Kwanini ndege haiwezi kufikia anga ya bluu?

Kwanini ndege haiwezi kufikia anga ya bluu?

K 4 LIFE

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2015
Posts
2,567
Reaction score
419
Wakuu,

Kama una uzoefu wa kusafiri kwa ndege, hivi ulishawahi kujiuliza kwa nini ndege ina uwezo wa kufikia mawingu meupe ya mvua lakini haina ubavu wa kufikia anga/ mawingu ya bluu? Why?
 
Ndege gani hizo unazo maanisha wewe..?
ndege za kijeshi au ndege za watalii..?
Maana usije kuwa una zungumzia ndege za kuwindia wanyama
mbugani.
 
Ndege gani hizo unazo maanisha wewe..?
ndege za kijeshi au ndege za watalii..?
Maana usije kuwa una zungumzia ndege za kuwindia wanyama
mbugani.

mkuu ndege za abiria na kivita
 
Hakuna anga lionekalo kwa Rangi uliyosema ,,,,,, unachokiona sio anga ila mwisho wa uwezo wa macho yako kuona

kwa hiyo una maanisha uwezo wa binadamu kuona ni hiyo anga ya bluu? acha uongo wewe
 
Mkuu hakuna wingi na bluu, ile rangi unayoiona ndio mwisho wako uwezo wako wa macho kuona. Halafu zyale maroketi ya Marekani yanapita huku yanapokwenda mwezini na kule kwenye satellite
 
Mkuu hakuna wingi na bluu, ile rangi unayoiona ndio mwisho wako uwezo wako wa macho kuona. Halafu zyale maroketi ya Marekani yanapita huku yanapokwenda mwezini na kule kwenye satellite

mkuu mbona ndege za abiria hazifikii huko?
 
Mambo mengine kwa akili za kibinadamu ni vigumu kufahamu ila kwa wale wasomaji wa Biblia watakubaliana na mimi kuwa ile wanayo inona bluu kule juu ni maji.
 
kwa hiyo una maanisha uwezo wa binadamu kuona ni hiyo anga ya bluu? acha uongo wewe

Usiwe Ukawa wewe,hakuna mawingu ya bluu,hiyo bluu unayoiona ni mwisho wa uwezo wako wa kuona....hata ukitumia kifaa gani huwezi ukafika sehemu ukasema hapa ndo kwenye anga la bluu...mfano mwingine ni kwenye barabara ndefu iliyonyooka unaona kama kwa mbali kuna majimaji na vijimoshimoshi lakini ukifika pale hukuti maji wala hivo vijimoshimoshi....rudi shule sasa ni elimu bure
 
Kwanza anga haina limit, usitarajie kuna mpaka labda una mkeka umetandikwa ndo uite anga. Unachoona ni chembe chembe za gesi na hewa ambayo kwa mbali unaona hiyo rangi lakini kadiri unavosogelea huwezi kuona hiyo rangi unayosema.

kidogo nakubaliana nawe
 
Mambo mengine kwa akili za kibinadamu ni vigumu kufahamu ila kwa wale wasomaji wa Biblia watakubaliana na mimi kuwa ile wanayo inona bluu kule juu ni maji.

mkuu acha fiksi bana unamaanisha yale ya blue ni maji? duh hii kali bana,kwa hiyo siku yakimwagika wote tuna RIP kwa mafuriko,ngoja kwanza niwatonye DAWASCO
 
Back
Top Bottom