mkuu enzi zile za JK kuna vikampuni vingi tu vya wahindi vilikuwa havipeleki michango ya wafanyakazi.
Alivyoingia magufuli wakapewa masharti ni lazima wafanyakazi wote wapewe mikataba,wafunguliwe akaunti za benki,mishahara yao ikatwe kodi na nssf.
Kuanzia mwaka juzi msisitizo ukatolewa hata kampuni nilizofanyia kazi wale wafanyakazi waliokuwa wanaitwa vibarua wote wamepewa mikataba,wakafunguliwa akaunti,wakaanza kukatwa kodi na nssf.
Hao wafanyakazi ninaokwambia walifanyakazi kwa miaka takribani 10 bila kukatwa kodi,nssf,hadi ilipofika mwaka juzi.
Jiulize kwa nini?japo unaleta ujuaji.