FortJeasus
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 603
- 397
Wiki moja tangu kuzinduliwa kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru Mashariki, nimeamua nifanye tathimini juu ya mwelekeo na mwenendo wa vipengele (components) 6 kama vilivyojidhihirisha na kisha kufuatiliwa na kuzingatiwa.Ili kuweza kuelewa mantiki iliyo nyuma ya hitimisho hapo juu,tuangalie viashiria (indicators) ambavyo kwazo mwenendo mzima wa kampeni umepimwa:
1.Kama kawaida,kampeni za CDM zimekuwa,kutokana na kuongozwa na wajenzi mahiri wa hoja, hususani Nassari, zikiongozwa kwa nguvu za hoja,zenye kushawishi akili,zinazovuta hisia za wasikilizaji, zikiambatana na masuluhisho ya matatizo mbalimbali ya wana -Arumeru.Kwa mfano ,tatizo la ukosefu wa ardhi linalotokana na kumilikishwa wawekezaji huku wananchi wakiachwa bila rasilimali hiyo muhimu.
2.Upepo mbaya unaovuma dhidi ya CCM kwa kushindwa kutatua matatizo yanayowakumba wakazi wa Arumeru Mashariki kama vile maji na ardhi,huku makada kadhaa wa CCM wakiwaaminisha wananchi kuwa sasa umefika wakati wa kutatua matatizo hayo kwa sharti kwamba wapewe kura za ubunge kwa mara nyingine tena.Inavyoelekea ,wananchi wengi wameikataa hoja hii.Hili lina mfanano wa kimantiki na harakati za miaka ya 1960 za kudai uhuru wa Tanganyika , ambapo mkoloni alitaka akubaliwe kuendelea kutawala licha ya kushindwa kuboresha maisha ya Watanganyika, kwa kutotoa huduma bora za jamii ,pamoja na kushindwa kuheshimu na kuthamini ubinadamu wetu.Sote tunafahamu Kambarage na wanaharakati wenzake ,wakiungwa mkono na Watanganyika wenzao, hawakuwa tayari kuendelea kuwapa wakoloni fursa ya kututawala,wakiamini kuwa haiwezekani kupata jibu tofauti kwa kuendelea kutumia mbinu zile zile.
3.Udhaifu wa kampeni za CCM, unaochangiwa , kwa kiwango kikubwa na uwezo mdogo wa kujenga hoja za kiakili unaoonyeshwa na mgombea wake, pamoja na udhaifu wa haiba na kimaadili miongoni mwa baadhi ya makada wa CCM wanaoongoza kampeni Arumeru.Aidha makada hao,tena wanaoonekana wamepata kupita shule,wanawaghilibu wananchi kuwa eti CHADEMA hawana serikali na hivyo hawapaswi kupewa nafasi ya kutoa mbunge Arumeru Mashariki!!Iwapo hoja hii ina ukweli wowote, inashangaza kwa nini wahusika hadi sasa hawaelezi kwa nini serikali hiyo hiyo ya CCM ,imewapa wana Arumeru fursa ya kuchagua mwakilishi wake!Wala hawataki kueleza kuwa maendeleo (uwekezaji ktk huduma za kijamii na kiuchumi) ni haki ya msingi ya wananchi, kwanza kama walipa kodi wa nchi hii, na pia kama watu wenye uhalali na mamlaka ya kikatiba kupata ama hata kudai haki za kiuchumi,kisiasa,na kijamii ,pasipo kuzingatia ufuasi,uanachama wa chama cha kisiasa.
4.Kama ilivyo hulka yake,CCM inaendelea kuamini na kutumia muda mwingi kwa kupiga nyimbo za mipasho kanakwamba hii ni silaha kuu mikononi mwake -ingawa ni sehemu mojawapo ya kampeni -na kupoteza muda ambao ungeweza kutumika kujadili masuala muhimu na kuvutia kura.
5.Faida ya kijiografia.Arumeru Mashariki inapakana kwa karibu kabisa na jimbo la Arusha Mjini, Hai na Moshi Mjini, na kupelekea majimbo haya kuwa na maingiliano makubwa ya kijamii ,kibiashara na kisiasa sawia. Imedhihirika, sasa, wana- Arumeru wamehamasika na sasa wapo tayari kufanya kile kilichopata kufanywa na jirani zao:kuikataa CCM na matendo yake.
6.Kutokana na pointi namba 5 ,upo uwezekano mkubwa wa kupata mawakala waaminifu kwa kutilia maanani kuwa, pamoja na umuhimu wa kufanya kampeni makini, ni lazima wapatikane mawakala imara na walinzi wa kura .Kwa kuwa Arumeru ipo jirani na Arusha Mjini na Moshi Mjini - maeneo yenye Vyuo kadhaa vya Elimu ya Juu ,na ambapo CDM ina makada wa kutosha - kuna uhakika wa kupata mawakala waaminifu kwa chama. John Mnyika ,mwaka 2010, pamoja na kutumia wananchi wa kawaida walio waaminifu kama mawakala, alitumia pia na vijana wa Vyuo vya Elimu ya Juu wa Dar er Saalam walioimarisha usalama wa kura.
Nawasilisha.
1.Kama kawaida,kampeni za CDM zimekuwa,kutokana na kuongozwa na wajenzi mahiri wa hoja, hususani Nassari, zikiongozwa kwa nguvu za hoja,zenye kushawishi akili,zinazovuta hisia za wasikilizaji, zikiambatana na masuluhisho ya matatizo mbalimbali ya wana -Arumeru.Kwa mfano ,tatizo la ukosefu wa ardhi linalotokana na kumilikishwa wawekezaji huku wananchi wakiachwa bila rasilimali hiyo muhimu.
2.Upepo mbaya unaovuma dhidi ya CCM kwa kushindwa kutatua matatizo yanayowakumba wakazi wa Arumeru Mashariki kama vile maji na ardhi,huku makada kadhaa wa CCM wakiwaaminisha wananchi kuwa sasa umefika wakati wa kutatua matatizo hayo kwa sharti kwamba wapewe kura za ubunge kwa mara nyingine tena.Inavyoelekea ,wananchi wengi wameikataa hoja hii.Hili lina mfanano wa kimantiki na harakati za miaka ya 1960 za kudai uhuru wa Tanganyika , ambapo mkoloni alitaka akubaliwe kuendelea kutawala licha ya kushindwa kuboresha maisha ya Watanganyika, kwa kutotoa huduma bora za jamii ,pamoja na kushindwa kuheshimu na kuthamini ubinadamu wetu.Sote tunafahamu Kambarage na wanaharakati wenzake ,wakiungwa mkono na Watanganyika wenzao, hawakuwa tayari kuendelea kuwapa wakoloni fursa ya kututawala,wakiamini kuwa haiwezekani kupata jibu tofauti kwa kuendelea kutumia mbinu zile zile.
3.Udhaifu wa kampeni za CCM, unaochangiwa , kwa kiwango kikubwa na uwezo mdogo wa kujenga hoja za kiakili unaoonyeshwa na mgombea wake, pamoja na udhaifu wa haiba na kimaadili miongoni mwa baadhi ya makada wa CCM wanaoongoza kampeni Arumeru.Aidha makada hao,tena wanaoonekana wamepata kupita shule,wanawaghilibu wananchi kuwa eti CHADEMA hawana serikali na hivyo hawapaswi kupewa nafasi ya kutoa mbunge Arumeru Mashariki!!Iwapo hoja hii ina ukweli wowote, inashangaza kwa nini wahusika hadi sasa hawaelezi kwa nini serikali hiyo hiyo ya CCM ,imewapa wana Arumeru fursa ya kuchagua mwakilishi wake!Wala hawataki kueleza kuwa maendeleo (uwekezaji ktk huduma za kijamii na kiuchumi) ni haki ya msingi ya wananchi, kwanza kama walipa kodi wa nchi hii, na pia kama watu wenye uhalali na mamlaka ya kikatiba kupata ama hata kudai haki za kiuchumi,kisiasa,na kijamii ,pasipo kuzingatia ufuasi,uanachama wa chama cha kisiasa.
4.Kama ilivyo hulka yake,CCM inaendelea kuamini na kutumia muda mwingi kwa kupiga nyimbo za mipasho kanakwamba hii ni silaha kuu mikononi mwake -ingawa ni sehemu mojawapo ya kampeni -na kupoteza muda ambao ungeweza kutumika kujadili masuala muhimu na kuvutia kura.
5.Faida ya kijiografia.Arumeru Mashariki inapakana kwa karibu kabisa na jimbo la Arusha Mjini, Hai na Moshi Mjini, na kupelekea majimbo haya kuwa na maingiliano makubwa ya kijamii ,kibiashara na kisiasa sawia. Imedhihirika, sasa, wana- Arumeru wamehamasika na sasa wapo tayari kufanya kile kilichopata kufanywa na jirani zao:kuikataa CCM na matendo yake.
6.Kutokana na pointi namba 5 ,upo uwezekano mkubwa wa kupata mawakala waaminifu kwa kutilia maanani kuwa, pamoja na umuhimu wa kufanya kampeni makini, ni lazima wapatikane mawakala imara na walinzi wa kura .Kwa kuwa Arumeru ipo jirani na Arusha Mjini na Moshi Mjini - maeneo yenye Vyuo kadhaa vya Elimu ya Juu ,na ambapo CDM ina makada wa kutosha - kuna uhakika wa kupata mawakala waaminifu kwa chama. John Mnyika ,mwaka 2010, pamoja na kutumia wananchi wa kawaida walio waaminifu kama mawakala, alitumia pia na vijana wa Vyuo vya Elimu ya Juu wa Dar er Saalam walioimarisha usalama wa kura.
Nawasilisha.