Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Kila tunapopata wasaa wa kujadili uchumi na hali za maisha ya watanzania, tumekuwa na jadi ya kuangalia zaidi hali ilivyo kitaifa na kisekta (MACRO LEVEL), bila ya kujadili sana hali na takwimu kimikoa/kiwilaya/kivijiji (MICRO LEVEL). Pamoja na kwamba huwa tunajadili hali za maisha ya watanzania waliopo vijijini, ni mara chache sana kwa sisi kudadisi hali za ndugu zetu hawa kwa undani, na huwa hatuendi mbali zaidi tu ya kutambua kwamba wingi wao ni karibia 70% ya jumla watanzania wote (milioni 42), na pia kutambua kwamba wengi wao (karibia 80%), wanajishughulisha na Kilimo.
Nia yangu ni kujaribu kuja na mada itakayotusaidia kuziba pengo hili la mjadala. Katika post yangu ya kwanza, sitajadili lolote zaidi ya kuweka tu takwimu muhimu na kumalizia kwa maswali ambayo nina amini yatatusaidia kuupa mjadala uhai.
Kwanza nadhani ni muhimu tuka tazama takwimu za uzalishaji wa sekta mbalimbali/mchango wa sekta mbalimbali katika Pato la Taifa (GDP), kwa kufananisha mwaka 2000 na mwaka 2010. Takwimu hizi zitakuwa na msaada katika mjadala, hasa kutusaidia kuelewa kwa undani kuhusu sekta gani zinatoa fursa zaidi za ajira, sekta zipi zinapanuka/zinasinyaa pamoja na madhara kwa umaskini kutokana na kupanuka/kusinyaa kwa sekta husika n.k..
Table 1: Mchango wa Sekta Katika Uzalishaji/Pato La Taifa
Takwimu za pili ambazo ni muhimu sana zinahusu pato la kila mtanzania kwa mwaka (GDP Per Capita) kwa kila mkoa wa Tanzania. Tufahamu tu kwamba duniani kote, GDP Per Capita ni kiashiria (indicator) cha hali ya wananchi kiuchumi i.e. kipato/income. Zifuatazo ni takwimu za pato la kila Mtanzania kwa mwaka 2010. Nimechukua kumi bora na kuziweka in ‘order of ranking':
Table 2: Vipato Vya Watanzania Kulingana na Mikoa Wanayotoka (GDP Per Capita)
Je, ni Mikoa ipi yenye vipato duni?
Table 3: Mikoa Maskini kuliko yote kwa kigezo cha Pato La Kila Mwananchi (GDP Per Capita)
Je, ni Mikoa ipi inachangia Zaidi Kwenye Pato la Taifa/Inayozalisha Bidhaa na Huduma Nyingi Zaidi Tanzania (GDP)?
Table 4: Kumi Bora Kwa Uzalishaji Wa Bidhaa na Huduma (GDP).
*Ukitazama orodha hii, ipo mikoa 12 na sio 10. Hii ni kwa sababu kuna mikoa miwili inalingana (Ruvuma na Tabora), na pia nimeongezea Mkoa wa Rukwa kwa makusudi kwa sababu upo katika kundi linaloitwa "The Big Four".
Je, ni Mikoa ipi yenye michango midogo zaidi kwenye pato la taifa/uzalishaji mdogo zaidi wa bidhaa na huduma Tanzania?
Table 5: Mikoa Yenye Michango Midogo Katika Uzalishaji/Pato la Taifa (bottom 5).
Je, Mikoa Ipi Hupewa Kipaumbele Katika Bajeti? Kwa mfano, kwa mwaka 2010, jumla ya bajeti iliyotengwa kwa ajili ya mikoa yote Tanzania ilikuwa T.sh trilioni 1.7. Ifuatayo ni orodha ya mikoa iliyopewa kipaumbele zaidi.
Table 6: Orodha ya kumi bora – vipaumbele katika Bajeti Ya Serikali.
Je, ni mikoa ipi inayotengewa fedha ndogo zaidi katika Bajeti ya Serikali?
Table 7: Mikoa Isiyopewa Kipaumbele Katika Bajeti Ya Serikali (Bottom five).
Yafuatayo ni baadhi ya maswali ambayo nadhani yanaweza kuipa mada hii uhai zaidi:
1. Je, wabunge wanapojadili bajeti na kujenga hoja mbali mbali kuhusu udogo au ukubwa wa bajeti husika, huwa wanazingatia nini zaidi? Umuhimu wa Sekta? Umuhimu wa Mikoa kiuchumi? Hali za wananchi kijamii na kiuchumi katika mikoa husika? Vigezo vya kisiasa?
2. Je, takwimu hizi zina ashiria nini juu ya malengo ya serikali kwenye sekta za kilimo na viwanda?
3. Je, Serikali inatumia vigezo gani kutenga viwango tofauti vya bajeti kwa mikoa:
· Mchango wa mkoa/mikoa husika katika pato la taifa/uzalishaji wa bidhaa na huduma?
· Hali ya za kiuchumi na kijamii za wananchi katika mikoa husika?
· Vigezo vya kisiasa?
4. Je, ile mikoa inayoitwa "The Big Four" – Iringa, Mbeya, Rukwa, na Ruvuma, hadhi hii inatokana na kigezo/vigezo gani?
· Mchango wa mikoa hii minne katika uzalishaji wa mazao ya chakula (food crops)?
· Mchango wao katika uzalishaji wa Kilimo kwa ujumla (food and cash crops)?
· Mchango wao wa jumla katika Pato la Taifa (GDP)?
5. Na mwisho, Je, nini iwe kipaumbele cha taifa (budget priority) kwa mwaka huu wa fedha na hata siku za usoni?
Nia yangu ni kujaribu kuja na mada itakayotusaidia kuziba pengo hili la mjadala. Katika post yangu ya kwanza, sitajadili lolote zaidi ya kuweka tu takwimu muhimu na kumalizia kwa maswali ambayo nina amini yatatusaidia kuupa mjadala uhai.
Kwanza nadhani ni muhimu tuka tazama takwimu za uzalishaji wa sekta mbalimbali/mchango wa sekta mbalimbali katika Pato la Taifa (GDP), kwa kufananisha mwaka 2000 na mwaka 2010. Takwimu hizi zitakuwa na msaada katika mjadala, hasa kutusaidia kuelewa kwa undani kuhusu sekta gani zinatoa fursa zaidi za ajira, sekta zipi zinapanuka/zinasinyaa pamoja na madhara kwa umaskini kutokana na kupanuka/kusinyaa kwa sekta husika n.k..
Table 1: Mchango wa Sekta Katika Uzalishaji/Pato La Taifa
SEKTA | MWAKA 2000 (%) | MWAKA 2010 (%) |
Kilimo, uwindaji na Misitu · Mazao · Mifugo · Misitu na Uwindaji | 29% · 21.7% · 5.1% · 2.7% | 24.1% · 17.8% · 3.8% · 2.4% |
Uvuvi | 1.8% | 1.4% |
Industry and Construction | 19.9% | 22.4% |
· Madini | · 1.5% | · 3.3% |
· Viwanda | · 8.8% | · 9.0% |
· Umeme na Gesi | · 2.1% | · 1.8% |
· Maji (Water Supply) | · 0.5% | · 0.4% |
· Construction (Ujenzi) | · 5.2% | · 8.0% |
Service Sector/Sekta ya Huduma | 45.3% | 43.9% |
· Trade and Repairs | · 12.8% | · 12.1% |
· Hotels and Restaurants | · 2.8% | · 2.3% |
· Transport | · 5.5% | · 5.1% |
· Communications | · 1.2% | · 2.1% |
· Financial Services | · 1.6% | · 1.8% |
· Real Estate and Business Services | · 10.7% | · 8.8% |
· Public Administration | · 6.6% | · 8.0% |
· Education | · 2.1% | · 1.4% |
· Health | · 1.2% | · 1.6% |
· Other Social and Personal Services | · 0.9% | · 0.6% |
Takwimu za pili ambazo ni muhimu sana zinahusu pato la kila mtanzania kwa mwaka (GDP Per Capita) kwa kila mkoa wa Tanzania. Tufahamu tu kwamba duniani kote, GDP Per Capita ni kiashiria (indicator) cha hali ya wananchi kiuchumi i.e. kipato/income. Zifuatazo ni takwimu za pato la kila Mtanzania kwa mwaka 2010. Nimechukua kumi bora na kuziweka in ‘order of ranking':
Table 2: Vipato Vya Watanzania Kulingana na Mikoa Wanayotoka (GDP Per Capita)
MKOA | PATO LA KILA MWANANCHI KWA MWAKA (T.Shillings) (2010) |
1. Dar-es-salaam | 1,740,947 (million) |
2. Iringa | 979,882 (laki) |
3. Arusha | 945,437 |
4. Mbeya | 892,877 |
5. Kilimanjaro | 879,432 |
6. Ruvuma | 866,191 |
7. Mwanza | 829,647 |
8. Tanga | 763,203 |
9. Morogoro | 744,234 |
10. Rukwa | 726,658 |
Je, ni Mikoa ipi yenye vipato duni?
Table 3: Mikoa Maskini kuliko yote kwa kigezo cha Pato La Kila Mwananchi (GDP Per Capita)
MKOA | PATO LA KILA MWANANCHI KWA MWAKA (T.Shillings) (2010) |
1. Singida | 483,922 (laki) |
2. Dodoma | 485,211 (laki) |
3. Kagera | 491,713 (laki) |
4. Kigoma | 499,428 (laki) |
5. Tabora | 528,832 (laki) |
Je, ni Mikoa ipi inachangia Zaidi Kwenye Pato la Taifa/Inayozalisha Bidhaa na Huduma Nyingi Zaidi Tanzania (GDP)?
Table 4: Kumi Bora Kwa Uzalishaji Wa Bidhaa na Huduma (GDP).
MKOA | UZALISHAJI WA BIDHAA NA HUDUMA (GDP) T.shillings (2010) |
1. Dar-es-salaam | T.sh 5.4 trillioni |
2. Mwanza | T.sh 3.0 trillioni |
3. Mbeya | T.sh 2.3 trillioni |
4. Shinyanga | T.sh 1.9 trillioni |
5. Iringa | T.sh 1.7 trillioni |
6. Morogoro | T.sh 1.6 trillioni |
7. Arusha | T.sh 1.5 trillioni |
8. Kilimanjaro | T.sh 1.3 trillioni |
9. Kagera | T.sh 1.3 trillioni |
10. Ruvuma | T.sh 1.2 trillioni |
11. Tabora | T.sh 1.2 trillioni |
12. Rukwa | T.sh 1.1 trillioni |
*Ukitazama orodha hii, ipo mikoa 12 na sio 10. Hii ni kwa sababu kuna mikoa miwili inalingana (Ruvuma na Tabora), na pia nimeongezea Mkoa wa Rukwa kwa makusudi kwa sababu upo katika kundi linaloitwa "The Big Four".
Je, ni Mikoa ipi yenye michango midogo zaidi kwenye pato la taifa/uzalishaji mdogo zaidi wa bidhaa na huduma Tanzania?
Table 5: Mikoa Yenye Michango Midogo Katika Uzalishaji/Pato la Taifa (bottom 5).
MKOA | UZALISHAJI WA BIDHAA NA HUDUMA (GDP) T.shillings (2010) |
1. Singida | T.sh Billioni 661 |
2. Pwani | T.sh Billioni 608 |
3. Lindi | T.sh Billioni 621 |
4. Kigoma | T.sh Billioni 906 |
5. Mtwara | T.sh Billioni 927 |
Je, Mikoa Ipi Hupewa Kipaumbele Katika Bajeti? Kwa mfano, kwa mwaka 2010, jumla ya bajeti iliyotengwa kwa ajili ya mikoa yote Tanzania ilikuwa T.sh trilioni 1.7. Ifuatayo ni orodha ya mikoa iliyopewa kipaumbele zaidi.
Table 6: Orodha ya kumi bora – vipaumbele katika Bajeti Ya Serikali.
MKOA | BAJETI YA MWAKA (T.sh) |
1. Dar-es-salaam | T.sh Billioni 154 |
2. Mwanza | T.sh Billioni 135 |
3. Mbeya | T.sh Billioni 109 |
4. Shinyanga | T.sh Billioni 104 |
5. Kilimanjaro | T.sh Billioni 100 |
6. Tanga | T.sh Billioni 92 |
7. Kagera | T.sh Billioni 88 |
8. Morogoro | T.sh Billioni 86 |
9. Iringa | T.sh Billioni 85 |
10. Arusha | T.sh Billioni 81 |
Je, ni mikoa ipi inayotengewa fedha ndogo zaidi katika Bajeti ya Serikali?
Table 7: Mikoa Isiyopewa Kipaumbele Katika Bajeti Ya Serikali (Bottom five).
MKOA | BAJETI YA MWAKA (T.sh) |
1. Mtwara | T.sh Billioni 57 |
2. Kigoma | T.sh Billioni 56 |
3. Singida | T.sh Billioni 50 |
4. Manyara | T.sh Billioni 54 |
5. Rukwa | T.sh Billioni 49 |
Yafuatayo ni baadhi ya maswali ambayo nadhani yanaweza kuipa mada hii uhai zaidi:
1. Je, wabunge wanapojadili bajeti na kujenga hoja mbali mbali kuhusu udogo au ukubwa wa bajeti husika, huwa wanazingatia nini zaidi? Umuhimu wa Sekta? Umuhimu wa Mikoa kiuchumi? Hali za wananchi kijamii na kiuchumi katika mikoa husika? Vigezo vya kisiasa?
2. Je, takwimu hizi zina ashiria nini juu ya malengo ya serikali kwenye sekta za kilimo na viwanda?
3. Je, Serikali inatumia vigezo gani kutenga viwango tofauti vya bajeti kwa mikoa:
· Mchango wa mkoa/mikoa husika katika pato la taifa/uzalishaji wa bidhaa na huduma?
· Hali ya za kiuchumi na kijamii za wananchi katika mikoa husika?
· Vigezo vya kisiasa?
4. Je, ile mikoa inayoitwa "The Big Four" – Iringa, Mbeya, Rukwa, na Ruvuma, hadhi hii inatokana na kigezo/vigezo gani?
· Mchango wa mikoa hii minne katika uzalishaji wa mazao ya chakula (food crops)?
· Mchango wao katika uzalishaji wa Kilimo kwa ujumla (food and cash crops)?
· Mchango wao wa jumla katika Pato la Taifa (GDP)?
5. Na mwisho, Je, nini iwe kipaumbele cha taifa (budget priority) kwa mwaka huu wa fedha na hata siku za usoni?