Fitinamwiko
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 4,803
- 1,416
Nimesoma habari ya Mh Nape kushangiliwa alipoingia katika ukumbi wa Mkutano wa Uchaguzi wa viongozi wa UVCCM Taifa pale Dodoma.
Vijana waliamini uwepo wa Mh Nape katika uchaguzi ule, kwa kiasi kikubwa kungepunguza matumizi ya rushwa kwa wajumbe wa mkutano. Kama tunavyofahamu, ndugu Nnauye ni mmoja wa wahubiri wa kupinga falsafa ya UFISADI na MAFISADI ndani ya CCM. Baada ya Mh Nape kufanya lile Vijana wengi walilotegemea la kuwakabili watoa rushwa ambao walikuwepo meta chache toka mjengoni na wanajulikana, Nape alikimbiria jukwaani na kuchukua gitaa na kuanza kuburudisha wajumbe na kuweka mandhari muluwaa kwa watoa rushwa.
Kila siku nasema "Nape hajui kazi yake" alijua fika kulikuwa na mivutano pamoja na rushwa nje nje, kama angetimiza wajibu wake, kuangalia kitu gani kinaendelea, rushwa isingeshinda uchaguzi ule. Kwa Nape gitaa lilikuwa bora na kuwaangusha vijana wengi waliomtarajia, matokeo yake umoja unamegeka.
Kama wajumbe wangejua Mh Nape alikwenda mkutanoni kupiga GITAA na sio kuwakabili MAFISADI, je wangemshangilia?
Vijana waliamini uwepo wa Mh Nape katika uchaguzi ule, kwa kiasi kikubwa kungepunguza matumizi ya rushwa kwa wajumbe wa mkutano. Kama tunavyofahamu, ndugu Nnauye ni mmoja wa wahubiri wa kupinga falsafa ya UFISADI na MAFISADI ndani ya CCM. Baada ya Mh Nape kufanya lile Vijana wengi walilotegemea la kuwakabili watoa rushwa ambao walikuwepo meta chache toka mjengoni na wanajulikana, Nape alikimbiria jukwaani na kuchukua gitaa na kuanza kuburudisha wajumbe na kuweka mandhari muluwaa kwa watoa rushwa.
Kila siku nasema "Nape hajui kazi yake" alijua fika kulikuwa na mivutano pamoja na rushwa nje nje, kama angetimiza wajibu wake, kuangalia kitu gani kinaendelea, rushwa isingeshinda uchaguzi ule. Kwa Nape gitaa lilikuwa bora na kuwaangusha vijana wengi waliomtarajia, matokeo yake umoja unamegeka.
Kama wajumbe wangejua Mh Nape alikwenda mkutanoni kupiga GITAA na sio kuwakabili MAFISADI, je wangemshangilia?