Kuna rafiki yangu alikuwa Mkurugenzi wa masoko wa Vodacom lakini line ya simu anayotumia ni Tigo. Kuna siku Mzee Baharesa nilimuona anakunywa maji ya Kilimanjaro wakati yeye ana maji yake ya Uhai. Mo Dewji ukimkuta pale New Africa hotel ambapo ni kama sebuleni kwake sijawahi kumuona akiagiza maji ya Masafi ambayo ni yake, yeye anaagiza Kilimanjaro maji. Mzee marehemu Mengi peke yake alikuwa proud na bidhaa zake, maji kwake yalikuwa Kilimanjaro tu. Haya kwenye mgahawa wa IPP pale The Guardian hiluwezi kukuta soda nyingine zaidi ya kampuni ya Coca-Cola na maji ya Kilimajaro.