srinavas
JF-Expert Member
- Jun 5, 2011
- 4,024
- 3,585
Habari za Jumatatu wanajamvi,
Nipo hapa leo naangalia Al-Jazeera ikiwa imepita miezi zaidi ya Miwili sasa kwanzia mapigano haya ya IDF na wanamgambo wa HAMAS kuanza mnamo Tarehe 7 mwezi wa kumi.
Ni wazi kwamba wote tunaona na Ulimwengu unashuhudia kuwa wanaoumia zaidi na kupata hasara kubwa ni Raia wasio na hatia wa PALESTINA Hasa wanawake , Watoto na wazee. Kwa kweli IDF moto anaoupeleka sio wa mchezo. Yaani ni anawapiga kwelikweli bila ya huruma.
Lakini ndugu zangu mtakuwa mashahidi pia kwamba na Sisi watanzania Tumeumizwa sana baada ya kusambaa kwa video inayosemekana , Narudia Tena INAYOSEMEKANA au INAYODHANIWA kuwa ni ya Mtanzania Mwenzetu Joshua Mollel aliyekuwa mafunzoni Israel akiuwawa Kikatili sana na watu wanaosadikika kuwa ni wanamgambo Wa HAMAS (The Images are very much Disturbing)
Nikiri kwamba mwanzoni mwa Vita hii sikuwa Upande wowote kwani mimi ninachokiona kuwa suluhu ya Mgogoro huu ni TWO STATE Solution na pia nilikuwa nawaona HAMAS na kuwafananisha na Wapigania UHURU kama ambao tumeshuhudia kwenye nchi zetu mbalimbali za Africa wakifanya Armed struggle na wakafanikiwa kukomboa nchi zao. Lakini kwa Video hii inayosambaa Imebadilisha mawazo yangu kabisa, Kila saa najiuliza kwani kijana yule ana makosa gani? Kijana yule sio myahudi kwanza ni mweusi kabisa, je amewakosea nini Wale watu mpaka kumuua kwa namna ile?? Kwa kweli myenye majibu anisaidie.
Sasa basi, Kwa kuwa hawa watu wanaoitwa HAMAS wanasababisha matatizo makubwa sana kwa wapalestina na pia hata sisi watanzania wametugusa, Kwanini Raia wa PALESTINA wanaoteseka kama wanawajua walipo si wataje tu wakakamatwe au wakapigwe?
Hivi kweli inamaana watu wa PALESTINA pamoja na mateso yote wanayoyapata bado wameamua kuwaficha hawa watu? Maana Raia hawa wa PALESTINA Wanapata adhabu kutokana na madhila waliyoyafanya hawa jamaa ya Tarehe Saba October, Wao kama wanawajua walipo wawataje Mateka waachiwe, angalau vita isimame kwa muda kwanza watu warudi mezani kujadiliana. Ninaumia sana nikiona jinsi watoto wadogo wanakufa na kuumia , Yaani mtoto mdogo maskini ya mungu unakuta amekatika miguu, mara mtoto kakatika mkono. Hii inaniuma sana kila nikiona namuwaza mtoto wangu na watoto ninaowajua wa hapa tanzania nakuwa naumia sana
NB: Ninajua kwamba kabla ya Tarehe 7 mwezi wa kumi bado wapalestina walikuwa wanateseka, Hivyo tafadhali msianze kunipa historia ya mashariki ya kati maana naifatilia, mimi ninachoongelea hapa ni kwanzia 7th October 2023.
Nawasilisha
Ni mimi Srinavas Yoghendra Chintalapati kutoka Indhira Gandhi Street Dar es salaam.
Nipo hapa leo naangalia Al-Jazeera ikiwa imepita miezi zaidi ya Miwili sasa kwanzia mapigano haya ya IDF na wanamgambo wa HAMAS kuanza mnamo Tarehe 7 mwezi wa kumi.
Ni wazi kwamba wote tunaona na Ulimwengu unashuhudia kuwa wanaoumia zaidi na kupata hasara kubwa ni Raia wasio na hatia wa PALESTINA Hasa wanawake , Watoto na wazee. Kwa kweli IDF moto anaoupeleka sio wa mchezo. Yaani ni anawapiga kwelikweli bila ya huruma.
Lakini ndugu zangu mtakuwa mashahidi pia kwamba na Sisi watanzania Tumeumizwa sana baada ya kusambaa kwa video inayosemekana , Narudia Tena INAYOSEMEKANA au INAYODHANIWA kuwa ni ya Mtanzania Mwenzetu Joshua Mollel aliyekuwa mafunzoni Israel akiuwawa Kikatili sana na watu wanaosadikika kuwa ni wanamgambo Wa HAMAS (The Images are very much Disturbing)
Nikiri kwamba mwanzoni mwa Vita hii sikuwa Upande wowote kwani mimi ninachokiona kuwa suluhu ya Mgogoro huu ni TWO STATE Solution na pia nilikuwa nawaona HAMAS na kuwafananisha na Wapigania UHURU kama ambao tumeshuhudia kwenye nchi zetu mbalimbali za Africa wakifanya Armed struggle na wakafanikiwa kukomboa nchi zao. Lakini kwa Video hii inayosambaa Imebadilisha mawazo yangu kabisa, Kila saa najiuliza kwani kijana yule ana makosa gani? Kijana yule sio myahudi kwanza ni mweusi kabisa, je amewakosea nini Wale watu mpaka kumuua kwa namna ile?? Kwa kweli myenye majibu anisaidie.
Sasa basi, Kwa kuwa hawa watu wanaoitwa HAMAS wanasababisha matatizo makubwa sana kwa wapalestina na pia hata sisi watanzania wametugusa, Kwanini Raia wa PALESTINA wanaoteseka kama wanawajua walipo si wataje tu wakakamatwe au wakapigwe?
Hivi kweli inamaana watu wa PALESTINA pamoja na mateso yote wanayoyapata bado wameamua kuwaficha hawa watu? Maana Raia hawa wa PALESTINA Wanapata adhabu kutokana na madhila waliyoyafanya hawa jamaa ya Tarehe Saba October, Wao kama wanawajua walipo wawataje Mateka waachiwe, angalau vita isimame kwa muda kwanza watu warudi mezani kujadiliana. Ninaumia sana nikiona jinsi watoto wadogo wanakufa na kuumia , Yaani mtoto mdogo maskini ya mungu unakuta amekatika miguu, mara mtoto kakatika mkono. Hii inaniuma sana kila nikiona namuwaza mtoto wangu na watoto ninaowajua wa hapa tanzania nakuwa naumia sana
NB: Ninajua kwamba kabla ya Tarehe 7 mwezi wa kumi bado wapalestina walikuwa wanateseka, Hivyo tafadhali msianze kunipa historia ya mashariki ya kati maana naifatilia, mimi ninachoongelea hapa ni kwanzia 7th October 2023.
Nawasilisha
Ni mimi Srinavas Yoghendra Chintalapati kutoka Indhira Gandhi Street Dar es salaam.