Mheshimiwa J.ndugai aliona kama LISSU ni mkosaji kwa kuomba miongozo mara nyingi na kuamua kumtimua bungeni.
SWALI:
1.kama wabunge wa ccm ndiyo wanaoongoza kisinzia bungeni,miongozo hiyo wangeomba saa ngapi wakati wanasinzia?
2.kama wabunge wa ccm ndiyo wanaongoza kwa utoro bungeni,muda wakuomba miongozo wataupata wapi?
3.kama wabunge wa ccm walichojaliwa ni matusi,je watakumbuka miongozo ya bunge?
4.kama wabunge wa ccm wanaongoza kwa kukaa nje ya majimbo yao,isipokuwa Pr.Majimarefu,wataomba miongozo kwa hoja gani wakati hoja walizo kwenda nazo bungeni hazikutokana na wapigakura wao?
5.kama wabunge wa ccm wanaongoza kwa rushwa km vile kina badwell,wataomba miongozo wamhhoji nani na nini?
6.kama wabunge wa ccm ni vinara kwa kututumia muda wa bunge kupongezana na kwasifia wake zao hadi wajukuu wao,watapata wapi muda wakutafakari ya kuombea miongozo?
7.kama wabunge wa ccm ndiyo wanaongoza kwa kusifia kila hoja ,wataomba miongozo ya nini?
8.kama wabunge wa ccm wanaona kwamba kila mbunge wao kama vile Deo filikunjombe anaikosoa serikali anaambiwa huyu atakuwa ni wa chadema,wataomba miongozo ili wakosoe nini?
9.kama wabunge wa ccm wanaona kazi yao pale ni kujipendekeza kwa rais hata kama maswala hayo yanataka kuboresha maslahi ya taifa,miongozo itatoka wapi?
10.kama spika na naibu spika wa ccm hayajui matusi yatolewayo kwa kiingereza na kuona hatua haitakiwi kuchukuliwa kwa mbunge aliyetukana kwa kiingereza,miongozo itaombwa kwa kazi gani?
11.kama wabunge wa ccm wanaona kazi iliyowapeleka bungeni ni kuwadhiti chadema tu ,wataomba miongozo ya nini?