Sayari nyingine bali ni mimi na wewe, wamekulia na kulelewa mazingira yetu hivyo wanachokifanya Mtanzania yoyote yule aliyezaliwa na kulelewa hapa pia angefanya!

Usione nchi zimesimama ukafikiri imetokea tu, hapana, wametoka mbali, tena sana!
kujenga mfumo imara wa serikali haiitaji miaka 50 wala kuwa na general vision ya taifa haiitaji miaka mingi ni kitendo tu cha viongozi kuwa na nia thabiti ya kuleta maendeleo wananchi ni just kuwamobilize tu.
 
Waarabu wa Dubai hata shule hawakusoma wametoka mbali ya wapi?


Soma Historia ya Waarabu, wana Civilization tayari, Islamic Civilization ni ya Waarabu, unajua Uislamu ni Dini ya Pili kwa ukubwa Duniani? Waliwezaje kuisambaza na kuendelea kuisambaza kuvutia watu wengi namna hiyo?

Wana maandishi yao Kiarabu, sisi hatuna tuliyonayo siyo yetu, wana Kalenda yao, sisi hatuna, waneshawahi kujenga Civilized cities kama Damascus, sisi hatuna Mji wowote tuliowahi kujenga ambao haukujengwa na Mzungu, hivyo wametuzidi sana tu na ndiyo maana wameweza kutumia rasilimali walizonazo na kuwasaidia sisi tumeshindwa, sasa kwa nini? Jibu ni civilization, hatujajenga bado civilization, tunadandia tu na kuchukuwa wengine!
 
kujenga mfumo imara wa serikali haiitaji miaka 50 wala kuwa na general vision ya taifa haiitaji miaka mingi ni kitendo tu cha viongozi kuwa na nia thabiti ya kuleta maendeleo wananchi ni just kuwamobilize tu.


Tena miaka 50 ni michache sana, hakuna jamii iliyofanikiwa kwa muda mfupi hivyo kama ipo itaje!
 
Soma Historia ya Waarabu, wana Civilization tayari, Islamic Civilization ni ya Waarabu, unajua Uislamu ni Dini ya Pili kwa ukubwa Duniani? Waliwezaje kuisambaza na kuendelea kuisambaza kuvutia watu wengi namna hiyo?

Wana maandishi yao Kiarabu, sisi hatuna tuliyonayo siyo yetu, wana Kalenda yao, sisi hatuna, waneshawahi kujenga Civilized cities kama Damascus, sisi hatuna Mji wowote tuliowahi kujenga ambao haukujengwa na Mzungu, hivyo wametuzidi sana tu na ndiyo maana wameweza kutumia rasilimali walizonazo na kuwasaidia sisi tumeshindwa, sasa kwa nini? Jibu ni civilization, hatujajenga bado civilization, tunadandia tu na kuchukuwa wengine!

Kondoa kuna michoro na maandishi yetu kabla ya kuvamiwa na wageni. Unafikiri hawakuwa na miji?
 
Haujanielewa labda, hoja yako ingekuwa sawa kama leo hii sisi tungekuwa na uwezo ya kuunda smart phone, lkn tunanunua, uwezo wa kuunda hatuna, kujenga micro electronic industry Tanzania na kuweza kuunda micro chips kwa elimu hii yetu ni bado sana, siwezi kusema haiwezekani lkn bado safari ni ndefu sana!
Unajua watu tunashindwa kumuelewa mleta mada, na nina hakika kuna watu wanaweza amini kwamba baadhi ya vifaaa hutengenezwa bongo, ndege sawa wao wanamiliki na sisi tunamiliki, ila je imeundwa hapa bongo ????? Wao wanatengeneza mashine za kutengenezea nguo na sisi tuna zinunua, je ???? Zimetengenezwa hapa bongo????
Watu mwandishi hawajamuelewa hapa ndipo kipimo cha elimu yetu yakufikilia inavyopata shida
 
Back
Top Bottom