Kwanini Serekali inakopa kama inaweza ku-print noti mpya

Mleta Mada, alikusududia lipatikane jibu mfano wa Hili. Na ndicho wasomi wetu wengi wanashindwa kuufikisha wanaelewa katika sauti ya kueleweka.

Kuchapisha pesa noti kuhudumia mkopo au baadhi ya shughuli kuna sababisha matatizo mengi kuliko suluhisho.

Ujerumani ikijiita Weimar republic waliprint noti nyingi mwaka 1922 kilichotokea ni mfumuko wa bei uliopitiliza(hyper inflation)

Ujerumani ilikuwa na deni kubwa baada ya kushindwa vita vya kwanza vya dunia, njia waliyotumia ni hii ya kuchapisha noti nyingi.

Pesa ikawa nyingi kwenye mzunguko kuliko kile ambacho nchi inaweza kuzalisha.

Mfumuko wa bei ukaibuka na kusababisha thamani ya tharafu yao kushuka thamani, na matokeo yake kushindwa kulipa deni kabisa.

Ukiangalia huo mfano unaweza kuona madhara ya kuchapisha noti nyingi.

Kikawaida kiwango cha noti kinachotolewa kinatakiwa kiendane na level ya uzalishaji wa bidhaa na huduma.

Ili kuelewa zaidi tuchukulie mfano wa muonyesha banda la video.

Uwezo wa banda la video ni kuingiza watu hamsini.

Kwa hiyo mwenye banda la video(mtengeneza noti) atatengeneza tiketi(noti) 50 kila tiketi iwe sh 2.

Kama mwenye banda la video akawa ana uhitaji sh 108, akaamua azalishe 54 kinachofuata hizi tiketi zitapanda bei kwa sababu siti ziko hamsini tu.

Sasa kama kuna mtu mwingine naye anaonyesha video wateja wanaweza kuhamia huko kwa sababu bei ni ya chini. Huyu mwingine atashindwa hata kuipata hiyo 108.

Kwa hiyo hapo njia nzuri ni kuwakopa wale baadhi walionunua tiketi 50, kwa sababu kuna wengine hawatoangalia movie wakati huo kwa hiyo utazikopa zile tiketi mfano 4 (mfano saving au kuuza dhamana za serikali,bond nk) na kuziuza kwa wengine ama kuzifanyia shughuri nyingine.

Ndio maana serikali inapokuwa na uhitaji wa kiasi cha pesa cha ziada na kodi ikawa haitoshi, hukopa kwa kwa kuuza treasury bill, treasury bonds nk au kukopa nje ya nchi kuliko kuchapisha noti mpya kwa sababu uchapishaji wa noti mpya haiongezi uzalishaji bali inaongeza pesa kwenye mzunguko.

Nadhani wenye uelewa zaidi watakufafanulia.

Baadhi ya link unazoweza pitia.
National debt of the United States - Wikipedia
Why do governments borrow money instead of printing it? - Quora
Hyperinflation in the Weimar Republic - Wikipedia
The problem with printing money - Economics Help

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SWALI LA KIJINGA

Je pesa inakuwaje nyingi mtaani kama mshahara unaolipwa ni uleule, au hata ukifanya kibarua pesa unayolipwa ni ileile,?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mishahara itapandishwa mkuu, posho zitakuwa nyingi, masharti ya kukopa bank yatapunguzwa, kutakuwa na unafuu kwenye ulipaji kodi n.k
Angalia sasa hivi hela ilivyo ngumu mtaani, serikali imefanya kinyume cha hayo
 
Mbona swali lilikuwa wazi sana, je inaprint hela kama mbadala wa kukopa pesa au huwa haiprint? Jaribu kujikita kwenye swali
"Kwanini Serekali inakopa kama inaweza ku-print noti mpya"
Swali lipo hivi mkuu, yaani kwa mfano kama huu. Sasa hivi serikali inajenga reli ya SGR kwa mkopo, ni kwanini basi tusiprint note mpya ili tujenge SGR kwa hela zetu hizo mpya badala yake tumeenda kukopa?
Kiuchumi kukopa kuna faida zaidi kuliko kuprint note mpya ila sometimes huwa wanaprint ila kwa taadhari kubwa sana na pia kutegemeana na sera za nchi kwa wakati huo.
So kuprint wanaprint ila lazima kufanywe kwa tahadhari kubwa sana otherwise uchumi utaanguka vibaya sana.
 
Kuna waziri sijui wa zambia au Zimbabwe, aliamka zake akasema watu wanalia maisha magum hamna pesa, wakaagiza pesa kibao ziwe printed zikaletwa nchini duh ikaharibu uchumi wao completely, kwenye principles of money mojawapo ni it should be scarce, yani pesa isiwe nyingi kwenye mzunguko maana ukiprint mihela mingi currency yako itashuka thamani ndio ka zimbabwe unaenda nunua mkate na bunda la pesa.. it's a very huge aspect this is the real world vitu haviwi solved kirahisi hivyo kijana

Sent using Jamii Forums mobile app
Wabongo bwana daah! Hivi waziri anaweza toa amri ela zika printiwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo kila mwenye printer atengeneze noti zake eeeeh! Nadhani hizo ndio zinaitwa Noti bandia..
 
Umeuliza swali zuri sana(logical question) cha msingi hapa ni kuwa kila nchi ina benki kuu ambayo ndiyo uratibu taratibu za kifedha na ndiyo inayoweza kuprint pesa za nchi husika kupitia sheria na taratibu za wizara ya fedha na nchi husika.Sasa katika swali lako la msingi kwa nini nchi ikope ili ali ina uwezo wa kutengeneza pesa yenyewe ni hivi uzalishaji/production ndiyo unadetermine kiwango cha pesa iliyopo kwenye mzunguko na sasa kama itaonekana pesa zimetengenezwa nyingi ina maana zitakuwa nyingi kwenye mzunguko kuliko production,hivyo kutasababisha mfumko wa bei kwani thamani ya vitu itakuwa juu kuliko thamani ya pesa ya nchi husika,uchumi utaharibika na ata power ya nchi kuimport bidhaa itakuwa dhaifu kabisa kwani itaitaji uwe na pesa nyingi muno kununua pesa ya kigeni,na hivyo uchumi utakuwa dhaifu na maisha ya wananchi kwa ujumla yatakuwa shida kuanzai kwa watu wa kawaida hadi kwa wafanyakazi.Kwa kuitimisha tu ni kwamba nchi yoyote ina uwezo huo ila tu haiwezi kufanya hivyo kutokana na taratibu za kiuchumi na pia taratibu za world bank.
 
"Kwanini Serekali inakopa kama inaweza ku-print noti mpya"
Swali lipo hivi mkuu, yaani kwa mfano kama huu. Sasa hivi serikali inajenga reli ya SGR kwa mkopo, ni kwanini basi tusiprint note mpya ili tujenge SGR kwa hela zetu hizo mpya badala yake tumeenda kukopa?
Kiuchumi kukopa kuna faida zaidi kuliko kuprint note mpya ila sometimes huwa wanaprint ila kwa taadhari kubwa sana na pia kutegemeana na sera za nchi kwa wakati huo.
So kuprint wanaprint ila lazima kufanywe kwa tahadhari kubwa sana otherwise uchumi utaanguka vibaya sana.
Exactly, nilitaka uondoe ile presumption inayojengeka kwamba hawaprint pesa kama namna moja wapo ya kukopa, pia nilitaka ufahamu kwamba hata kuchapisha pesa ni kukopa pia, means unawakopa wananchi wako, na usipowalipa in time basi bidhaa hupanda bei as a means of balancing the accounts
 
Habari zenu. Wanauchumi na wadau wengine wote humu ndani..

Naleta mada hii kwa misingi ya kutaka kuelewa, kama nchi inaweza Ku print noti mpya. Kwanini inakopa pesa?

Kwanini ina madeni kama uwezo wa kuyalipa na pesa mpya ipo

Kwa wenye uelewa. Tusaidiane tafadhali.
Mnisaidie concept ya "inflation" piaView attachment 1400170

Sent using Jamii Forums mobile app
Pesa sio yale makaratasi,Nithamani.Ndio maana sio lazima ulipwe cash,unaweza lipwa kwa checki,kwa bank trnasfer kwa mobile money etc kwa sababu ya value.So kwa lugha nyingine serikali hata ikichapa note lazima value iwe created ili kuwe na exchange.

Sasa kwa nini serikali inakopa badala ya kuchapa noti?Kwa sababu serikali haina uwezo wa kucreate value ya kutosha.Serikali inatengeneza value kwa kukusanya kodi toka kwa wananchi na hivyo kuweza kulipa gharama za kuendesha nchi.Ili wananchi walipe kodi lazima wazalishe value ama kwa kilimo,biashara au hata miamala na katika kuexchange value serikali inatoza hapo kodi kidogo ili iweze kujiendesha.Sasa iwapo serikali haiwezi kukusanya kodi ya kutosha kwa sababu yoyte ile basi inabidi itafuta watu ambao wameweze kucreate value ya ziada ambayo wameweka kama akiba au uwekezaji na kuwakopa ila watumie value hio kufanya mambo yake huku wakikusanya kodi kwa ajili ya kulipa deni.

Hivyo basi kuchapa noti bila kucreate value hakuwezi kutatua tatizo la serikali kukosa Pesa bali italiongoza kwa kuondoa incentive ambayo iatapunguza uzalishaji na hivyo uchumi kudorora.

Nimejaribu kutumia lugha nyepesi kama nimekosea kidogo nitwajibika.
 
Jamani, mtu anaomba kujizwa na ameonyesha kutokua na uelewa na ameuliza maswali ya msingi badala mumjibu munamcrash. Bragging eti nyie ndo wachumi. Aisee. Pole kaka. Bila shaka majibu umeshayapata.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao hao wanaomponda ni zero kichwani , hata wao hawajui wamjibu nin wamebaki kukariri Tu madesa ya demand and supply ,
 
Nimeyapata majibu ndugu Yangu asante kwa kuwa muelewa.

Hili Jukwaa Lina wahuni wachache, ila pia waelewa wapo.

Nimekiri kabisa kutokuwa na Uelewa ila bado MTU anakuambia " rudi shule usome Economics za form 2.".
Jamani, mtu anaomba kujizwa na ameonyesha kutokua na uelewa na ameuliza maswali ya msingi badala mumjibu munamcrash. Bragging eti nyie ndo wachumi. Aisee. Pole kaka. Bila shaka majibu umeshayapata.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitasoma Kuhusu Monetary Policy na Hizi issues kwa undani zaidi.

Asante kwa kunipa mwanga
Nakupa msaada kidgo ti,ila uende ukachimbue zaid:

Serikali yoyote,huwa na central bank yake ambayo inasimamia maswala ya fedha na kuhakikisha mzunguko wa pesa inakuwa vyema.

Katika uchumi,tuna sera kadhaa ambazo zinazungumzia uchumi wa taifa kwa ujumla na uchumi wa mtu mmoja mmoja,yaan aggregate economy and individual economy.

Aggregate demand ndio inahusika na mada yako.
Na hapo utasoma sera tofauto ambazo zinaelezea uchumi wa nchi unavyoendeshwa.

Kwa uchache,kuna sera ya monetary policy,ambayo yenyewe inazungumzia suala la usambazaji wa pesa na interest rate.
Hapa utaona namna ambavyo central banks,inavyopunguza bonds notes,na kuongeza interest rates ili ku control inflation katika taifa.

Naomba niishie hapo ila naomba utafute vitabu vya uchumi usome aggregate demand,macro economics.itakusaidia kukupa elimu zaid.

Siku zijazo nitafundisha somo la uchumi.
Lakin hadi jf watoe fulsa yakuwanyanyua watu wanaotoa mada hapa..atleast rewards,kuliko kupoteza mda bure.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Okeeey..

Kwahiyo suala LA kuchapisha noti ndio inashusha thamanicha pesa? Je hii ndio sababu shilingi 5 (dala) ya leo haina thamani tena.

Asante kwa maelezo yenye tija
Daah haya ngoja niweke neno. Kusema serikali haichapishi pesa si kweli, serikali huwa inachapisha pesa kama njia moja wapo ya kuwakopa wananchi wake (pesa kama pesa yenyewe ni worthless kama haiwi backed by goods na services zinazozalishwa au zilizopo)

Yaani serikali inapokosa fedha lets say ya mishahara, basi inaweza ikachapisha kiasi (limited amount) ili kulipa hiyo mishahara, ila hii inabidi ifanyike kwa kiasi kidogo sana ili kuepusha kushuka kwa thamani ya pesa (over inflation) ambapo utakuta mkate unapanda toka 1,000/= hadi 10,000/= pengine,

Hivyo pesa inaweza ikakosa thamani katika manunuzi na ikawa sawa na toilet paper tu. Sasa njia nyingine ya kukopa ndio hiyo ya mabenki ya kibiashara, mikopo toka mataifa rafiki na mashirika ya maendeleo kwa masharti/ riba maalum.

Na ukitaka kuamini serikali huwa inawakopa wananchi wake kwa kuchapisha pesa jiulize kwanini soda ilikuwa inauzwa 150/= ila leo inauzwa 500/=, means imewakopa wananchi na haijawalipa bado, otherwise soda ilipaswa iuzwe bei ile ile ya 150/=

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom