Kwanini niliamua kwenda kwa mganga

Kwanini niliamua kwenda kwa mganga

Mkuu wewe anzisha tu ya kwako na thread mpya maaana sasa tunasubiri mno chief72 haji kumalizia!!! Anaturusha roho!!

hahhaaa, ngoja kwanza nianze, nitakuwa naiandika kwnt .txt kwanza na kuiedit maana watu wanaonifahamu wakiisoma tu watajua real id yangu.
 
Kaiibua Nigeria. Mtoamada mwenyewe anasubiri part 2 aje aipesti
 
hahhaaa, ngoja kwanza nianze, nitakuwa naiandika kwnt .txt kwanza na kuiedit maana watu wanaonifahamu wakiisoma tu watajua real id yangu.
Haya mkuu tunasubiri ati maana hawa walozi wanaotaka madaraka kwa ndumba ni hatari sana.
 
duu story tamu.kweli.na inakoelekea ina fundisho kubwa..chief7 bado twasubiri baba..
 
Si umalizie nawewe!? Muone..................
 
Sawa lakini angemalizia ili tupate kitu kamili kwani kupata nusunusu inakera


labda kafuzu kutoka kwa Shigongo hamna kuandika story kamili kwa wakati mmoja ili atushike masikio na mchao vizuri hehehehe
 
baada ya kupandishwa cheo kazini na kukabidhiwa ofisi ndipo mambo yalipo anza, maisha niiyo lelewa ni ya kidini na hata wazazi wangu hawakuwa wa kuamini ki-viile mambo hayo, lakini baada ya kupandishwa cheo siku tano tu baada ya kupewa ofisi lilikuja zinga la joka mithili ya chatu mchana kweupeee, likipanda ngazi taratibu watu wakaliona kulipiga ikawa ishu hadi likafanikiwa kuingia ofisini mwangu, liliruka ofisi zote za jirani na kuingia ofisini kwangu,niliwaita watu wenye uzoefu wa kupiga nyoka wakaingia ofisini kulitafuta halikuonekana hadi hii leo yapata mwaka, licha ya kutoa kila kitu ktk ofisi, vitimbi havikuishia hapo siku ingine mara nikute ofisi nzima imejaa sisimizi.usiku ndo usiseme, nikaona niandike barua ya kuachia nafasi kwa boss ili kunusuru roho yangu, kabla sijaikabidhi kwa boss nikaomba ushauri kwa jaaa zangu ambao wanafanya ofisi zingine, wakanishauri kufanya ivo ni uzaifu mkubwa jamaa mmoja akanishauri niwaone viongozi wa dini ila kwa angalizo kama imani ninayo, ki ukweli nikapima tabia yangu nikaona imani nilonayo ni kwa kuabudu tu na si kwa kupambana na washirikina.penye wengi pana mengi jamaa mmoja akasema nakupa namba ya mtu atakusaidia, nikapiga namba nilopewa ikapokewa nikaomba kuonana nae akanambia njoo sheli naweka mafuta pikipiki yangu, kweli kufika sheri nikamkuta, cha ajabu sikuamini kuona mganga mwenyewe kijana tu afu kapiga pamba kama mwanamziki wa bongo fleva, kumuuliza kama ndiye akajibu naa ndio mimi, kwa kuwa nilikuwa na gari akasea nimfuate twende kwake, yeye akiwa kwenye pikipiki, kufika kwake nivoingia nikakuta sebule ya kawaida haina hata kibuyu wala nini, kwa hali hiyo nikaanza ingiwa na hofu kuwa huyu si mganga atakuwa tapeli tu, nilipoketi akaanza kunihoji wapi nilipata namba yake, nikajibu kuwa wewe ni mtu mkubwa bwana namba yako ya simu sio ishu. akaniuliza dhumuni langu au shida hasa ni nini?nikamuelezea yoote, cha ajabu akaniabia okey nimekuelewa ila nenda nitakupigia simu, nilishangaa style hii ya uganga, kweli baada ya siku mbili akaniita kwa simu nikaenda, akanambia....mimi kazi za uganga huwa sipendi kufanya kwani mi ni mjasiria mali lakini nikiamua kufanya sibahatishi hata kidigo, nasimamisha shuguli zangu kwa muda tupambane na hao washenzi wanaojifanya wao vidume wa kupika vyungu, picha lina anza akaniambia niende stationery nikanunua bunda la karatasi la Rim-A4, nikaenda kulinunua nikarudi akatoa karatasi kama ishirini akanipa nizikanyage,na mambo mawili matatu ya waganga, akazichukua zile karatasi huwezi amini zilikuwa zina maandishi chungu mzima akazisoma na hakuniambia kitu na baadae akazichoma moto............part 1;stay tuned for part 2...ni habari ilonitokea na ni ukweli..........

Mkuu umeikatishia pahala pa tamu. Hata hivyo jitahidi kuandika katika aya
 
Mhhhhhhhh..hatari sana maofisini heri yangu mjasiriamali, natoka kidogo mtanijuza history itakapoendelea!!
 
Endelea basi au wakazini ndie alikutenda huyo aliekupa namba ukatapeliwa bila kujijua?
 
Nasikitika haukufuata njia ya Mungu, as imani yako ingejengeka tu.
 
Back
Top Bottom