Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,278
- 8,868
Naombeni tutafakari ni kwanini Mpendazoe hakupewa mafao yake ya ubunge wakati ule,Lakini Zitto anapewa?
Hili si jambo la kupuuza kwa ustawi wa Demokrasia yetu na sheria za nchi.
Ni vema tujadili kujua kama bunge letu lina upendeleo wa sheria au kanuni?
Tujiulize angekuwa Lissu Mnyika,Wenje au Mnyaa wangepewa?
Hili si jambo la kupuuza kwa ustawi wa Demokrasia yetu na sheria za nchi.
Ni vema tujadili kujua kama bunge letu lina upendeleo wa sheria au kanuni?
Tujiulize angekuwa Lissu Mnyika,Wenje au Mnyaa wangepewa?
*************** Majibu kutoka kwa Zitto ****************
Naomba niweke sawa kidogo tu kuondoa upotoshaji wa makusudi. Kwanza mimi nasikia tu kwenye vyombo vya habari kuhusu suala la mafao. Halinisumbui. Nawakumbusha;
- Toka mwaka 2011 mwezi Juni niliacha kupokea posho za vikao. Kwa mwaka posho za vikao ni takribani shs 24 milioni.
- Wabunge hupewa msamaha wa kodi kwenye magari wanayonunua. Kwa kuwa napinga misamaha ya kodi nilikataa na mpaka namaliza ubunge sijatumia msamaha huo wa kodi.
Kwa hiyo suala la fedha sio suala la msingi kabisa kwangu kwenye maamuzi yangu.
Fact: Mpendazoe alilipwa kiinua mgongo chake kwa muda wa miezi aliyotumikia Bunge. Sio kweli kwamba hakupewa kiinua mgongo chake. Alipewa na tunaweza kuthibitisha
Last edited by a moderator: